RAIS KIKWETE AFANYA UTEUZI WA MAKATIBU WAKUU NA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA

RAIS KIKWETE AFANYA UTEUZI WA MAKATIBU WAKUU NA MAKATIBU TAWALA WA MIKOA

Like
331
0
Thursday, 06 November 2014
Local News

 

RAIS Jakaya Mrisho Kikwete amefanya uteuzi wa Makatibu Wakuu wa Wizara kwa kuteua Makatibu Wakuu wanne wapya na kuhamisha mmoja, uteuzi uliomuondoa Katibu Mkuu Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Charles Pallangyo ambaye sasa anakua Katibu Tawala wa Mkoa wa Geita.

Rais Kikwete amefanya uteuzi na uhamisho wa Makatibu Tawala wa Mikoa.

Taarifa iliyotolewa mjini Dodoma jana jioni na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue imesema kuwa Uteuzi huo ambao umeanza na Makatibu Wakuu na Makatibu Tawala wa Mikoa wanaapishwa leo, Ikulu, Dar es Salaam.

Comments are closed.