Rais Magufuli Atoa tamko la kutengewa eneo kwa Wafanyabiashara wadogo stendi mpya Dodoma.

Rais Magufuli Atoa tamko la kutengewa eneo kwa Wafanyabiashara wadogo stendi mpya Dodoma.

6
973
0
Thursday, 18 June 2020
Local News

Rais Magufuli ametoa agizo kwa Mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin Kunambi, kuhakikisha wafanyabiashara ndogondogo (Machinga), mama lishe pamoja na magari ya mizunguko mifupi jijini, (Daladala) kutengewa maeneo ya kufanya kazi katika stendi mpya ya kisasa Dodoma.

Ametoa agizo hilo Jun 18 kwa njia ya simu, baada ya Mkurugenzi kuwatembelea wafanyabiashara katika stendi hiyo na kusikiliza kero zao.

Ameongeza kuwa Mama lishe lazima wawepo, ikiwa stendi hiyo imejengwa kwaajiri ya watanzania wote wakiwepo maskin ambapo Hakuna sababu ya kuwa na stendi ya watanzania wote wa maisha yote,.

Usafiri mwingine wa daladala na pikipiki Rais amesema Nilazima jiji litengeneze mazingira, watu wa daladala wawe wanaweza kufika pale, wa bodaboda waweze kufika pale, wa pikipiki waweze kufika pale, ili kusudi hata mvua ikiwa inanyesha mtu asianze kutembea na mizigo yake, wapo wengine wagonjwa.

Aidha ametoa onyo kwa walinzi waliopewa kazi kwenye stendi hiyo kutoka Suma JKT kuacha kuwarusha watu vichura na kufanya kazi ya kuwalinda, kama wanavyofanya mikoa mingine ikiwa hapo sio jeshini wanapaswa kuwalinda .

Kwa upande wake Mkurugenzi, Kunambi ameahidi kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa ndani ya muda mfupi na kuwatafutia vijana mikopo kama ambavyo Rais ameagiza.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *