Rangi ya ngozi yako yaweza kukupa uraia nchini Liberia

Rangi ya ngozi yako yaweza kukupa uraia nchini Liberia

Like
521
0
Monday, 26 March 2018
Global News

Tony Hage ameishi Liberia kwa zaidi ya miaka hamsini.
Na ndipo mahali alipo kutana na mke wake kisha kuanzisha biashara yake yenye mafanikio.
Aliendelea kuishi Liberia katika kipindi ambacho raia wengi wa nchi hiyo wali kimbia ili kuepuka machafuko akilenga kuiona nchi anayoipenda ikipata mafanikio.
Mpaka sasa bwana Hage si raia wa Liberia, amezuiwa kupata uraia wa kudumu wa nchi hiyo kwa sababu ya rangi ya ngozi yake na asili ya familia yake kutoka huko Lebanon.
‘Tutakuwa watumwa’
Nchi ya Liberia iliyoko mashariki mwa Afrika, ilianzishwa kama makazi ya watumwa wanaorejea Afrika kutoka huko Marekani sehemu ambayo walikuwa wakinyanyasika.
Lakini cha ajabu tangu ilipo tengenezwa katiba mpya kiliwekwa kipengele cha kutoa uraia kwa watu wenye asili ya Afrika tu na kutoa kizuizi kwa watu weupe.
Miaka mingi baadae, rais mpya wa Liberia na mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu George Weah anapingana na kipengele hicho na kusema ni kitu kisicho cha lazina lakini pia ni ubaguzi.
Anaongeza kuwa ubaguzi wa rangi unaondoa kabisa tafsiri ya Liberia, neno ambalo linamaanisha uhuru.
Msimamo huo wa Rais wa Liberia umezua tafrani katika maeneo mbali mbali ya nchi hiyo.
“Watu weupe watawatawala wa Liberia weusi” mfanyabiashara Rufus amesema.

Anaamini kuwa mpango wowote ule wa kutoa nafasi za uraia kwa watu tofauti na wenye asili ya Afrika utaharibu nafasi ya wa Liberia kuendeleza nchi yao.
Pia anasema ni hatari kuruhusu watu wa nchi nyingine kuwa na umiliki wa mali huko Liberia.
Bwana Oulagbo sio mtu pekee kuweka wazi hofu yake, kundi jipya la utetezi wa raia ‘Citizen’s Action Against Non-Negro Citizenship and Land Ownership’ limejipanga kupambana na mipango ya Rais.
Kila nchi imejengwa kwa misingi maalumu, kama ukii shusha thamani misingi hiyo nchi lazima iyumbe, kiongozi wa kundi hilo Fubbi Henries ameiambia BBC.
Anaongeza kuwa Bwana Weah anatakiwa kushughulikia sera sahihi kwa wa Liberia.
“Tunahitaji kuweka biashara zetu sawa, sekta ya elimu na kilimo na si uraia au umiliki wa ardhi kwa watu weupe” amesema.
Licha ya utajiri wake wa mali asili, linapo kuja swala la wastani wa mapato kwa kila mtu Liberia ni nchi ya 225 kati ya 228 ambapo kwa mwaka 2017 pekee mtu mmoja alipata dola za kimarekani 900 tu.
Hata hivyo asilimia tatu ya pato la taifa la Liberia inatokana na wale wanaoishi nje ya nchi – na baadhi ya familia hutegemea fedha kutoka Marekani.
Lakini Bwana Weah anashutumiwa kwa kutoitathimini vyema hali hiyo anasema liberia ina hali mbaya kiuchumi na yeye anakwenda kutatua hilo.
Baada ya miaka mingi ya vita vya kiraia na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola mwaka 2014 ahadi za George Weah zimekuwa kama muziki masikioni mwa raia wa Liberia.
Kubadilishwa kwa sheria sasa ni sawa na kumweka mtoto wa miaka miwili na mtu wa miaka 45 katika ulingo wa ngumi kuona kama wanaweza pigana kwa haki. Anasema Fubbi Henries kiongozi wa kundi la kiraia.
Anasisitiza kuwa lazima mtoto wa miaka miwili ataonewa hivyo basi wa Liberia bado hawana nguvu hiyo.
Usikizano
Hofu ya watu kutoka mataifa mengine sio kitu kipya, jamii ya wa lebanoni wameizoe sasa.” Baadhi ya watu wanaweza chukulia hii kama kitisho, kwamba wageni wanakuja kuchukua fursa zetu lakini si hivyo, bwana Hage anaiambia BBC akiwa nyumbani kwake Monrovia.
Hata hivyo kuna kipindi familia za Kilebanoni zilikuwa na biashara katika maeneo mengi ya nchi, na mpaka sasa wanamiliki baadhi ya hoteli na biashara kubwa katika nchi hiyo lakini hii isiwatie hofu majirani zetu wazaliwa wa Liberia.

Hage anaamini kuwa kama pendekezo la Rais litapia, hii itafungua njia ya ushirikiano zaidi. Sasa anasherekea sikukuu yake ya kuzaliwa ya 15 akiwa ndani ya Liberia, na haja wahi kujuta kuishi Liberia.
“Nina furaha si kwa sababu sina uraia wa Liberia, ninafuraha kwa sababu Rais Weah anatazamia mwelekeo wa nchi hii”

Comments are closed.