REAL MADRID NA BORUSSIA DORTMUND ZATINGA HATUA YA 16

REAL MADRID NA BORUSSIA DORTMUND ZATINGA HATUA YA 16

Like
248
0
Wednesday, 05 November 2014
Slider

Mabingwa watetezi wa michuano ya klabu bingwa Ulaya klabu ya Real Madrid imefanikiwa kutinga katika hatua ya 16 bora ya michuano hiyo kwa kuilaza klabu ya Liverpool kwa goli 1-0.

Goli la Real limefungwa na mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Karim, Benzema aliyeunganisha krosi safi iliyojazwa na beki wa kushoto wa Brazil Marcelo.

Mechi hiyo iliyokuwa inatazamiwa kuwa ya kipekee kwa mchezaji Cristiano Ronaldo aliyekuwa anafukuzia rekodi ya ufungaji magoli 71 iliyowekwa na Raul Gonzalenz, alishindwa kutamba mbele ya beki KoloToure aliyeonekana kumbana vilivyo.

Wakati huohuo klabu ya Borussia Dortmund nayo imefanikiwa kukata tiketi ya hatua ya 16 bora baada ya kupata ushindi mnono wa magoli 4-1 dhidi ya Galatasaray.

Matokeo mengine ya michezo ya jana 5/Nov/2014

Arsenal 3-3 Anderlecht

Juventus 3-2 Olympiacos Piraeus

Malmo FF 0 vs 2 Atletico Madrid

FC Basel 4 vs 0 Ludogorets

Benfica 1 vs 0 Monaco

Zenith 1 vs 2 Bayer Leverkusen

Comments are closed.