Sayari ambayo iko karibu na nyota imegunduliwa na wanasayansi

Sayari ambayo iko karibu na nyota imegunduliwa na wanasayansi

Like
1113
0
Thursday, 15 November 2018
Global News

Wataalamu wa elimu ya sayansi wamegundua sayari ambayo inazungua karibu kabisa na nyota pamoja na jua.

Sayari kama hizi zina uwezekana kuwa na malengo muhimu katika kutafuta ishara ya maisha ya kizazi kijacho kuona mbali.

Ukubwa wa sayari hizo zinafikiriwa kuwa mara tatu zaidi ya dunia, huku dunia imewekwa katika kiwango cha ubora zaidi duniani.

Guillem Anglada Escudé na wenzake waliandika katika jarida la ‘Nature’ na kusema kwamba wamegundua sayari yenye ukubwa mara tatu zaidi ya dunia.

” Tunafikiri kwamba hizi ndizo sababu ambazo zinatoa sifa na kuna uwezekano kwamba sayari nyingi za miamba ziko juu ya anga.

Sayari hizi zina utajiri mkubwa wa mvuke unaotokana na maji, gesi ukaa na vitu vingine vinavyolingana na hiyo.

Jua liko karibu

Mfano wa karibu zaidi ni mionzi ya jua ambayo inadhaniwa kuepo katika mwezi wa ‘Saturn’ ambao unajulikana kama Titan.

Mwezi huo umetengenezwa na majimaji. Na wakati mwingine maji ya mvua na maziwa yanatokana na gesi asilia kutoka katika sayari hiyo.

Sayari ya nyota ya Barnard iko mbali na nyota kama lilivyo jua na sayari ya Mekuri .

Hii ni sayari ambayo iko karibu na dunia baada ya Proxima ambayo ilitangazwa kugundulika mwaka 2016.

Nyota ya Bernard haina mwanga wa kutosha , mwanga wake unaokaribia kuwa na asilimia 3 ya mwanga wa jua.

Sayari ambayo inajulikana kuwa na theluji, ambapo katika tamaduni za zamani lilikuwa eneo ambalo maji yalibaki kuwa kimiminika katika uso wa dunia.

Kiwango chake cha joto kinakadiriwa kuwa na nyuzi joto 150 katika uso wa dunia.

Hata hivyo hali yake ya hewa inaweza kuleta joto na kufanya hali ya hewa kuwa nzuri zaidi.

“Tunaweza kufanya jaribio moja ambalo linaweza kubaini utofauti wake, hivyo tutajumuisha taarifa zote kwa makini.

Tumebaini kuwa kuna makosa mengi yanayotokana na vifaa mbalimbali ambavyo vilitumika.

Hii haimaniishi kuwa tunalenga kupata takwimu mpya lakini tunataka watu waelewe namna ambavyo mfumo unaathirika.

Kitu pekee ambacho tumekifanya ni kuonesha ishara kuwa na uhakika na zenye uhalisia” alieleza mtaalamu wa sayansi ya anga kutoka chuo kikuu cha Queen Mary kilichopo London .

Kizazi kijacho kinaweza kuja kuangalia kwenye mtandao vilevile wanasayansi wataweza kuonesha kutofautisha vitu ambavyo vinapatikana katika sayari.

Hii itajumuisha gesi kama oksijeni kibailojia.

Sio mara ya kwanza kwa sayari kudaiwa kuwa iko karibu ya nyota ya Barnard.

Mwaka 1960, mwanasayansi Peter van de Kamp, anayefanya kazi nchini Marekani amechapisha ushaidi wa nyota hiyo.

Hata hivyo madai ya van de Kamp yanadai kuwa na utata kwa sababu wanasayansi wengine walishindwa kupata matokeo kama yake.

Inawezekana kuwa ni vigumu kwa Peter van de Kamp kuthibitisha.

Ishara inaweza kuwa ndogo sana kutokana na mbinu aliozotumia, Guillem Anglada Escudé alisema.

Hatahivyo taarifa mpya inajumuisha viashiria vya sayari ya pili ya nyota ya Barnard ambayo haifanaishwi kabisa na dunia.

Taarifa mpya zinaonyesha ushaidi wa uwepo wa sayari hiyo kuwepo kwa muda mrefu.

cc;BBC

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *