Serikali ‘yakaza buti’ mzozo wa korosho

Serikali ‘yakaza buti’ mzozo wa korosho

1
553
0
Monday, 12 November 2018
Local News

Rais John Magufuli

Rais John Magufuli amesema kwamba kuanzia Jumatatu wanunuzi wa korosho hawaruhusiwi tena kununua bidhaa hiyo kutoka kwa wakulima.

Serikali sasa iko tayari kununua korosho hizo kwa gharama ya shilingi 3,300 badala ya shilingi 3000 za kitanzania ambayo ni sawa na dola 1.4.

Na kukabidhi rasmi kwa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kuzichukua korosho hizo.

Mzozo huu wa korosho umekuwa gumzo kubwa kwasababu korosho zina umuhimu mkubwa kutokana na kuwa usafirishaji wake katika nchi za nje ndio mojawapo ya kitega uchumi nchini.

Pamoja na uamuzi huo, rais Magufuli ametangaza kukitaifisha kiwanda kimoja cha korosho kilichokuwa kiamilikiwa na mtu binafsi kinachofaamika kama ‘Bucco’ na kuwakabidhi wanajeshi.

Amesema kiwanda hicho kina uwezo kwa kutengeneza korosho mpaka kilo 20 elfu kwa mwaka hivyo hizo tani hizo 70 elfu ni kidogo sana kazi za wanajeshi.

“Na kuanzia leo wanajeshi inabidi wakakizingire na wakishindwa na kupewa watu wengine” Rais Magufuli amesisitiza.

Soko la Korosho Kimataifa

Rais Magufuli ameongeza kwa kusisitiza kuwa ameangalia soko la korosho na korosho za Tanzania ni za kiwango cha juu.’

Kwa upande wao wakulima,bbc ilizungumza na mmoja wa mfanyabiashara na mkulima wa zao la korosho ambaye alisifu umuhimu wa korosho katika uchumi wa mkoa wa Mtwara.

Alibainisha kwamba korosho inatoa ajira za muda katika mkoa huo lakini mfumo uliokuepo ulikuwa unarudisha nyuma mauzo na kuwafanya wakulima kushindwa kupata faida.

Na kwa upande wao wanunuzi wa zao hilo walishindwa kufikia bei ambayo wangeweza hata kuuuza mwaka jana.

Mnamo mwezi Juni mjadala mkali ulizuka nchini Tanzania kuhusu mapendekezo ya bajeti ya mwaka 2018 /2019 katika zao la korosho. Mapendekezo hayo ni pamoja na kuondolewa kwa ruzuku ya asilimia 65 iliyokuwa inaenda kwenye Mfuko wa Maendeleo wa Korosho na badala yake, iende kwenye mfuko mkuu wa serikali.

Chama cha ushirika kilibainisha tatizo lililopo la teknolojia ya kunyunyizia na utegemezi wa pembejeo kutoka nje.

Kwa takribani miaka 10, korosho imekuwa zao lililoleta matokeo chanya ambapo tangu mwaka 2007/08 bei ilikuwa shilingi 250 mpaka 500 kwa kilo ila sasa hivi wastani ni shilingi 3000 mpaka 5000 kwa kilo.

Msimamo wa serikali kuhusu bei ya korosho

Ingawa mwezi Oktoba tarehe 28, 2018 baada ya serikali ya Tanzania kufanya mazungumzo na wanunuzi wa zao la korosho, Serikali ililazimika kuchukua hatua ya kuwalazimisha wanunuzi kununua korosho hizo na hata kutishia kuwafutia leseni wafanyabiashara hao.

Katika mazungumzo hayo Serikali iliungana na msimamo wa wakulima wa korosho wa kukataa bei ya kati ya shilingi 1,900 hadi 2,700 kwa kilo, na hivyo kukubaliana kuwa korosho zitanunuliwa kwa bei isiyopungua shilingi 3,000 kwa kilo.

Na mtaalamu wa uchumi na biashara nchini Tanzania, Johakim Bonaventure anasema serikali imeamua kutekeleza sera ya kuweza kuhodhi ile kodi ya kuuza nje, mwanzoni ilikuwa inahozi kwa asilimia 35 ya kipato hicho lakini sasa hivi imechukua na ile asilimia 65.

‘Ni jambo jema lakini kiuchumi kuna mambo kadhaa ambayo yanaweza kuwa yameandamana nayo na mojawapo ni kupunguza uwezo wa vyombo vinavyosimamia mazao sio korosho pekee yanayolimwa katika baadhi ya maeneo.’

Mtaalamu huyo amesema kama zao la korosho likiweza kuathirika basi pato linaweza kuathirika pia.Bado kuna uwezekano wa kukaa chini kuangalia faida na hasara.

Mwaka jana zao la korosho limeweza kuleta mapato makubwa katika taifa na sasa linatangazwa kuanzishwa katika maeneo mengine 17.

cc;BBCswahili

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *