SHAMBULIO LAUA WANAFUNZI 47

SHAMBULIO LAUA WANAFUNZI 47

Like
254
0
Monday, 10 November 2014
Global News

IMEELEZWA kuwa, shambulizi limetokea katika shule moja ya upili wakati wanafunzi wakiwa wamekusanyika shuleni humo mjini Potiskum Kaskazini Mashariki mwa Nigeria.

Duru zinasema kuwa wanafunzi 47 wameuawa katika shambulizi hilo linalosemeklana kufanywa na mshambuliaji wa kujitoa mhanga ambaye alikuwa amevalia sare za shule.

Shambulizi lilitokea wakati wanafunzi wakiwa wamekusanyika wakati wa asubuhi. Mji wa Potiskum ambapo shule hiyo ipo, umekuwa kitovu cha mashambulizi ambayo yamekuwa yakifanywa na Boko Haram.

NIGERIA

 

 

Comments are closed.