Taifa Stars Yajiliwaza kwa DRC Congo, Yaifunga Mabao 2-0

Taifa Stars Yajiliwaza kwa DRC Congo, Yaifunga Mabao 2-0

Like
695
0
Wednesday, 28 March 2018
Sports

Taifa Stars imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo katika mchezo wa kirafiki uliopigwa jana.

Stars ilifunga mabao yake kipindi cha pili baada ya kile cha kwanza kwenda suluhu ya 0-0  kupitia kwa Mbwana Samatta na Shiza Ramadhan Kichuya.

Stars ilipata ushindi huo ikiwa imetoka kupoteza mchezo uliopita dhidi ya Algeria kwa jumla ya mabao 4-1 huko Algiers.
Kocha wa Taifa Stars, Mayanga ameeleza kuwa mchezo huo ulikuwa vizuri kutokana na vijana wake kuonesha nidhamu na kuwa imara zaidi kwenye safu ya ulinzi, kitu ambacho kilipelekea wapinzani washindwe kupata bao.

Aidha, Mayanga amesema Congo walishindwa kuisumbua Stars kutokana na kuwa wazito miguuni na kuwapa faida Stars kupata mabao hayo mawili.

Comments are closed.