Teknolojia ya VAR yaibeba Italia dhidi ya Uingereza

Teknolojia ya VAR yaibeba Italia dhidi ya Uingereza

Like
459
0
Wednesday, 28 March 2018
Sports

Teknolojia ya video (VAR) imeibeba timu ya taifa ya Itali kufanikiwa kuchomoza na sare ya bao 1 – 1 dhidi ya Uingereza mchezo wa kirafiki.

Wakati Uingereza ikifanikiwa kuongoza mchezo huo baada ya kupata bao lake dakika ya 26 kupitia kwa Jamie Vardy kunako dakika ya 87 mchezaji wa Itali, Lorenzo Insigne akaisawazishia timu hiyo kwa msaada wa teknolojia ya VAR huko Wembley.

Timu ya taifa ya Uingereza ilikuwa ikitarajia kupata ushindi wake wa pili baada ya kuifunga Netherlands kwa bao 1-0 lakini mwamuzi wa mchezo huo Deniz Aytekin aliamuru penati na kuifanya Italia kusawazisha na kumalizika kwa sare ya 1 – 1 baada ya kupitia VAR.

Kikosi cha Uingereza: Butland (6), Young (7), Walker (7), Stones (6), Tarkowski (6), Trippier (7), Dier (7), Oxlade-Chamberlain (7), Sterling (8), Lingard (7), Vardy (7).

Wachezaji wa akiba: Rose (6), Lallana (6), Rashford (6), Cook (6), Henderson (6).

Kikosi cha Italia: Donnarumma (7), Zappacosta (6), Rugani (6), Bonucci (6), De Sciglio (7), Pellegrini (6), Jorginho (7), Parolo (6), Candreva (6), Immobile (6), Insigne (7).
Wachezaji wa akiba: Chiesa (7), Belotti (6), Gagliardini (6).

Kwenye mchezo huo uliyokuwa na kasi na ushindani mkubwa aliyeibuka nyota wa mchezo ni Raheem Sterling

 

Comments are closed.