TOM CRUISE AKANA KUMTENGA MWANAE

TOM CRUISE AKANA KUMTENGA MWANAE

Like
170
0
Tuesday, 07 April 2015
Entertanment

Tom Cruise amesema hakupata nafasi ya kukutana na mtoto wake kwa takribani mwezi sasa kufuatia kubanwa na ratiba kikazi ambapo kwa maelezo aliyoyatoa star huyo amedai hali hiyo imetokana na kuwa busy na kushoot filamu ya “Mission Impossible 5” huko London. Hivyo yalibaki masaa kadhaa aweze kukutana na binti yake Suri. Ila chanzo kinadai kuwa muigizaji huyo alikuwa mapumzikoni kwa takribani wiki mbili mara baada ya ratiba ya kushoot kufungwa lakini hakwenda kumtazama mwanae.

 

Chanzo cha karibu na Katie Holmes kimezungumza na mtandao wa Tmz kuwa Tom hajamtembelea mwanae mwenye mwenye umri wa miaka 8 kwa takribani mwaka mmoja sasa.

 

Mwakilishi wa muigizaji huyo amekana taarifa hizo na kusema sizakweli kwani Tom amekuwa akimtembelea mtoto mara kadhaa hivi karibuni ila kwa kiwango cha chini akiwa na dhamira yakumuepusha na Camera za mapaparazi.

 

Chanzo cha karibu na Katie Holmes kimekana taarifa hiyo ya msemaji wa Tom nakusema muigizaji huyo anajitenga nao

Comments are closed.