WAHU ATANGAZA KUVUNJA UKIMYA

WAHU ATANGAZA KUVUNJA UKIMYA

Like
172
0
Tuesday, 07 April 2015
Entertanment

Mkali kutoka code ya 254 kwa Uhuru Kenyata Wahu ni miongoni mwa wasanii wachache Afrika Mashariki walioweza kudumu kwenye tasnia ya muziki kwa zaidi ya muongo mmoja.

Kumekuwa na kimya kirefu kwa msanii huyu toka afanye vizuri na wimbo wake wa still a liar kwenye vituo tofauti vya redio na tv.

Kufuatia ukimya huo maswali yamekuwa mengi kwenye mitandao ya kijamii kwa mashabiki wake kutaka kufahamu iwapo kama ameachana kabisa na muziki na haya ni majibu yake.

‘’j_doctor did you withdraw from the music industry???? just thinking…

wahukagwi @vj_doctor I’m a housewife now!! jus kidding…took a break to concentrate on family and other business ventures, but releasing something real soon!!’’

mmoja wa mashabiki aliuliza iwapo kama msanii huyu ameacha kabisa muziki ndipo alipojibu kwa utani kuwa yeye ni mama wa nyumbani kwa sasa kisha akatoa maelezo kwa kina baada ya kusema kuwa huo ni utani

Wahu ameeleza kuwa aliamua kupumzika kwa muda ili kujishughulisha na mambo ya kifamilia ikiwa ni pamoja na biashara lakini mashabiki wake watarajie ujio mpya wa msanii huyo

Comments are closed.