Trump ‘hakusuka njama na Urusi’ kushinda uchaguzi

Trump ‘hakusuka njama na Urusi’ kushinda uchaguzi

Like
467
0
Monday, 25 March 2019
Global News

Kampeni iliyoendeswa na rais wa Marekani Donald Trump ‘haikushirikiana na Urusi wakati wa uchaguzi wa 2016, kwa mujibu wa muhtasari wa ripoti ya ya mwanasheria mahususi Robert Mueller iliyowasilishwa kwenye bunge la Congress ,Jumapili.

Muhtasari wa ripoti haukuelezea ikiwa Bwana Trump alizuia utekelezwaji wa sheria – lakini pia haikumuhusisha rais na madai hayo.

Ripoti hiyo iliwekwa kwa muhtasari kwa ajili ya Congresi na Mwanasheria Mkuu, William Barr.

Trump alituma ujumbe wa twitter kujibu muhtasari wa ripoti yake akisema: ” hakuna ushirikiano, hakuna kuzuia sheria.”

Rais Trump, ambaye mara kwa mara aliuelezea uchunguzi kama ”uwindaji wa kichawi”, alisema Jumapili kwamba “ni aibu kwamba nchi ililazimika kupitia hili”, akiuelezea uchunguzi dhidi yake kuwa “kuangushwa kwa jambo lililo kinyume cha sheria “.

Ripoti hiyo inakamilisha uchunguzi wa miaka miwili wa Bwana Mueller, ambapo wakati wa uchunguzi huu washirika wa karibu wa rais walishitakiwa, na wakati mwingine hata kufungwa.

“Japo ripoti hii haionyeshi kuwa rais alifanya uhalifu, haimuweki huru ,”Bwana Mueller aliandika katika ripoti yake.

Kile kilichomo kwatika muhtasari wa ripoti

Barua ya muhtasari wa ripoti hiyo ya Bwana Barr inaainisha matokeo ya uchunguzi unaohusiana na juhudi za Urusi za kushawishi matokeo ya uchaguzi wa 2016.

Bwana Barr alihitimisha ripoti yake kwa kusema: “Mchunguzi maalum hakumpata Trump, mtu yeyote wa Marekani au afisa wa kampeni ya Trump na hatia ya kushirikiana au kwa kufahamu kuratibu ushirikiano wowote na Urusi .”

Sehemu ya pili ya barua hiyo ilizungumzia suala la kuzuwia utendaji wa sheria . Muhtasari wa Bwana Barr unasema ripoti wa mchunguzi mkuu “Hatimae haimuweki katika nafasi ya kushtakiwa “.

Uchunguzi wa Robert Mueller umechukua takribani miaka miwili

“Kwa hiyo baraza la uchunguzi halikutoa hitimisho – kwa njia moja au nyingine- juu ya ikiwa mienendo iliyochunguzwa ilikuwa ni ya kuzuwia utendaji wa kisheria ,”ilielezea barua hiyo.

Bwana Barr anasema kuwa ushahidi haukutosha “kubaini kwamba rais alitenda kosa la kuzuwia utendaji wa washeria “.

Bwana Barr alikamilisha barua yake kwa Congresi kwa kusema kuwa atafichua mengi zaidi katika ripoti kamili , lakini akasema baadhi ya yanazuwiwa kutangazwa.

“Kutokana na masharti hayo , mpango wa mchakato wa ripoti hiyo utategemea kwa upande mmoja juu ya namna wizara ya mambo ya nje itakavyoweza haraka kubaini yaliyopendekezwa na jopo kuu la mahakama ambayo kw amujibu wa sheria hayapaswi kutangazwa kwa umma ,” aliandika.

” Nimeomba msaada wa mchunguzi mkuu katika kutambua taarifa zote zilizomo kwenye ripoti haraka iwezekanavyo .”

Walichosema wanasiasa wa marekani kuhusu Muhutasari wa ripoti

Mjumbe wa Congresi Jerry Nadler, ambaye ni mwenyekiti wa tume ya sheria wa Democratic katika bunge la wawailishi, alisisitiza kuwa mwanasheria mkuu hakusema moja kw amoja kwamba Trump alizuwia utendaji wa sheria .

“Barr anasema kwamba rais huenda alizuwia uutekelezwaji wa sheria, lakini kupatikana na hatia hiyo , ‘serikali itahitaji kutoa ushahidi wa kutosha kwamba mtu alifanya hivyo kwa kukusudia, au kuhusika katika mwenendo wa kuzuwia utekelezwaji wa sheria’.”

Seneta wa Democratic Richard Blumenthal, ambaye ni mjumbe wa kamati ya Seneti ya sheria, alisema kwamba japo ushahidi ulikosa wa “kushtakiwa kwa uhalifu wa kushirikiana “, bado maswali yanabakia juu ya ikiwa Bwana Trump alihusika.

Katika taarifa ya pamoja , Spika wa bunge kutoka chama cha Democratic Nancy Pelosi na kiongozi wa wabunge wa Democratic katika seneti Chuck Schumer walisema barua ya Bwana Barr ” inaibua maswali mengi kama inavyoyajibu” na wakatoa wito wa ripoti kamili kutolewa.

“kwa rais kusema yuko huru kabisa inakwenda kinyume kabisa na maneno ya Bwana Mueller na maneno yake hayapaswa kuchukuliwa kuwa ni ya kuaminika ,” ilisema taarifa yao.

Afisa habari wa ikulu ya White House Sarah Sanders alielezea matokeo ya uchunguzi huo kuwa “ya kumuweka huru kwa jumla rais”.

Wakili wa Trump, Rudy Giuliani, alisema ripoti “ilikuwa bora kuliko nilivyotarajia “. Nae Seneta wa Republican Mitt Romney aliafiki “habari njema “, akituma ujumbe wake wa twitter kwamba ”Ni wakati wa taifa kusonga mbele “.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *