UFARANSA YAANZA VIZURI KOMBE LA DUNIA DHIDI YA AUSTRALIA

UFARANSA YAANZA VIZURI KOMBE LA DUNIA DHIDI YA AUSTRALIA

Like
429
0
Saturday, 16 June 2018
Slider
Ufaransa imefanikiwa kuibuka na ushindi wake wa kwanza katika michuano ya Kombe la Dunia mwaka huu nchini Russia wa mabao 2-1 dhidi ya Australia.
Mabao ya mchezo huo yametiwa kimiani na Antoine Griezmann katika dakika ya 58 kwa njia ya mkwaju wa penati na la pili likitiwa kimiani na Paul Pogba (80′).
Bao pekee la Australia liliwekwa wavuni na Mile Jedinak mnamo dakika ya 62 kwa mkwaju wa penati.
Mechi hii imekuwa ya kwanza kushuhudiwa penati mbili ndani ya dakika 90 zikipigwa kwa pande zote.
Ushindi huu wa Ufaransa unawapa alama tatu muhimu kwenye kundi C ambapo baadaye Peru na Denmark watakuwa wanacheza pia kutoka kundi hilo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *