Uingereza yaipatia Tanzania Sh307 bilioni

Uingereza yaipatia Tanzania Sh307 bilioni

Like
317
0
Friday, 10 August 2018
Local News

Serikali ya Uingereza imetoa msaada wa Sh 307.5 bilioni kwa Tanzania ikiwa ni sehemu ya kumuunga mkono Rais John Magufuli katika elimu, mapambano dhidi ya rushwa na uboreshaji huduma za afya.

Msaada huo umetangazwa leo Ijumaa Agosti 10, 2018 na Waziri wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza, Penny Mordaunt alipokutana na kufanya mazungumzo na Rais Magufuli Ikulu jijini Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa leo na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa, inasema kuwa Mordaunt amesema fedha hizo zimetolewa kuunga mkono vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Tano.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *