Wallace Karia; mchezo wa October 12 ni Muhimu sana

Wallace Karia; mchezo wa October 12 ni Muhimu sana

Like
492
0
Saturday, 06 October 2018
Local News

“Mchezo wa October 12 ni muhimu sana kabla ya October 16, 2018 kwa hiyo sasa hivi tuangalie wa October 12 kwa sababu inabidi tukacheze kule Cape Verde halafu October 16 tunamalizia hapa Wallace Karia, Rais TFF.
Watanzania waiunge mkono Taifa Stars, Waziri Mwakyembe na serikali yetu kwa kuchangia lakini mchango huo ni nauli yao wenyewe ya kuwafikisha Cape Verde.

Cape Verde tutakwenda kwa mambo mawili, tangu ndege yetu imenunuliwa mipango yake ilikuwa ni kuwa na safari za nje ya nchi. Hii itakuwa safari yake ya kwanza nje ya nchi kwa hiyo tutaweka historia lakini tutaweka historia kwenda kuishangilia timu yetu na tuweke historia ya kupata ushindi kule.

Tutaondoka October 9 usiku na alfajiri ya October 10 tutakuwa tumefika Cape Verde na jioni wachezaji watafanya mazoezi, baada ya mchezo wa October 12, usiku tutaondoka kurudi nyumbani.

Kikubwa ni kwamba, ndege haitaweza kuondoka kama haitakuwa na watu wa kutosha. Ndege ina viti 22 vya Business class ambapo tayari viti 15 vimeshalipiwa, viti 31 vya Economy class vimeshalipiwa kwa ajili ya wachezaji na benchi la ufundi.”

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *