Watu 1000 wahofiwa kufariki kutokana na kimbuga Msumbiji

Watu 1000 wahofiwa kufariki kutokana na kimbuga Msumbiji

Like
1059
0
Tuesday, 19 March 2019
Global News

Idadi ya watu waliofariki kutokana na kimbunga Idai nchini Msumbiji sasa huenda ikawa ya juu na kufikia watu 1000 rais Filipe Nyusi amesema.

Bwana Nyusi alisafiri kwa ndege katika maeneo yalioathirika zaidi siku ya Jumatatu. Alielezea kuona miili ikielea juu ya mito.

Tayari kuna hatari ya maisha ya zaidi ya watoto 100,000 na watu wazima kufuatia kikmbunga hicho huku mito katika maeneo yaliothirika zaidi ikivunja kingo zake , kulingana na shirika la Save the Children.

Mafuriko yaliofanyika mapema mwezi huu yamezidishwa na kimbunga Idai ambacho kilikumba eneo la kaskazini mwa Msumbiji mnamo tarehe 15 mwezi Machi 2019 na kusababisha unahiribifu mkubwa wa nyumba , shule, hospitali na miundo mbinu.

Kulingana na serikali ya Msumbiji takriban watu 600,000 wameathiriwa , huku maisha ya zaidi ya watu 1000 yakidaiwa kupotea huku yale ya watu 100,000 yakihitaji msaada wa dharura mjini Beira.

Kiwango cha janga hilo kinazidi kuongezeka kila dakika na shirika la Save the Children lina wasiwasi mkubwa kuhusu watoto na familia walio katika hatari huku viwango vya mafuriko vikizidi kuongezeka anasema Machel Pouw mkuu wa operesheni ya shirika hilo nchini Msumbiji.

Save the Children ni mwanachama wa COSACA wakishirikiana na shirika la OXFAM pamoja na lile la CARE na linafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na serikali pamoja na taasisi za usimamizi wa majanga ili kuwasaidia watoto walioathirika

Kimbunga hicho kilishuka katika mji wa bandari wa Beira siku ya Alhamisi kikiwa na upepo wenye kasi ya hadi kilomita 177 kwa saa , lakini mashirika ya misaada yalifika katika eneo hilo siku ya Jumapili.

Mfanyikazi mmoja wa Umoja wa mataifa aliambia BBC kwamba kila nyumba mjini Beira- ambapo ni mji wenye makaazi ya watu nusu milioni iliharibiwa.

Gerald Bourke, kutoka kwa shirika la chakula duniani , alisema: Hakuna nyumba ambayo haikuathiriwa . hakuna Umeme, hakuna mawasiliano.

Barabara zimejaa magogo ya nyaya za umeme. Paa za nyumba zimeanguka pamoja na nyuta zake. raia wengi wa mji huo wamepoteza makaazi yao.

Idadi rasmi ya watu waliofariki nchini Msumbiji inadaiwa kuwa watu 84 kufuatia mafuriko na upepo mkali.

Kimbunga hicho kimewaua takriban watu 180 katika eneo lote la Afrika Kusini.

Shirika la msalaba mwekundu limeelezea uharibifu huo kuwa mbaya zaidi na wa kutisha. Watu wamelazimika kuokolewa wakiwa juu ya miti , Jamie LeSeur mkuu wa IFRC aliambia BBC.

Nchini Zimbabwe takriban watu 98 wamefariki huku 217 wakiwa hawajulikani waliko mashariki na kusini serikali imesema.

Idadi ya watu waliofariki inashirikisha wanafunzi wawili wa shule ya St Charles Lwanga katika wilaya ya Chimanimani, ambao walifariki baaada ya bweni lao kuathiriwa kutokana na mawe yaliosombwa na maji hayo katika mlima.

Malawi pia nayo iliathiriwa vibaya . Mafuriko nchini humo yaliosababishwa na mvua kabla ya kimbunga hicho kuwasili yalisababisha mauaji ya vifo 122 kulingana na mitandao ya mashirika ya misaada.

Serikali ya Uingereza inasema kuwa itatoa msaada wa kibinaadamu wenye thamani ya £6m kwa Msumbiji na Malawi.

Pia imesema kuwa itatuma mahema pamoja na maelefu ya mahema nchini Msumbiji.

Uharibifu wa Beira ni mkubwa kiasi gani?

Wengi wa wale wanaojulikana kufariki waliuawa karibu na mji wa Beira , ambao ndio mji mku wa nne kwa ukubwa ukiwa na idadi ya watu isiopungua nusu milioni kulingana na mamlaka.

Zaidi ya watu 1500 walijeruhiwa na miti pamoja na vifusi vilivyoanguka ikiwemo paa , kulingana na maafisa katika mji mkuu wa Maputo waliozunguzma na BBC.

”Karibu kila kitu kimeathiriwa na janga hili” , Alberto Mondlane , gavana wa mkoa wa Sofala unaoshirikisha Beira alisema siku ya Jumapili. Tuna watu wanaotaabika kwa sasa , wengine juu ya miti na wanahitaji sana msaada.

Barabara inayounganisha Beira na maeneo mengine ya taifa hilo iliharibiwa vibaya, lakini usafiri wa ndege hadi maeneo yalioathirika pakubwa umeanzishwa.

Rais Filipe Nyusi alikata ziara yake ya Swaziland ili kutembelea maeneo yalioathirika.

Manusura katika hospitali moja katika wilaya ya Chimanimani walizungumza kuhusu vile mafuriko hayo yalivyoharibu nyumba zao na kuwasomba wapendwa wao.

”Hadi sasa sijui ni wapi mwangu yupo” , Jane Chitsuro aliambia shirika la habari la AFP . ”hakuna samani , hakuna nguo ni vifusi na mawe pekee’.

Nyumba ya Praise Chipore pia nayo iliharibiwa .

”Mwanangu alikuwa nami kitandani akasombwa na mafuriko huku mafuriko makubwa yakinisomba mie pia”, alisema.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *