Watu 55 wafariki katika ajali ya basi Kenya wakielekea Kisumu, Magufuli atuma rambirambi

Watu 55 wafariki katika ajali ya basi Kenya wakielekea Kisumu, Magufuli atuma rambirambi

Like
631
0
Thursday, 11 October 2018
Local News

Watu 55 wamefariki dunia nchini Kenya baada ya basi walilokuwa wakisafiria kupata ajali kwenye barabara kuu ya Nairobi-Kisumu.

Walioshuhudia wanasema kuwa ajali hiyo ilitokea leo mwendo wa saa kumi na moja alfajiri.

Ajali hiyo mbaya ilitokea katika eneo la Fort Ternan Kaunti ya Kericho.

Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli ni miongoni mwa waliotuma salamu za rambirambi kwa Wakenya.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *