Winnie Mandela afariki dunia Afrika Kusini akiwa na miaka 81

Winnie Mandela afariki dunia Afrika Kusini akiwa na miaka 81

Like
858
0
Tuesday, 03 April 2018
Local News

Winnie Mandela, mke wa zamani wa Nelson Mandela, ambaye pia alipigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na miaka 81.
Habari za kifo chake zimethibitishwa na msaidizi wake.
Winnie alizaliwa mnamo 26 Oktoba mwaka 1936, na ingawa yeye na mumewe – Nelson Mandela – walitalikiana mapema miaka ya 1990, Winnie Madikizela Mandela kama alivyofahamika rasmi alisalia kutoa mchango katika maisha ya Bw Mandela.
Alikuwepo na walishikana mikono alipokuwa akiondoka gerezani baada ya kufungwa kwa miaka 27.
Lakini maisha yake pia yalikumbwa na utata.
Msemaji wa familia Victor Dlamini amesema kupitia taarifa kuwa: “Amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu, ambapo amekuwa akiingia na kutoka hospitalini mara kwa mara tangu mwnazo wa mwaka.
“Alifariki kwa amani mapema Jumatatu adhuhuri akiwa amezungukwa na familia na wapendwa wake.”
Askofu mstaafu na mshindi wa tuzo ya Nobel Desmond Tutu amemsifu kama “ishara kuu ya vita dhidi ya ubaguzi wa rangi,” kwa mujibu wa AFP.
Winnie alikuwa na miaka 20 hivi pale alipojipata katika siasa.
Alisomea kazi ya utoaji huduma za kijamii na haraka aliyazoea maisha ya kuwa mama na mwanasiasa.
Katika kipindi chote cha miaka 27 mumewe alipokuwa gerezani bila matumaini ya kuachiwa huru kutokana na hukumu ya kifungo cha maisha jela alichopewa mwaka 1964, Bi Winnie alilazimika kubeba jukumu la ulezi wa watoto na pia kuendeleza kampeni za kisiasa kutaka mashujaa wa kupigania nchi yao waachiwe huru hasa mumewe.
“Kamwe hatutapoteza matumaini na watu wangu hawatapoteza matumaini kamwe, bila shaka tunatarajia kwamba kazi itaendelea,” alisema wakati huo.
Kutokana na hayo Bi Winnie Mandela alilazimishwa kusalia tu huko Brandford katika jimbo lao la Orange Free katika miaka ya 70 baada ya operesheni mojawapo za kupambana na ubaguzi wa rangi zilizokuja kujulikana zaidi kama the Soweto Uprising.

Kama ilivyomtokea mumewe, Bi Winnie alifungwa gerezani, na hata kuwekwa katika kizuizi cha pekee yake ambacho ni mojawapo ya vifungo vigumu zaidi gerezani vinavyowaathiri wafungwa kisaikolojia.
Lakini baada ya kuachiwa kwake mtindo wa mapambano yake dhidi ya ubaguzi wa rangi ulianza kupata sifa mbaya hasa pale alipoonekana kuendekeza tabia ya kuwavisha tairi shingoni wale waliolengwa kwa tuhuma za usaliti na kisha kuwachoma moto.
“Kwa ‘mikufu yetu’ tutaikomboa nchi hii,” alizoea kusema.
Mambo yalizidi kumwendea mrama kutokana na matendo ya baadhi ya walinzi wake katika kile kikundi kilijulikana kama the Mandela United Football Club.
Walipatikana kuhusika katika kitendo cha kumteka nyara na kumuua kijana mmoja mwenye umri wa miaka 14 aitwae Stompie Moeketsi -kwa tuhuma za kwamba alikuwa akitoa siri kwa maadui zao.
Japo Bi Winnie Mandela aliepuka hukumu ya kifungo jela – baadaye tume ya ukweli na maridhiano iliyoongozwa na askofu Desmond Tutu, iliyokuwa inachunguza ukweli kuhusu matendo tata katika vita dhidi ya ubaguzi wa rangi na kutafuta maridhiano, ilimpata Bi Mandela na hatia ya kutowajibika kisiasa wala kimaadili wakati wa kitendo hicho.

Winnie Mandela mkutano mkuu wa ANC 54th ANC Johannesburg.Haki miliki ya pichaAFP
Image caption
Winnie Mandela alidumisha uhusiano na mumewe wa zamani licha yao kutalikiana mwaka 1996
Winnie Mandela, mke wa zamani wa Nelson Mandela, ambaye pia alipigana dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi Afrika Kusini amefariki dunia akiwa na miaka 81.
Habari za kifo chake zimethibitishwa na msaidizi wake.
Winnie alizaliwa mnamo 26 Oktoba mwaka 1936, na ingawa yeye na mumewe – Nelson Mandela – walitalikiana mapema miaka ya 1990, Winnie Madikizela Mandela kama alivyofahamika rasmi alisalia kutoa mchango katika maisha ya Bw Mandela.
Alikuwepo na walishikana mikono alipokuwa akiondoka gerezani baada ya kufungwa kwa miaka 27.
Lakini maisha yake pia yalikumbwa na utata.
Msemaji wa familia Victor Dlamini amesema kupitia taarifa kuwa: “Amefariki baada ya kuugua kwa muda mrefu, ambapo amekuwa akiingia na kutoka hospitalini mara kwa mara tangu mwnazo wa mwaka.
“Alifariki kwa amani mapema Jumatatu adhuhuri akiwa amezungukwa na familia na wapendwa wake.”
Askofu mstaafu na mshindi wa tuzo ya Nobel Desmond Tutu amemsifu kama “ishara kuu ya vita dhidi ya ubaguzi wa rangi,” kwa mujibu wa AFP.
Winnie alikuwa na miaka 20 hivi pale alipojipata katika siasa.
Alisomea kazi ya utoaji huduma za kijamii na haraka aliyazoea maisha ya kuwa mama na mwanasiasa.
Katika kipindi chote cha miaka 27 mumewe alipokuwa gerezani bila matumaini ya kuachiwa huru kutokana na hukumu ya kifungo cha maisha jela alichopewa mwaka 1964, Bi Winnie alilazimika kubeba jukumu la ulezi wa watoto na pia kuendeleza kampeni za kisiasa kutaka mashujaa wa kupigania nchi yao waachiwe huru hasa mumewe.
“Kamwe hatutapoteza matumaini na watu wangu hawatapoteza matumaini kamwe, bila shaka tunatarajia kwamba kazi itaendelea,” alisema wakati huo.
Kutokana na hayo Bi Winnie Mandela alilazimishwa kusalia tu huko Brandford katika jimbo lao la Orange Free katika miaka ya 70 baada ya operesheni mojawapo za kupambana na ubaguzi wa rangi zilizokuja kujulikana zaidi kama the Soweto Uprising.
Bi Mandela (pichani mwaka 1988) alihusika makubwa kukabiliana na utawala wa ubaguzi wa rangiHaki miliki ya pichaREUTERS
Image caption
Bi Mandela (pichani mwaka 1988) alihusika makubwa kukabiliana na utawala wa ubaguzi wa rangi
Kama ilivyomtokea mumewe, Bi Winnie alifungwa gerezani, na hata kuwekwa katika kizuizi cha pekee yake ambacho ni mojawapo ya vifungo vigumu zaidi gerezani vinavyowaathiri wafungwa kisaikolojia.
Lakini baada ya kuachiwa kwake mtindo wa mapambano yake dhidi ya ubaguzi wa rangi ulianza kupata sifa mbaya hasa pale alipoonekana kuendekeza tabia ya kuwavisha tairi shingoni wale waliolengwa kwa tuhuma za usaliti na kisha kuwachoma moto.
“Kwa ‘mikufu yetu’ tutaikomboa nchi hii,” alizoea kusema.
Mambo yalizidi kumwendea mrama kutokana na matendo ya baadhi ya walinzi wake katika kile kikundi kilijulikana kama the Mandela United Football Club.
Walipatikana kuhusika katika kitendo cha kumteka nyara na kumuua kijana mmoja mwenye umri wa miaka 14 aitwae Stompie Moeketsi -kwa tuhuma za kwamba alikuwa akitoa siri kwa maadui zao.
Japo Bi Winnie Mandela aliepuka hukumu ya kifungo jela – baadaye tume ya ukweli na maridhiano iliyoongozwa na askofu Desmond Tutu, iliyokuwa inachunguza ukweli kuhusu matendo tata katika vita dhidi ya ubaguzi wa rangi na kutafuta maridhiano, ilimpata Bi Mandela na hatia ya kutowajibika kisiasa wala kimaadili wakati wa kitendo hicho.
ANC leader Nelson Mandela and wife Winnie raise fists upon his release from Victor Verster prison, 11 February 1990 in PaarlHaki miliki ya pichaAFP
Image caption
Nelson na Winnie Mandela baada yake kuachiliwa huru Februari 1990
Licha ya misukosuko hiyo Bi Mandela alibaki kuwa mtu muhimu sana katika siasa za Afrika kusini na kuwa mwakilishi muhimu waa wanawake waliopambana kufa na kupona dhidi ya utawala wa ubaguzi wa rangi uliokuwa unaendelezwa na Wazungu walio wachache nchini humo.
Katika siku za baada ya uhuru wa Afrika Kusini anakumbukwa zaidi kwa kuwa miongoni mwa wachache katika uongozi wa ANC waliomuunga mkono aliyekuwa rais wa Afrika Kusini Thabo mbeki katika kushtumu na kulaani vikali vitendo vya kuwashambulia wahamiaji wa Kiafrika huko nchini Afrika Kusini.
KUSINI – mashambulio yaliyobadikwa jina xenophobic attack. Pia amekuwa muungaji mkono mkubwa wa kiongozi wa chama cha Economic Freedom Fighters CHA Julius Malema , kilichojimegua kutoka ANC ambacho kilimkosoa vikali rais aliyelazimika kung’atuka Jacob Zuma.
Historia ya Bi Winnie Madikizela Mandela, hadi kifo chake inabaki akikumbukwa zaidi kama mama wa taifa la Afrika kusini aliyesimama kidete dhidi ya ubaguzi wa rangi katika umri wake wote.

Comments are closed.