Ajali ya Treni yaua 20 Misri

Ajali ya Treni yaua 20 Misri

Like
886
0
Thursday, 28 February 2019
Global News

Watu 20 wamekufa na wengine 40 kujeruhiwa baada ya kutokea ajali ya treni katika njia kuu ya treni nchini humo.

Tukio hilo limetokea baada ya treni hiyo kugonga kizuizi cha kupunguza kasi, katika kituo kimoja cha treni katikati ya mji.

Ajali hiyo imesababishwa na kulipuka kwa tanki la mafuta la treni hiyo, hali iliyosababisha majengo ya jirani pia kuungua.

chanzo cha ajali hiyo bado hakijajulikana, lakini saa chache baadaye, Waziri anayeshughulika na usafiri Hisham Arafat alijiuzulu.

Watu walioshuhudia ajali hiyo wamesema wameona miili kadhaa katika janga baya kukumba nchi hiyo katika siku za hivi karibuni, hususan kwa usafiri wa treni.

Mmoja wa mashuhuda, Ahmed Mahmoud ameliambia shirika la Habari la AFP, kuwa alitoa miili ya watu 20 na kuiweka kwenye gari la wagonjwa, yote ikiwa imechomeka.

Aidha amesema kawaida treni likikaribia kituoni huja kwa mwendo wa taratibu, lakini siku hiyo lilikuwa katika kasi.

Awali vyombo vya habari vya nchi hiyo viliripoti kwamba watu waliofariki ni 25 huku wengine 50 wakiwa wamejeruhiwa.

Waziri mkuu wa nchi hiyo Mostafa Madbouli ameapa kutoa adhabu kali kwa yeyote yule atakayehusika kupanga ajali hiyo.

Kwa upande wake, Rais wa nchi hiyo Abdul Fattah al Sisi ametuma salamu za rambirambi kwa familia za marehemu na kusisitiza kuwa watu wote waliojeruhiwa watapata msaada wowote watakaohitaji.

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *