Wakili wa zamani wa Trump aliambia bunge kuwa rais huyo wa Marekani alipanga uongo

Wakili wa zamani wa Trump aliambia bunge kuwa rais huyo wa Marekani alipanga uongo

Like
606
0
Thursday, 28 February 2019
Global News

Wakili wa zamani wa rais wa Marekani Donald Trump, Michael Cohen amedai kwamba kiongozi huyo alimtaka adanganye kuhusu mpango biashara kuhusu biashara ya ujenzi wa jengo mjini Moscow wakati wa kampeni ya uchaguzi wake.

Katika ushahidi alioutoa bungeni, Cohen amesema Trump aliratibu mipango ya siri kwa ujenzi wa jengo kubwa, hata wakati alikana kuhusika na biashara yoyote Urusi.

Ameeleza pia kwamba Trump alifahamu kuhusu kufichuliwa kwa barua pepe zilizodukuliwa za chama cha Democrat na amemuita kiongozi huyo “mbaguzi”, “tapeli” na “muongo”.

Trump alijibu: “Anadanganya ili kupunguza kifungo chake gerezani.”

Rais wa Marekani alichukua muda katika kujitayarisha kukutana na kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong-un huko Hanoi, Vietnam, siku ya Jumatano kumjibu kupitia ujumbe wa Twitter wakili wake huyo wa zamani.

Cohen amesema nini kuhusu mradi wa Moscow?

Katika ushahidi wake wa wazi katika kamati ya bunge la wawakilishi Jumatano, amesema Trump “alifahamu na aliratibu” mipango ya ujenzi wa jengo ‘Trump Tower’ mjini Moscow, huku akikiri wazi kwamba hana biashara yoyote na Urusi.

“Wakati huo huo nilikuwa nashauriana na kujadiliana na Urusi kwa niaba yake,” Cohen ameeleza katika ushahidi wake, “angeniangalia machoni na aniambie hakuna bishara yoyote Urusi na alafu atoke aende kuwadanganya raia wa Marekani kwa kusema hilo hilo. Kwanamna yake, alikuwa akiniambia nidanganye..”

“Alitaka nidanganye,” aliongeza.

Hatahivyo, Cohen ameshtakiwa kwa kulidnagnya bunge alipotoa ushahidi mnamo 2017 kwambajitihada za kujenga jengo refu la Trump huko Moscow zilisitishwa kufikia Januari 2016.

tangu hapo amekiri kwamba kumekuwepo majadiliano yalioendelea hadi Juni 2016 wakati wa kampeni ya uchaguzi, licha ya kwamba ujenzi wa mradi huo haukuendelea.

Cohen ameomba msamaha kwa kauli yake ya awali bungeni, ambayo anatuhumu kwamba ‘ilikaguliwa na kuhaririwa’ na mawakili wa Trump.

Cohen amewaambia wabunge kwamba Trump ni mbaguzi wa rangi.

Amesema: “Aliwahi kuniuliza nitaje jina la nchi moja ambayo inaongozwa na mtu mweusi ambayo sio ‘shithole’ kwa maana ya shimo la choo.

“Huu ulikuwa wakati ambapo Barack Obama ndiye alikuwa rais wa Marekani.

“Tulipokuwa tumo ndani ya gari tukipita mtaa duni huko Chicago, alitamka kwamba ni watu weusi tu wanaoweza kusihi katika hali kama hiyo.

“Na aliniambia kwamba watu weusi hawawezi kumpigia kura kwasababu ni wapumbavu. Lakini bado niliendelea kufanya kazi naye.”

Mchambuzi wa masuala ya kisiasa nchni Tanzania, said Msonga ambaye ameifuatilia sakata hii, ametathmini kwamba katika maelezo ambayo bwana Cohen ameyatoa bungeni, ‘unaona moja kwa moja amejaribu kushambulia baadhi ya hoja za rais Donald Trump ambazo amekuwa akizisimamia kwa muda mrefu.

‘Kwa mfano amekuwa akishughulika na masuala ya vyombo vya habari, familia pamoja na masuala ya ule ukuta wa Mexico na urafiki wake na viongozi ambao wao walikuwa wanafikiria ni maadui wa Marekani’.

Kwa jumla, Msonga anasema ni mambo ambayo yanaweza yakaibua hoja na hisia ambazo zinaweza zikampatia bwana Trump kipindi kigumu wakati wa uchaguzi wa mwaka 2020 pale atakapowania nafasi ya kuiongoza tena Marekani.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *