Global News

GUATEMALA: 130 WAPOTEZA MAISHA BAADA YA KIJIJI KUFUNIKWA NA MATOPE
Global News

ZAIDI ya watu 130 wamefariki dunia baada ya maporomoko ya matope kukiangamiza kijiji kimoja, kando ya mji mkuu wa Guatemala.   Taarifa iliyotolewa leo na mamlaka za nchi hiyo ya Amerika ya Kati, ikiwa ni siku ya tatu tangu janga hilo kutokea, zinasema idadi mpya ya waliopatikana wamekufa imefikia 131, huku wengine 300 wakiwa hawajuilikani walipo.   Maporomoko yenye matope mazito yalikifunika kijiji cha El Cambray katika manispaa ya Santa Cantarina Pinula, na kuharibu nyumba 125, usiku wa...

Like
163
0
Monday, 05 October 2015
MAREKANI: DONALD TRUMP ATANGAZA KUFUKUZA WASYRIA IWAPO ATAPATA RIDHAA YA KUWA RAIS
Global News

DONALD TRUMP amesema atawafukuza wakimbizi kutoka Syria walioko nchini Marekani iwapo atakuwa rais. Bilionea huyo, ambaye kwa sasa anaongoza kwenye kinyang’anyiro cha kusaka tiketi ya kuwania urais kupitia chama cha Republican amesema katika mkutano wa kisiasa kuwa akishinda watarudi kwao. Matamshi hayo ni tofauti na aliyoyatoa mapema mwezi huu akihojiwa na Fox News aliposema Marekani inafaa kuwapokea wakimbizi...

Like
206
0
Thursday, 01 October 2015
TALIBAN YATIMULIWA KUNDUZ
Global News

MAAFISA wa Afghanistan wanasema kuwa wamedhibiti maeneo muhimu ya mji wa kaskazini wa Kunduz kutoka kwa wapiganaji wa Taliban. Oparesheni iliotekelezwa usiku kucha imesababisha kuchukuliwa kwa maeneo muhimu ya serikali mbali na kusababisha uharibifu mkubwa kwa wapiganaji. Lakini wapiganaji wa Taliban wanasisitiza kuwa wanashikilia maeneo makubwa ya mji...

Like
193
0
Thursday, 01 October 2015
MARIKANA: AFRIKA YA KUSINI KULIPA FIDIA
Global News

SERIKALI ya Afrika Kusini imesema italipa fidia kwa familia za wafanyakazi wa mgodini waliouawa wakati wa kuzuka kwa mgogoro wa Marikana mwaka 2012. Rais wa nchi hiyo Jacob Zuma ameeleza kuwa taarifa za kina kuhusu malipo zitatolewa na jopo huru linaloongozwa na jaji. Kwa upande wa familia, wakili wao ameripotiwa kuunga mkono tangazo hilo la...

Like
255
0
Thursday, 01 October 2015
BENDERA YA PALESTINA YAANZA KUPEPEA UN
Global News

BENDERA ya Palestina imepeperushwa kwa mara ya kwanza katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York. Bendera hiyo ilipandishwa kwenye mlingoti kwenye sherehe iliyohudhuriwa na Rais wa Palestina Mahmoud Abbas. Akihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Bw Abbas amesema ni jambo lisiloeleweka kwamba hadi sasa suala la Palestina kuwa taifa bado...

Like
288
0
Thursday, 01 October 2015
MSHUKIWA WA IS AFIKISHWA MAHAKAMANI MALI
Global News

MSHUKIWA wa kundi la wapiganaji wa kiislamu, anayetuhumiwa kuharibu makavazi ya kihistoria nchini Mali, anatarajiwa kufikishwa mbele ya mahakama ya kimataifa ya ICC wakati wowote kuanzia sasa. Anatuhumiwa kuteleza uhalifu wa kivita. Ahmad Al Faqi Al Mahdi, alikabidhiwa kwa mamlaka kuu nchini Niger siku ya Jumamosi ambapo inasemekana aliamrisha au kutekeleza uharibifu katika makavazi ya kale huko...

Like
187
0
Wednesday, 30 September 2015
MAJESHI YA NATO YAWASILI KUNDUZ
Global News

KIKOSI maalum cha shirika la kujihami la muungano wa mataifa ya Magharibi NATO, kinasemekana kufika mji wa Kunduz nchini Afghanistan. Nia hasa ni kujaribu kuutwaa tena mji huo, ambao kwa sasa uko chini ya udhibiti wa kundi la wapiganaji wa...

Like
356
0
Wednesday, 30 September 2015
MAHAKAMA YA UHALIFU KUANZISHWA SUDANI KUSINI
Global News

UMOJA wa Afrika umesema mahakama maalumu itaundwa kwa ajili ya kuwashitaki washukiwa wa makosa ya uhalifu wa kivita nchini Sudani kusini ambapo imekumbwa na mzozo mkubwa tangu mwaka 2013. Hatua hii inalenga kuunga mkono hatua ya Afrika kushughulikia migogoro yao wenyewe. Uundwaji wa mahakama ni sehemu ya makubaliano ya Rais Salva Kiir na Kiongozi wa waasi, Riek Machar yaliyotiwa saini baada ya kuwepo shinikizo kutoka kwa viongozi wa...

Like
230
0
Wednesday, 30 September 2015
WAUZAJI WA MBOGAMBOGA WATOA WITO KUMALIZIKA KWA SOKO JIPYA BABATI
Global News

WAUZAJI wa mboga mboga na matunda waliopo karibu na soko la Mjini Babati Mkoani Manyara, ambao wanauza bidhaa zao chini wametoa ombi kwa halmashauri ya mji huo kumalizia ujenzi wa soko jipya ili waweze kuhamishia bidhaa zao hapo. Wakizungumza  wakati mwenge wa uhuru ukiweka jiwe la msingi kwenye soko jipya, wafanyabiashara hao wamedai wanakuwa na wakati mgumu kwani soko la sasa ni dogo na halitoshelezi mahitaji. Hata hivyo, mkuu wa wilaya ya Babati Crispin Meela, amemweleza kiongozi wa mbio za...

Like
287
0
Wednesday, 30 September 2015
YEMEN: SHAMBULIO LA NDEGE LAUA 131
Global News

IDADI  ya  watu  waliouwawa  katika  shambulio  la  anga kwenye  sherehe  ya  harusi  nchini  Yemen  imefikia  watu 131, na kuaminika kuwa  shambulio  hilo ni baya kuwahi kutokea  katika  vita  nchini Yemen. Muungano unaoongozwa na Saudi Arabia ambao unafanya  mashambulizi  ya  anga  dhidi  ya  maeneo  ya waasi  nchini  Yemen  umekanusha kuhusika  na shambulio  hilo  huku msemaji wa  muungano huo amesema wanamgambo wa  eneo hilo huenda wameshambulia  kwa  makombora. makombora  hayo yaliyorushwa jana...

Like
175
0
Tuesday, 29 September 2015
URUSI KUUNGANA NA MAREKANI KWENYE MAPAMBANO DHIDI YA IS
Global News

NCHI ya Urusi imesema kuwa inatafakari uwezekano wake wa kuifuata Marekani ili kuwashambulia kwa ndege wapiganaji wa kundi la Islamic State (IS). Rais wa nchi hiyo Vladimir Putin ameyasema hayo baada ya kukutana na Rais wa Marekani Barack Obama kwenye maongezi ya nje ya mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa (UN). Hata hivyo hotuba zilizotolewa na viongozi hao katika mkutano huo, ziliashiria mgawanyiko kuhusu jinsi ya kumaliza vita nchini Syria ambapo Urusi ilisema itakua “kosa kubwa” kutofanya kazi...

Like
189
0
Tuesday, 29 September 2015