Dk. Mukwege na Murad washinda Tuzo ya Nobel ya Amani

Dk. Mukwege na Murad washinda Tuzo ya Nobel ya Amani

Like
465
0
Saturday, 06 October 2018
Global News

Daktari raia wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Dennis Mukwege na mwanaharakati kutoka jamii ya Wayazidi, Nadia Murad, wameshinda Tuzo ya Nobel ya Amani, 2018 kwa jitihada zao za kupambana na unyanyasaji wa kingono.

Tangazo la ushindi wa Dk. Mukwege na Murad wa Tuzo ya Nobel limetolewa na mwenyekiti wa kamati ya tuzo hiyo Berit Reiss-Andersen mjini Oslo muda mchache uliopita. Bi Reiss Andersen amesema wote wawili wamekuwa nembo ya mapambano dhidi ya janga la unyanyasaji wa kingono, ambalo limeenea kutoka mzozo mmoja hadi mwingine, kama vuguvugu la MeeToo lilivyodhihirisha.

”Washindi hawa wawili wametoa mchango mkubwa katika kuumulika na kuupinga uhalifu huo wa kivita. Dennis Mukwege ni mtu aliyejitolea maisha yake kuwasaidia wahanga hao. Nadia Murad ni shahidi anayesimulia unyanyasaji, uliofanywa dhidi yake na dhidi ya wengine.” Amesema Reiss-Andersen.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *