Donald Trump na familia yake wachunguzwa kwa kudaiwa kukwepa kodi

Donald Trump na familia yake wachunguzwa kwa kudaiwa kukwepa kodi

Like
705
0
Wednesday, 03 October 2018
Global News

Maafisa nchini Marekani katika jimbo la New York wamesema wamelazimika kuchunguza madai kwamba Rais Donald Trump alisaidia familia yake kukwepa kodi ya mamilioni ya dola katika miaka ya 1990.

Ripoti iliyochapishwa na gazeti la New York Times imemshutumu Rais Trump kwa kuhusika na mpango wa ulipaji kodi ubabaishaji pamoja na udanganyifu ili kuficha makadirio yanayomhusu yeye pamoja na ndugu na wazazi wake.

Ikulu ya White House imetupilia mbali madai hayo kuwa ni ya upotoshaji.

Msemaji wa White House Sara Sanders ameongeza kusema malipo yote yote yalikuwa yakikaguliwa na kupitishwa na mamlaka za kodi kwa miaka mingi iliyopita.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *