HABARI PICHA: Mke wa Kibonde azikwa Makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam

HABARI PICHA: Mke wa Kibonde azikwa Makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam

Like
4904
0
Saturday, 14 July 2018
Local News

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Sofia Mjema (katikati), akiwafariji wafiwa wakati wa mazishi ya Mke wa Ephraim Kibonde, Sara aliyezikwa katika makaburi ya Kinondoni jijini Dar Es Salaam jana July 13/2018.

Marafiki na watu waliokuwa karibu na Marehemu Sarah Kibonde ambao walisoma pamoja katika shule ya Msingi Muhimbili.

Mkurugenzi Mkuu E-fm & @tvetanzania Francis Cizza na Meneja Mkuu, Dennis Ssebo ni miongoni mwa watu walioshiriki kwenye mazishi ya Bi. Sarah Kibonde aliyezikwa Jana July 13/2018 Katika makaburi ya Kinondoni jijini Daresalaam.

Sehemu ya watu wa karibu na familia ya Ephraim Kibonde wakiwemo wafanyakazi wenzake ambao wameungana kuikakamilisha safari ya mwisho ya Bi. Sarah Kibonde.

Zoezi la Kuweka Maua ya Shahada juu ya Kaburi la Sarah Kibonde

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Mh. @paulmakonda aliyeambatana na Mkurugenzi Mkuu wa E-fm & Tv-E @majizzo pamoja na Maneja Mkuu @sseboefm walijumuika kwenye karanga baada ya kukamilisha shughuli za mazishi.

Mkurugenzi Mkuu  wa E-fm & Tve,  Francis Cizza (wa pili kutoka kulia),  Mbunge wa Chalinze(CCM), Ridhiwani Kikwete( katika ), Meneja Mkuu wa E-fm & Tve, Dennis Ssebo  Pamoja na  Mkuu wa Kitengo cha Security wa  Efm na TVE, Kinanda wa kwanza Kulia wakitoka kwenye eneo la Kaburi alipozikwa Salah Kibonde

 

Jana  July 13, 2018 Familia, ndugu, jamaa na marafiki wa karibu na mtangazaji Ephraim Kibonde wameuaga na kuuzika mwili wa marehemu Sara Kibonde ambaye ni mke wa mtangazaji Kibonde nyumbani kwake, Ubungo Kibangu na kisha baadae kuupumzisha mwili wake katika makaburi ya Kinondoni.

E Digital imekuwekea  baadhi ya matukio kwa picha zilizo ripotiwa na Team yetu E Digital na kuziweka pia kwenye Ukurasa wetu wa Instagram

 

 

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *