JE WAZAZI HUKWAMISHA VIPAJI VYA WATOTO?

JE WAZAZI HUKWAMISHA VIPAJI VYA WATOTO?

1
799
0
Tuesday, 09 October 2018
Global News

Nafasi ya mzazi katika kukwamisha au kuendeleza kipaji cha mtoto

 Kipaji ni uwezo wa kuzaliwa nao wa kufanya jambo fulani kwa ngazi ya juu bila kufundishwa au baada ya kufundishwa kidogo tu. Kipaji kinaweza kuwa cha kimwili au cha kiakili lakini pia kinaweza kuendelezwa au kudumazwa.

Mzazi ni mtu wa kwanza anayeweza kutambua uwezo ama kipaji cha mtoto wake. Hata hivyo ana fursa ya kuendeleza au kutokukiendeleza kipaji cha mtoto.

Baadhi ya wazazi hutambua vipaji vya watoto mapema na kuanza kuviendeleza kwa kuwapatia nyenzo mbali mbali ambazo huwasaidia katika kuboresha uwezo walio nao.

Lakini pia wapo wazazi ambao wanamalengo yao juu ya ni kitu gani wanapenda watoto wao wafanye. Ama yamkini hawana ufahamu wa nini cha kufanya ili kumwendeleza mtoto mwenye kipaji .Hata hivyo vipo baadhi ya vipaji ambavyo wazazi huona ni upotevu tu wa maadili mfano kuimba na kucheza mziki.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *