JUKATA YAWATAKA WANANCHI KUSHIRIKI,KUISOMA NA KUILEWA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA

JUKATA YAWATAKA WANANCHI KUSHIRIKI,KUISOMA NA KUILEWA KATIBA ILIYOPENDEKEZWA

Like
303
0
Monday, 13 October 2014
Local News

Jukwaa la Katiba Tanzania- JUKATA limewasihi wananchi kushiriki katika kuhamasishana na kupata Elimu itakayowawezesha Kuisoma na Kuielewa Katiba inayopendekezwa ili kujiandaa na zoezi la upigaji Kura za Katiba hiyo.

Wito huo umetolewa jijini Dar es salaam na mwenyekiti wa JUKATA- DEUS KIBAMBA

Pia imesema inaunga mkono makubaliano kati ya Vyama vya Siasa na Mheshimiwa Rais juu ya kufanyika kwa kura ya maoni baada ya Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015

Amesema kuwa ili uelimishaji ufanikiwe kwa kiasi kikubwa ni vyema kwa mamlaka husika kuwezesha upatikanaji wa kutosha wa nakala za katiba inayopendekezwa na rasimu ya katiba

 

Comments are closed.