Kabati akabidhi viungo bandia kwa walemavu Iringa

Kabati akabidhi viungo bandia kwa walemavu Iringa

Like
697
0
Monday, 21 January 2019
Local News
Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Iringa, Ritta Kabati kupitia programu ya ‘Peoples Empowerment Foundation’ chini ya Kampuni ya Camal Group amefanikisha kuwakabidhi viungo bandia walemavu 10 wa miguu kutoka wilaya tofauti za mkoa huo ambao walikosa msaada na kulazimika kuishi wakiwa na upungufu wa viungo vya mwili.
 
Hayo yamesemwa na Mratibu wa Ofisi ya Mbunge huyo ambapo amesema kuwa Mh. Ritta Kabati alifanya ziara ya kikazi katika mkoa wa Iringa na kubaini uwepo wa walemavu zaidi ya 110 wa viungo mbalimbali vya mwili.
 
Mratibu huyo wa Mbunge Kabati amesema kuwa zoezi la kuwakabidhi walemavu hao viungo bandia lilifanyika January 20 mwaka huu Jijini Dar es laam na lilidhaminiwa na kampuni ya Camal Group na Mgeni rasmi katika shughuli hiyo alikuwa naibu waziri wa nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Kazi Ajira, Vijana na Watu wenye Ulemavu, Stela Ikupa.
 
“Mbunge alifanya ziara katika mkoa wa Iringa ndipo alipobaini uwepo wa hawa hatu wenye mahitaji maalumu tuliwapata watu zaidi ya 110 kutoka wilaya tofauti za mkoa wa Iringa lakini leo tumekuja na wahitaji 10 wa viungo vya miguu ambao wanakabidhiwa viungo hivi,”amesema Mgongo
 
Kwa upande wao baadhi ya wahitaji waliopata viungo hivyo bandia wamemshukuru Mbunge wa viti maalumu mkoa wa Iringa, Ritta Kabati kwa kufanikisha kuwatafutia viungo hivyo kisha kuwasafirisha kutoka Iringa hadi Dar es laam kuwakabidhi viungo ambavyo vitawasaidia kuishi na kuendesha shughuli zao kwa ufanisi.
Katika hatua nyingine Ofisi ya Mbunge huyo imetoa shukrani kwa Mkurugenzi wa manispaa ya Iringa kwa kutoa ushirikiano wakutosha ikiwemo kuwasafirisha wahitaji hao hadi Dar es laam kufanikisha jambo hilo na kuwaomba wadau wengine mkoani humo kujitokeza kuwasaidia watu wenye mahitaji maalumu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *