Kiongozi wa #BringBackOurGirls kuwania urais Nigeria

Kiongozi wa #BringBackOurGirls kuwania urais Nigeria

Like
498
0
Thursday, 11 October 2018
Global News
Oby Ezekwesili ni mwanamama jasiri na maarufu nchini Nigeria anayetaka hivi sasa kupambana katika ulingo wa siasa za kuwania urais katika taifa ambalo kwa miaka mingi ni wanaume ndio wanaozihodhi siasa za nchi hiyo.

Mwanamke aliyeongoza kampeni ya kimataifa ya kutaka waachiwe huru wasichana washule ya Chibok waliotekwa nyara na kundi la itikadi kali la Boko Haram sasa ameamua kugombea urais nchini Nigeria.Oby Ezekwesili ni mwanamke mashuhuri nchini humo.

Oby Ezekwesili ni mwanamama jasiri na maarufu nchini Nigeria anayetaka hivi sasa kupambana katika ulingo wa siasa za kuwania urais katika taifa ambalo kwa miaka mingi ni wanaume ndio wanaozihodhi siasa za nchi hiyo.

Aliwahi kuwa makamu wa rais wa benki kuu ya dunia na pia ni mwasisi mwenza wa shirika la kimataifa la Transparency ambalo liko mstari wa mbele katika kuipiga vita rushwa duniani,ambayo kwahakika ndio tatizo kubwa katika nchi yakeo hiyo yenye utajiri wa mafuta,Nigeria.

Lakini pengine anafahamika zaidi hasa katika mapambano yake ya kupigania kuachiwa huru wasichana wa shule waliokuwa wametekwa nyara na kundi la wanamgambo wa Boko Haram linalotumia kisingizio cha dini ya kiislamu kuendeleza uovu na ukatili. Kundi hilo liliwateka nyara wasichana zaidi ya 200 wa shule kutoka jamii ya wachibok mwaka 2014.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *