Kombe la FA: Mabingwa watetezi Chelsea kuminyana na Man Utd

Kombe la FA: Mabingwa watetezi Chelsea kuminyana na Man Utd

1
1026
0
Tuesday, 29 January 2019
Sports

Mabingwa watetezi wa kombe la FA, Chelsea, wataminyana na mabingwa mara 12 wa kombe hilo, Manchester United, katika mzunguko wa tano wa michuano hiyo.

Mechi ya miamba hiyo itakuwa ni marudio ya fainali ya mwaka jana mabapo Chelsea waliibuka na ushindi.

Timu ya Ligi Daraja la Pili ya Newport County wanaweza kuminyana na mabingwa wa Ligi ya Premia Manchester City iwapo watawang’oa Middlesbrough katika mechi yao ya marudiano.

Timu ya Ligi Daraka la Kwanza Doncaster Rovers wamenuwia kuwang’oa Crystal Palace iliyopo kwenye Ligi ya Premia baada ya kutoka sare mchezo wao wa kwanza wa mzunguko wa nne.

Michezo ya raundi ya tano ya michuano ya FA itapigwa kati ya tarehe 15 na 18 ya mwezi Februari.

Ratiba kamili ya raundi ya tano ya FA:

Bristol City v Shrewsbury Town/Wolverhampton Wanderers

AFC Wimbledon v Millwall

Doncaster Rovers v Crystal Palace

Middlesbrough/Newport County v Manchester City

Chelsea v Manchester United

Swansea v Barnet or Brentford

Portsmouth/Queens Park Rangers v Watford

Brighton & Hove Albion/West Bromwich Albion v Derby County

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *