Serikali  yaapa kuwanasa wauaji, yadai yamechochewa na ushirikina

Serikali yaapa kuwanasa wauaji, yadai yamechochewa na ushirikina

Like
509
0
Wednesday, 30 January 2019
Local News

Serikali ya  imeahidi kuwachukulia hatua kali wale wote watakaobainika kuhusika katika mauaji ya watoto mkoani Njombe.

Waziri Kangi Lugola amesema tayari serikali imepata majina ya wote waliohusika katika mauaji ya watoto Njombe.

Watoto sita, wakiwemo watatu wa familia moja wenye umri chini ya miaka 10 wamepatikana wakiwa wamefariki katika mazingira ya kutatanisha mkoani humo.

Akizungumza Bungeni leo, Waziri wa Mambo ya Ndani nchi, Kangi Lugola amesema tayari wameshabaini baadhi ya wale waliohusika na mauaji hayo na hatua kali zitachukuliwa.

“Uchunguzi wa awali unaonesha kuwa mauaji hayo yametokana na imani za kishirikina…n tayari tumeshawabaini baadhi ya wale ambao wameshiriki. Nawataka watu waache kuichezea serikali. Tutaanza na mkoa wa Njombe,” ameonya Lugola.

Lugola hata hivyo hakusema ni watu wangapi mpaka sasa wametiwa mbaroni kutokana na mauaji hayo.

Vurugu Njombe

Siku ya Jumanne, polisi mkoani Njombe walilazimika kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya wananchi walioandamana katika baadhi ya mitaa wakimtaka mtu anayedaiwa kuwa ni mtekaji wa watoto mkoani humo.

Umoja wa Mataifa (UN) umetoa tamko kuhusu mauaji hayo ikisema inaungana na serikali ya kulaani ‘unyama’ huo waliofanyiwa watoto.

Tamko lililotolewa na UN leo Jumanne Januari 29, 2019 limekemea mauaji hayo ikieleza kuwa hayakubaliki na kubainisha kuwa watoto wana haki ya msingi ya kulindwa kutokana na vurugu ili waweze kufurahia na kupata mahitaji yao muhimu.

“Umoja wa mataifa unaungana na Serikali  kupinga vitendo hivyo vibaya. Kama UN tupo tayari kusaidia Serikali katika jitihada zao za kukabiliana na tatizo hilo,” inaeleza taarifa hiyo ikimnukuu mratibu mkazi wa UN hapa nchini, Alvaro Rodriguez.

“Zaidi ya hayo tunatoa wito kwa wadau wote kuungana pamoja kuhakikisha kunakuwa na usalama wa watoto kuanzia katika makazi, shule na maeneo mengine miongoni mwa jamii.”

Watoto wanapitia katika aina nyingi za unyanyasaji katika maeneo mengi duniani, “Hili linatakiwa likome,” amesema mwakilishi wa Unicef nchini , Maniza Zaman.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *