Maadhimisho ya miaka 100 tangu kumalizika WW1 yafanyika Ufaransa

Maadhimisho ya miaka 100 tangu kumalizika WW1 yafanyika Ufaransa

Like
876
0
Friday, 09 November 2018
Global News
Rais wa Ufaransa anatarijiwa kuwa mwenyeji wa marais Donald Trump, Vladimir Putin na viongozi wengine wa dunia mjini Paris kwa ajili ya kuadhimisha miaka 100 tangu kumalizika Vita Vikuu vya Kwanza.

Rais Emmanuel Macron amedhoofika kisiasa baada ya kufanya ziara kaskazini mashariki mwa Ufaransa ambako alilazimika mara kwa mara kutega sikio lake ili kusikiliza malalamiko ya watu juu ya sera zake ambazo haziungwi mkono na wananachi wa kawaida aliotarajia kuhusiana nao vizuri.

Ziara ya siku sita alizofanya kwenye majimbo, miji na vijiji vilivyoathirika vibaya na Vita Vikuu vya Kwanza nchini Ufaransa iliamuliwa na rais huyo mwenyewe na kuzingatiwa na ofisi yake kuwa ziara isiyokuwa na kifani kutokana na muda wake na maudhui tangu enzi ya urais wa Jenerali Charles de Gaulle.

Kwa kuzitembelea sehemu ambako mapigano yalitanda na kwa kuzitembelea kumbukumbu za vita zinazoababisha majonzi makubwa, rais Macron alifikia lengo lake mojawapo ni kuonyesha jinsi askari walivyojitoa mhanga na wakati huo huo kusisitiza tahadhari juu ya mgawiko wa a barani Ulaya na kuzuka kwa siasa za kizalendo za mrengo mkali wa kulia ambazo ni hatari zinazomtia wasi wasi.

Marcon alilazimika kuzitetea sera za serikali yake juu ya nishati. Bei za juu za petroli zimegonga vichwa vya habari. Serikali yake imeongeza bei ya mafuta ili kugharimia juhudi za kupambana na uchafuzi wa mazingira lakini hatua hiyo imewakasirisha madereva na wamiliki wa malori wanaokusudia kuipinga kwa kuzuia barabara nchini Ufaransa kote wiki ijayo.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *