MSUMBIJI YAFANYA UCHAGUZI MKUU WA RAIS NA WABUNGE

MSUMBIJI YAFANYA UCHAGUZI MKUU WA RAIS NA WABUNGE

Like
329
0
Wednesday, 15 October 2014
Global News

Wapiga kura wanaelekea kwenye vituo vya kupigia kura nchini Musumbiji leo kumchagua rais mpya na wabunge kwenye uchaguzi wenye upinzani mkali tangu taifa hilo lipate uhuru mwaka 1975.

Takriban watu 11 wamejiandikisha kupiga kura nchini humo wakiwemo wengine 90,00 wanaoishi mataifa ya kigeni.

 

141014160822_mozambique_election_512x288__nocredit

 

Zaidi ya watu milioni 10 wamejiandikisha kupiga kura katika uchaguzi wa leo, ambao unaonekana kuwa wa kwanza kidemokrasia tangu nchi hiyo ilipojipatia uhuru wake kutoka kwa Wareno mwaka 1975.

Chama tawala, cha Frelimo, ambacho kimekuwa mamlakani tangu mwaka 1975, kinakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa chama cha upinzani cha Renamo.

 

141015074418_moza_3

Rais Arrnando Guebuza (kushoto) na muasi wa zamani wa Renamo Afonso Dhlakama walifikia mkataba wa amani Septemba

 

 

 

 

 

 

 

 

Kiongozi wa Renamo,Afonso Dhlakama, alitoka mafichoni mwezi jana na kuingia katika kinyang’anyiro cha uchaguzi mkuu katika dakika za mwisho baada ya kufikia makubaliano ya amani na serikali.

Mgombea wa chama tawala ni Filipe Nyusi, ambaye ni waziri wa zamani wa ulinzi.

Msumbijini moja ya nchi zinazokuwa kwa kasi barani Afrika na mshindi wa uchaguzi atahakikisha rasilimali za nchi ikiwemo gesi zinatumiwa vyema.

 

 

 

 

 

 

Comments are closed.