Padri mwimba Rap asimamishwa kazi

Padri mwimba Rap asimamishwa kazi

Like
502
0
Tuesday, 26 June 2018
Global News

Padri wa Kanisa Katoliki aliyejizolea umaarufu nchini Kenya kwa
kutoa ibada kwa mtindo wa ku-rap,Paul Ogalo maarufu kwa jina la
‘Sweet Paul’ amesimamishwa kazi.
Padri Ogalo (45) amekuwa akitumia staili ya ku-rap kuwashawishi
vijana nchini Kenya kwenda kusali ili wajiweke karibu na Mungu.
Taarifa hiyo ya kusimamishwa kazi kwa Padri huyo imetolewa na
Askofu Mkuu wa jimbo Katoliki la Homa Bay, Philip Anyolo ambaye
amemtaka padri huyo achague kati ya kuwa rapper au kuwa Padri.
Kwa mujibu wa Gazeti la Daily Nation la nchini Kenya limeeleza
kuwa Padri Ogalo amesimamishwa kwa mwaka mmoja kutoongoza
ibada au misa kwa kipindi cha mwaka mmoja ingawaje
ameruhusiwa kushiriki ibada na shughuli nyingine za Kanisa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *