Rais Trump akiri mwanahabari Jamal Kashoggi huenda akawa amefariki

Rais Trump akiri mwanahabari Jamal Kashoggi huenda akawa amefariki

Like
833
0
Friday, 19 October 2018
Global News
Rais wa Marekani Donald Trump amekiri huenda mwaandishi habari wa Saudi Arabia Jamal Kashoggi amefariki na kutishia kuchukuwa hatua kali iwapo itathibitika viongozi wa Saudi Arabia walihusika na kifo chake.

Mwanahabari jamal khasoggi

Onyo la Rais huyo wa Marekani limekuja wakati serikali yake ikizidisha ukali juu ya kupotea kwa Mwaandishi Habari Jamal Khasoggi kulikoibua ghdhabu ya Kimataifa. Trump amesema kwa sasa wanasubiri majibu ya uchunguzi kabla ya kutoa taarifa ya aina yoyote.

Kabla ya Trump kuzungumza siku ya Alhamisi utawala wake ulitangaza kuwa waziri wake wa fedha Steven Mnuchin amejiondoa kwenye mkutano mkubwa wa uwekezaji unaoandaliwa na Saudi Arabia.

Wakati huo huo aafisa wa Marekani wakisema kuwa Waziri wa mambo ya kigeni Mike Pompeo alimuonya mwanamfalme wa Saudi Arabia Mohammed bin Salman kuwa uaminifu wake kama kiongozi wa siku za usoni wa taifa hilo uko mashakani.

Pompeo amesema Saudi Arabia inapaswa ipewe muda wa siku chache zijazo wa kufanya uchunguzi wa wazi na unaoaminika kabla Marekani haijaamua namna na vipi itakavyojibu.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *