RAIS WA GHANA ATOA AMRI YA KUKAMATWA KWA MWENYEKITI WA SHIRIKISHO LA SOKA LA GHANA

RAIS WA GHANA ATOA AMRI YA KUKAMATWA KWA MWENYEKITI WA SHIRIKISHO LA SOKA LA GHANA

Like
392
0
Wednesday, 23 May 2018
Global News

Rais wa Ghana Akufo-Addo amemrisha kukamatwa mwenyekiti wa shirikisho la kandanda la Ghana Kwesi Nyantekyi, ambaye pia ni makamu wa rais wa kwanza wa shirikisho la kandanda barani Afrika CAF.

Hatua hiyo inafuatia makala moja ya uchunguzi ambayo inamhusisha Kwasi Nyantekyi na vitendo vya ulaghai.

Inadaiwa kuwa alitumia jina la rais wakati akipanga na kutekeleza ulaghai huo.

Uchunguzi huu uliofanywa na mwandishi wa habari maarufu Anas Aremeyaw Anas uliwasilishwa kwa rais.

Uchunguzi huu pia unadaiwa kufichua vitendo vya ufisadi miongoni mwa maafisa wengine wa shirikisho la kandanda nchini Ghana.

Video hiyo inapangiwa kuonyeswa kwa umma tarehe sita mwezi ujao.

Kwesi Nyantenkyi amekuwa rais wa shirikisho la kandanda nchini Ghana tangu mwaka 2005 na hajatamka lolote.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *