Local News

Lukuvi aanza na bibi aliyemlilia Maguful
Local News

Kilio cha Nyasasi Masige, mkazi wa Bunda mkoani Mara mbele ya Rais John Mgufuli kuhusu kuwapo kwa njama za kudhulumiwa ardhi yake, kimezaa matunda baada ya waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi kutua wilayani humo na kumaliza mgogoro huo. Waziri Lukuvi anayetembelea Mkoa wa Mara kutatua migogoro ya ardhi na kutekeleza agizo la Rais Magufuli, jana aliwaagiza watendaji wa idara ya ardhi mkoani humo kushirikiana na wenzao wa Halmashauri ya Mji wa Bunda kupima upya eneo...

Like
651
0
Tuesday, 18 September 2018
Tanzia: CCM Yapata Pigo, Guninita Afariki Dunia
Local News

ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana CCM (UVCCM), Taifa na baadaye akawa Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam, John Guninita amefariki dunia leo Alhamisi, Septemba 13, 2018 alfajiri katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa amelazwa akipatiwa matibabu. Taarifa za msiba huo zimethibitishwa na mdogo wake na marehemu, Gerald Guninita ambaye naye aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Kilolo wakati wa Uongozi wa Awamu ya Nne. Kwa mujibu wa Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Huduma kwa...

Like
519
0
Thursday, 13 September 2018
MENEJA SIMBA AFUNGIWA  MWAKA MMOJA NA TFF KUJIHUSISHA NA SOKA, FAINI
Local News

Meneja wa Simba SC, Robert Richard amefungiwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kwa muda wa mwaka mmoja kujihusisha na masuala ya soka huku adhabu hiyo ikiambatana na faini ya shilingi za Kitanzania, milioni 4. Adhabu hiyo imetolewa kutokana na kosa la kuihujumu timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa...

Like
484
0
Monday, 10 September 2018
TUMENUFAIKA NA MKUTANO WA  FOCAC-MAJALIWA
Local News

WAZIRI MKUUKassim Majaliwa amesema Tanzania imepata mafanikio makubwa kutokana na kushiriki kwake katika Mkutano wa Jukwaa la Ushirikiano kati ya China na Afrika (FOCAC).   Amesema kikao hicho kimekuwa na tija kwa Tanzania kutokana na maeneo ya vipaumbele yaliyojadiliwa katika mkutano huo hususani masuala ya uwekezaji kwenye sekta ya viwanda.   Waziri Mkuu aliyasema hayo jana (Jumatano, Septemba 05, 2018) alipokutana na waandishi wa habari katika kikao cha majumuisho ya ziara yake ya kikazi China ambako alikwenda kumuwakilisha Rais...

1
447
0
Thursday, 06 September 2018
Msafara wa Rais Magufuli wapata ajali Mara
Local News

MSAFARA wa Rais John Magufuli uliokuwa ukielekea wilayani Ukerewe mkoani Mwanza, umepata ajali katika kijiji cha Kasuguti, kata ya Kisorya, wilayani Bunda mkoani Mara, leo Septemba 4, 2018 baada ya magari manne kugongana katika eneo ambalo barabara ilikuwa ikijengwa. Taarifa za awali zinadai kuwa waandishi wawili wa habari wamejeruhiwa baada ya gari walimokuwa kupinduka. Amesema chanzo cha ajali hiyo ni vumbi lilikuwa limetapakaa barabarani kutokana na msafara huo hivyo madereva kushindwa kuona vizuri njia lakini hakuna madhara makubwa licha...

Like
599
0
Wednesday, 05 September 2018
Tunatoa Pole kwa Mama Mzazi wa Mbunge ‘Sugu’ Ambaye Amefarik Dunia Jana
Local News

Mama mzazi wa Mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu (CHADEMA), amefariki dunia jana Jumapili Agosti 26, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH), alikokuwa akipatiwa matibabu. Uongozi wa TV E na EFM Redio unatoa pole kwa Mbunge Sugu pamoja na Familia yake, Mungu hawaongoze kwenye kipindi hiki Kigumu....

1
383
0
Monday, 27 August 2018
Lugola amuagiza DCI amkamate aliyekuwa mkurugenzi Nida
Local News

Waziri wa Mambo ya Ndani, Kangi Lugola amemuagiza Mkurugenzi wa Makosa Jinai nchini (DCI) kumkamata aliyekuwa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (Nida), Dickson Maimu kabla ya saa 12 jioni leo na tayari ameshakamata na kupelekwa Dar es Salaam. Lugola pia ameagiza kukamatwa kwa wamiliki wa kampuni tatu zinazodaiwa kuhusika katika mradi wa vitambulisho vya taifa, Gotham’s International Limited, Gwiholoto Impex Ltd na Aste Insurance wanaodaiwa kufanya udanganyifu na kushindwa kurejesha fedha walizotumia kinyume na utaratibu....

Like
545
0
Tuesday, 21 August 2018
Rais wa Uganda Museveni anakanusha kwamba Bobi Wine amejeruhiwa
Local News

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amekanusha kwamba mbunge wa upinzani Bobi Wine amejeruhiwa. Katika taarifa yake ya kwanza kuhusu afya ya mbunge huyo aliyekamatwa na vikosi vya usalama nchini, Museveni amevishutumu vyombo vya habari kwa kile alichokitaja ni kueneza habari zisizo za kweli kuhusu suala hilo. Kulingana na ripoti mbalimbali za vyombo vya habari mbunge huyo ambaye pia ni msanii, Robert Kyagulanyi ana matatizo ya figo ambayo yanahitaji kutibiwa ipasavyo na madaktari bingwa waliobobea katika kutiba sehemu nyeti kama hizo...

Like
480
0
Monday, 20 August 2018
Hali ya Kingwalla Yazidi Kuimarika
Local News

HALI ya Waziri wa Maliasili na Utali, Dkt. Hamisi Andrea Kigwangalla imeendelea kuimarika vizuri kutokana na matibabu anayopatiwa katika Hospitali ya Taifa, Muhimbili alikolazwa baada ya kupata ajali ya gari akiwa mkoani Arusha kuelekea Dodoma kikazi. Picha zinaonesha Kigwangalla akiwa amepata nafuu na kutoka nje ya Jengo la Hospitali hiyo jambo linaloonyesha faraja huenda akapona hivi karibuni. Mbunge huyo wa Nzega (CCM) alipata ajali wiki chache zilizopita baada ya gari lake kupinduka na kusababisha kifo cha Afisa habari wake, Hamza Temba...

Like
649
0
Tuesday, 14 August 2018
Biteko atoa wiki moja kwa muwekezaji kulipa kodi ya madini serikalini
Local News

Naibu waziri wa madini, Dotto Biteko akizungumza na wachimbaji wadogo wa eneo la Kilalani, baada ya kutembelea eneo hilo.     Serikali imempa muda wa wiki moja nwekezaji mmiliki wa kampuni ya Amazon Trading (T)Company Limited Abdi Hozza kuhakikisha anailipa serikali kodi ya pango ya uwekezaji kiasi cha dola za Marekani 70,020 sawa na zaidi ya shilingi milioni 140 za kitanzania anazodaiwa tangu mwaka 2011 katika machimbo ya Kalalani eneo la Umba wilayani Korogwe kutokana na leseni nane za uchimbaji...

Like
611
0
Tuesday, 14 August 2018
RC MAKONDA AVIWEZESHA KIUCHUMI VIKUNDI VYA JOGGING KWA KUVIPATIA MITAJI
Local News

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda leo ameanza rasmi mpango wa kuviwezesha kiuchumi vilabu vya Jogging kwa kuvipatia mitaji ya kuwezesha kuanzisha miradi ya kujikwamua kiuchumi. Akizungumza wakati wa Bonanza la Vilabu vya Jogging Dar es salaam RC Makonda ameanza kwa kukabidhi kitita cha zawadi ya shilingi milioni 10 kwa washindi wa makundi mbalimbali pamoja na kuahidi kukabidhi shilingi Million Saba kwa chama cha Jogging Temeke ili waweze kuwa na SACOS yao endapo atajiridhisha kuwa wamekidhi...

Like
502
0
Sunday, 12 August 2018