Global News

Rais wa Ukraine aiomba Nato kutuma meli
Global News

Rais wa Ukraine Petro Poroshenko ameiomba Nato kutuma meli kwenda bahari ya Azov kufuatia makabiliano yaliyotokea kati ya Ukraine na Urusi baharini eneo la Crimea. Poroshenko aliliambia gazeti la Ujerumani Bild kuwa anaamini kuwa meli hizo zitapelekwa “kuisaidia Ukraine na kuweka ulinzi”. Siku ya Jumapili Urusi ilivamia meli tatu za Ukraine na kuwashika mabaharia wake kutoka Kerch strait. Nato imesema inaunga mkono Ukraine ambayo si mwanachama wake. Siku wa Jumatano Rais wa Urusi Vladimir Putin alimlaumu Bw Poroshenko kwa kuanzisha...

Like
653
0
Thursday, 29 November 2018
Wachina 3 kufikishwa mahakamani Nairobi kufuatia sakata ya tikiti treni SGR
Global News

Raia watatu wa China wanaofanya kazi na reli mpya nchini Kenya SRG watafikishwa mahakamani baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika kwenye sakati ya tikiti. Hii ni baada ya mwendesha mashtaka mkuu nchini Kenya kuidhinisha tume ya kupambana na ufisadi kuwafungulia mashtaka raia hao watatu wa China. Li Gen, anayesimamia usafiri , Li Xiaou meneja wa ulinzi na Sun Xin ambaye ni mfanyakazi watafunguliwa mashtaka ya kujaribu kuwahonga maafisa waliokuwa wanachunguza sakata hiyo ya tikiti. Watatu hao wanaripotiwa kujaribu kuwahonga...

Like
569
0
Monday, 26 November 2018
auua mpenzi wake na kumpika’
Global News

Mwanamke mmoja raia wa Morocco anatuhumiwa kumuua mpenzi wake na kumfanya kitoweo huko Falme za Kiarabu, waendesha mashtaka wanasema. Tukio hilo linadaiwa kufanyika miezi mitatu iliyopita, laikini limegundulika hivi karibun baada ya jino la binaadamu kuonekana kwenye mashine ya kusagia matunda ya mwanamke huyo. Mtuhumiwa huyo amekiri kutenda makosa hayo, na kuseam ulikuwa wakati wa “uwendawazimu”, gazeti la serikali la The National linaripoti. Mwanamke huyo ambaye yupo kwenye miaka ya 30 atapandishwa kizimbani baada ya kukamilika...

Like
530
0
Thursday, 22 November 2018
Donald Trump hatousikiliza mkanda wa sauti ya mauwaji ya Khashoggi
Global News

Rais wa Marekani Donald Trump amesema amejuzwa kuhusu mkanda wa sauti wa mauaji ya mwanahabari Jamal Khashoggi lakini amesema binafsi hatousikiliza. “Ni mkanda wa maumivu, ni mkanda mbaya,” Trump ameiambia runinga ya Fox News. Shirika la ujasusi la Marekani CIA linaaminika kufikia kikomo kuwa mwanamfalme Mohammed bin Salman aliamrisha kutekelezwa kwa maujai hayo, japo bado Ikulu ya White House haijathibitisha uchunguzi huo. Saudi Arabia imeziita taarifa hizo kuwa ni za uongo na kudai kuwa bin Salman hakuwa na taarifa yoyote...

Like
412
0
Monday, 19 November 2018
Marekani kutoa ripoti ya mwisho juu ya mauaji ya Khashoggi
Global News

Rais Donald Trump amesema jana kwamba Marekani itatoa ripoti yake ya mwisho wiki ijayo juu ya mauaji ya Jamal Khashoggi, kufuatia ripoti ya shirika la ujasusi la nchi hiyo, CIA, iliyosema kwamba Mwanamfalme Mohammed Bin Salman wa Saudi Arabia ndiye aliyeamrisha kuuawa kwa mwandishi habari huyo. Saudi Arabia mara kwa mara imekuwa ikibadilisha kauli yake rasmi juu ya mauaji hayo ya Oktoba 2. Kwanza ilikana kujua chochote kile juu ya mahala alipo Khashoggi na baadaye kusema kwamba aliuawa ndani ya...

Like
506
0
Sunday, 18 November 2018
Watu 76 wafa, zaidi ya 1,000 hawajulikani walipo moto wa California
Global News

Idadi ya watu wasiojulikana walipo hadi sasa kutokana na moto mbaya kabisa jimbo la California, Marekani, imepindukia 1,200, huku mabaki ya miili 76 ikiwa imepatikana na msako ukiendelea. Tathmini iliyotolewa na mkuu wa Kaunti ya Butte ulitokea moto huo, Kory Honea, alisema siku ya Jumamosi (Novemba 17) kwamba ongezeko la idadi ya watu wasiojulikana walipo linatokana na juhudi za ofisi yake kuchunguza idadi ya simu za dharura zilizopigwa wakati wa masaa ya awali ya moto huo kuanza mnamo tarehe 8...

Like
958
0
Sunday, 18 November 2018
Viongozi wa Afrika wakutana kujadili mageuzi katika Umoja wa Afrika
Global News

Viongozi wa nchi na mawaziri kutoka nchi 55 wa Umoja wa Afrika wanakutana katika kile kinachoonekana juhudi za dakika ya mwisho za kufikia makubaliano kuhusu haja ya kuufanyia Umoja wa Afrika mageuzi. ais wa Rwanda Paul Kagame amewahimiza viongozi wenzake wa nchi za Afrika kufikia makubaliano kuhusu maguezi yaliyojadiliwa kwa muda mrefu kuhusu Umoja wa Afrika. Kagame ameyasema hayo katika mkutano maalumu wa kilele wa Umoja huo unaofanyika Addis Ababa, Ethiopia. Je, mageuzi yatafikiwa? Viongozi wa nchi na mawaziri kutoka...

Like
727
0
Saturday, 17 November 2018
CIA ‘yamlaumu mwanamfalme wa Saudia ‘
Global News

Shirika la ujasusi la Marekani(CIA) linaamini kuwa Mwanamfalme Mohammed bin Salman wa Saudi Arabia ndiye aliyeamuru kuuawa kwa mwandishi wa habari Jamal Khashoggi. Vyanzo kutoka shirika hilo vinasema kuwa vina ushahidi wa kutosha kuthibitisha kuwa huenda mrithi huyo wa ufalme wa Saudi Arabia alijuwa kuhusu mipango ya kumuua Khashoggi.   Kauli hiyo ya CIA, iliyoripotiwa kwanza na gazeti la Washington ni ya hali ya juu kabisa kutolewa na Marekani mpaka sasa, ikimuhusisha moja kwa moja mtawala huyo mtarajiwa wa Saudi...

Like
373
0
Saturday, 17 November 2018
Walinda amani wa MONUSCO wauawa DRC
Global News

Umoja wa Mataifa umesema walinda wake amani wapatao 7 wameuawa katika mapigano yaliyozuka karibu na mji wa Beni kaskazini mwa Kivu, mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Ni eneo lililoathiriwa zaidi na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola nchini humo. Bado haijajulikana ni kundi gani la waasi limehusika na mashambulizi. Akizungumza na Waandishi wa Habari juu ya tukio hilo, msemaji wa Umoja wa Mataifa Stephane Dujarric amesema wanajeshi hao waliokufa, 6 ni kutoka Malawi na 1 Tanzania. ”..Walinda amani wameuawa...

1
652
0
Friday, 16 November 2018
Morocco imezindua treni inayokwenda kwa kasi zaidi Afrika
Global News

Morocco imezindua treni inayokwenda kwa kasi zaidi barani Afrika – itakayopunguza nusu ya muda unaotumika kusafiri katika miji ya kibiashara na kiviwanda Casablanca na Tangi Mfalme Mohammed VI na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron waliipanda treni hiyo katika safari ya uzinduzi kutoka Tangier hadi katika mji mkuu Rabat. Takwimu kuu kuhusu treni ya kasi Afrika: Treni imepangiwa kwenda kwa kasi ya 320km kwa saa Itakapunguza kwa zaidi ya nusu muda unaotumika kusafiri 200km kutoka mji wa Casablanca hadi Tangi kuwa...

Like
738
0
Friday, 16 November 2018
Sayari ambayo iko karibu na nyota imegunduliwa na wanasayansi
Global News

Wataalamu wa elimu ya sayansi wamegundua sayari ambayo inazungua karibu kabisa na nyota pamoja na jua. Sayari kama hizi zina uwezekana kuwa na malengo muhimu katika kutafuta ishara ya maisha ya kizazi kijacho kuona mbali. Ukubwa wa sayari hizo zinafikiriwa kuwa mara tatu zaidi ya dunia, huku dunia imewekwa katika kiwango cha ubora zaidi duniani. Guillem Anglada Escudé na wenzake waliandika katika jarida la ‘Nature’ na kusema kwamba wamegundua sayari yenye ukubwa mara tatu zaidi ya dunia. ” Tunafikiri kwamba...

Like
1109
0
Thursday, 15 November 2018