Local News

PICHA: SHIKA NDINGA KIBAHA 2016
Local News

Odinga zikiwa jukwaan zikisubiri kushindaniwa Majaji wakiandaa eneo la kufanya mashindano Swebe Santana akisherehea Choggo Chema Mmoja ya washiriki akipokea maelekezo Mashabiki wakifuatilia mtanange Mashindano yakiendelea David Urasa akikabidhi zawadi kwa baadhi ya washiriki walioingia kwenye fainali kuiwakilisha Kibaha Washindi wa pikipiki wakiwa kwenye pikipiki zao Matery Mushi akikabidhi zawdi kutoka Vodacom Meneja Mkuu E-fm, Denis Ssebo akizungumza na wakazi wa Kibaha Mzee Kungu baya akitoa burudani ya...

Like
590
0
Monday, 09 May 2016
MUFTI MKUU AWATAKA WATANZANIA KUJENGA UMOJA NA USHIRIKIANO
Local News

MUFTI Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuber bin Ally amewataka watanzania kudumisha umoja na mshikamano ili kujenga taifa na kuleta maendeleo. Sheikh Zuber ameyasema hayo wakati akizungumza na baraza kuu la waislamu Tanzania BAKWATA katika semina elekezi kwa viongozi wa baraza hilo Taifa. Naye Sheikh mkuu wa mkoa wa Mtwara Nurdin Abdala Athumani ameongeza kuwa watanzania ili wapate maendeleo ni lazima watumie viwanda ipasavyo kuzalisha na kudumisha suala la umoja pamoja na amani iliyopo kwa manufaa ya...

Like
302
0
Friday, 06 May 2016
WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA NA WATOTO YAKUSUDIA KUTOA TAARIFA YA WANAWAKE WANAOFARIKI KWA MATATIZO YA UZAZI
Local News

WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa inakusudia kutoa taarifa ya wanawake wanaofariki Dunia kutokana na matatizo ya uzazi kila baada ya miezi mitatu ili kukabiliana na tatizo la vifo vya wanawake nchini.   Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu Jijini Dar es Salaam wakati akifungua Mkutano wa Viongozi Wanawake kuhusu masuala ya Afya.   Ameeleza kuwa, katika uteuzi atakaoufanya kwenye bodi zilizo chini ya Wizara...

Like
253
0
Friday, 06 May 2016
ILALA: POLISI YAWATOA HOFU WANANCHI JUU YA HALI YA USALAMA
Local News

JESHI la polisi Mkoa wa kipolisi Ilala limewahakikishia usalama wananchi wa Mkoa wa kipolisi Ilala na kuachana na taarifa za uvumi kuwa hali ya usalama katika mkoa huo wa kipolisi sio nzuri.   Akizungumzia suala hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Lucas Mkondya amesema kuwa Jeshi la Polisi limejipanga ipasavyo kukabiliana na uhalifu wa aina yoyote.   Kuhusiana na malalamiko ya wananchi wa Buguruni kuhusiana na kuwepo kwa kundi la vibaka na waporaji kamanda Mkondya amesema...

Like
225
0
Thursday, 05 May 2016
DARESALAAM INATARAJIWA KUWA NA WATU MILIONI 10 IFIKAPO 2030
Local News

MKOA wa Dar es salaam unatarajiwa kuwa na watu milioni 10 ifikapo mwaka 2030 hivyo ni muhimu kuzingatia uboreshaji wa Jiji kulingana na idadi ya watu.   Hayo yamebainishwa leo na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mheshimiwa Paul Makonda wakati akizungumza na wanahabari ofisini kwake ambapo amesema kuwa kutokana na kuwepo kwa ongezeko la watu serikali ilibuni mradi wa uendelezaji wa Jiji kwa ufadhili wa benki ya dunia.   Amesema kuwa ukuaji wa Jiji la Dar es salaam unakabiliwa na makazi...

Like
241
0
Thursday, 05 May 2016
AJIRA KWA VIJANA BADO NI CHANGAMOTO
Local News

MKURUGENZI wa Idara ya Ajira Ameir Ali Ameir amesema tatizo la ajira nchini bado ni changamoto kubwa kwa vijana kutokana na vijana wengi kukosa sifa za kuajiriwa na baadhi yao kuchagua kazi za kuajiriwa.   Ameir ameyasema hayo katika Ukumbi wa Kidongo chekundu wakati alipokuwa akifungua mafunzo ya Kuwajengea Uwezo wa Kamati za Ajira za Wilaya za Mjini na Magharibi.   Amesema vijana ndio nguvu kazi katika jamii hivyo wana nafasi kubwa katika kulitumika Taifa kwa  kufanya kazi lakini mtazamo wa vijana bado...

Like
355
0
Thursday, 05 May 2016
SERIKALI YATANGAZA KUTOA MAFUNZO KWA WASIMAMIZI NA MADEREVA WA KEMIKALI
Local News

SERIKALI imesema kuwa inatarajia kutoa mafunzo kwa wasimamizi 61 wa shughuli za Kemikali na madereva 123wanaosafirisha Kemikali mbalimbali ili kuzuia athari zinazotokana na matumizi yasiyozingatia sheria na kanuni za kemikali.   Akizungumza jana Jijini Dar es salaam  wakati wa mkutano na waandishi wa Habari, Mkuu wa Kitengo Cha Utafiti na ubora wa Mifumo Benny Mallya kutoka Ofisi ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali amesema mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa sheria ya usimamizi na udhibiti wa kemikali za viwandani...

Like
329
0
Thursday, 05 May 2016
VITA DHIDI YA DAWA ZA KULEVYA NI JUKUMU LA KILA MMOJA WETU
Local News

JAMII imetakiwa kushirikiana na Serikali pamoja na Sekta binafsi zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya kwani vita hiyo ni ya kila Mtanzania mwenye nia njema na vijana. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Kituo cha kusaidia waathirika wa Dawa za kulevya cha Pili Misana Foundation kilichopo Kigamboni jijini Dar es salaam Bi Pili Misana alipozungumza na Waandishi wa habari katika hafla ya kituo hicho kufikisha miaka minne tangu kuanzishwa kwake. Bi. Misana amesema tangu kuanzishwa kwa vituo...

Like
276
0
Wednesday, 04 May 2016
TEKNOLOJIA YAIWEZESHA SEKTA YA FEDHA KUPIGA HATUA
Local News

SERIKALI imesema kuwa maendeleo katika sekta ya fedha kwa kutumia teknolojia yamepiga hatua kubwa kwa  kupitia mkonge wa Taifa imekuwa rahisi kwa Watanzania kutumia na kuchochea kasi ya biashara na kujenga uchumi wa Taifa kwa ujumla. Akizungumza na E fm Jijini Dar es salaam Naibu Waziri fedha na Mipango Dokta Ashatu Kijaji amesema kuwa Watanzania wana nafasi kubwa ya kutumia teknolojia hiyo vizuri na itasaidia kuinua uchumi na kuchochoea maendeleo ya Taifa. Amebainisha kuwa Serikali imejipanga vizuri katika kudhibiti udanganyifu na...

Like
308
0
Wednesday, 04 May 2016
TED CRUZ AJIONDOA KWENYE KINYANG’ANYIRO MAREKANI
Local News

SENETA wa jimbo la Texas Ted Cruz amejiondoa katika kinyang’anyiro cha uteuzi wa kugombea nafasi ya urais wa Marekani kupitia chama cha Republican. Cruz ametoa tangazo lake muda mfupi baada ya kupoteza kura katika kampeni za mwisho Indiana. Katika hatua nyingine Seneta wa Vermont- Bernie Sanders amemshinda Hillary Clinton kwenye uchaguzi wa mchujo wa kuteua mgombea urais wa chama cha Democratic katika jimbo la...

Like
187
0
Wednesday, 04 May 2016
WATU LAKI NNE HUPOTEZA MAISHA KILA MWAKA KUTOKANA NA MABADILIKO YA HALI YA HEWA
Local News

INAKADIRIWA kuwa Watu laki nne hupoteza maisha kila mwaka Nchini kutokana na athari zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa ikiwemo mafuriko, ukame na migogoro ya rasilimali kwa Wakulima na Wafugaji. Hayo yamesemwa Jijini Dar es salaam na Dokta Azma Simba katika Semina maalum ya Wanahabari iliyoandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Mamlaka ya hali ya hewa lengo ikiwa ni kuwajengea uwezo Wanahabari kutoa elimu juu ya athari za mabadiliko ya tabia nnchi. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya...

Like
224
0
Wednesday, 04 May 2016