Local News

BUNGE LAPITISHA MUSWADA KUZUIA VITENDO VYA UHARAMIA DHIDI YA MIUNDOMBINU
Local News

BUNGE LA JAMHURI ya Muungano wa Tanzania limepitisha Muswada wa Azimio la Bunge kuridhia Itifaki ya kuzuia vitendo vya uharamia dhidi ya Miundombinu ya Kudumu iliyojengwa chini ya Bahari ya mwambao wa Bara ya mwaka 1988 iliyowasilishwa November 21 mwaka huu na Waziri wa Uchukuzi Dokta HARRISON MWAKYEMBE. Muswada huo umepitishwa leo Bungeni mjini Dodoma mara baada ya Wabunge kujadili kwa kina na kutoa mapendekezo ya maboresho ambayo yatawezesha kukomesha vitendo vya uharamia katika masuala mbalimbali nchini. Katika hatua nyingine...

Like
225
0
Monday, 24 November 2014
MANISPAA YA MOSHI YAHITAJI MAABARA 13
Local News

VYUMBA 13 vya Maabara ya Masomo ya Sayansi, Vinahitajika katika Shule za Sekondary kwenye Halmashauri ya Manispaa Moshi, mkoani Kilimanjaro. Akizungumza na Waandishi wa Habari Ofisini kwake Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Moshi SHAABAN NTARAMBE ameeleza kuwa vyumba hivyo vya Maabara vitakamilika na kufikisha idadi ya Maabara 42 zinazohitajika katika Manispaa hiyo. Amebainisha kuwa kwa sasa ni Maabara 29 zimekamilika hivyo kufanya upungufu wa maabara...

Like
715
0
Monday, 24 November 2014
WAKAZI WA NGARENARO WAMO HATARINI KUPATA MAGONJWA
Local News

utupaji watoto Wachanga umekithiri katika mto Ngarenaro jijini Arusha hali inayohatarisha magonjwa kwa watumiaji wa Maji yanayotoka katika Mto huo. Kutokana na hali hiyo wakazi waliopo karibu na mto huo wamelazimika kufanya usafi wa mazingira mara kwa mara. Mkazi wa eneo la Kambi ya Fisi ambako pia mto huo unapita MWAJUMA MBAGA amesema wanalazimika kila mtu kuwa mlinzi wa mwenzake katika kuulinda mto huo. Kazi ya kuusafisha mto huo inafanywa na wakazi wa eneo hilo kwa kushirikiana na Jumuiya ya...

Like
248
0
Monday, 24 November 2014
MACHALI AITAKA SERIKALI KUHESHIMU MISINGI YA UTAWALA BORA
Local News

KAMBI RASMI ya Upinzani Bungeni imeishauri serikali kuwashirikisha kikamilifu wananchi masuala mbalimbali muhimu ili wawe na uelewa wa kutosha kuhusu masuala hayo kabla ya kuyaridhia moja kwa moja. Ushauri huo umetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na msemaji wa kambi ya upinzani kupitia wizara ya uchukuzi mheshimiwa MOSES MACHALI wakati akichangia muswada wa azimio la bunge kuridhia itifaki ya kuzuia vitendo vya uharamia dhidi ya miundombinu ya kudumu iliyojengwa chini ya bahari ya mwambao wa bara ya mwaka 1988 iliyowasilishwa na...

Like
287
0
Friday, 21 November 2014
TACAIDS KUADHIMISHA SIKU YA UKIMWI NJOMBE
Local News

  TUME ya kudhibiti Ukimwi-TACAIDS inatarajia kuadhimisha siku ya Ukimwi duniani ambapo mwaka huu maadhimisho hayo Kitaifa yatafanyika Mkoani Njombe. Maadhimisho hayo yatakayoanza Novemba 24 hadi Disemba Mosi mwaka huu, yamebeba kauli mbiu isemayo Tanzania bila maambukizo , ubaguzi na Unyanyapaa inawezekana. Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam, Mkurugenzi wa Sera, Mipango ya utafiti wa Tume hiyo Dokta Raphael Kalinga, amesema asilimia 99 ya watanzania wamesikia kuhusu Ukimwi na kati yao asilimia 60 tu ndiyo wanaelewa....

Like
254
0
Friday, 21 November 2014
WAKAZI WA NAMTUMBO WAMO HATARINI
Local News

ASILIMIA kubwa ya wakazi wa Wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma hawatumii vyoo vya kudumu hali ambayo inahatarisha usalama wa afya zao. Uchunguzi uliofanywa na EFM katika baadhi ya vijijivya Wilaya hiyo umebaini kuwa wananchi wengi wanatumia vyoo vya muda ambavyo siyo salama hasa kipindi cha Mvua kwani vimejengwa kwa nyasi bila kuezekwa. Vijiji ambavyo wananchi wake wanatumia vyoo vya muda ni pamoja na Luegu, Nahoro, Ukiwayuyu, Ngwinde na Namanguli...

Like
337
0
Friday, 21 November 2014
BABA BORA KUHAMASISHA WANAUME KUTIMIZA WAJIBU WAO
Local News

WANAUME wametajwa kuwa   na ushiriki mdogo katika suala zima la malezi ya Watoto hali inayosababisha washindwe kupata malezi yao. Hayo yameelezwa na Mratibu wa SAVE THE CHILDREN Zanzibar RAMADHAN RASHID wakati wa Uzinduzi wa   Kampeni ya BABA BORA ambayo inahamasisha Wanaume kushiriki Malezi ya Watoto na sio jukumu hilo kuachiwa Wanawake Pekee. Kampeni hiyo imezinduliwa na Shirika la Save The Children kwa kushirikiana na Umoja wa Nchi za...

Like
279
0
Friday, 21 November 2014
KONGAMANO LA KIMATAIFA KUFANYIKA LEO
Local News

  KONGAMANO la Kimataifa la Masuala ya Uongozi linafanyika leo jijini Dar es salaam kwa lengo la kujifunza Misingi ya Uongozi bora, Barani Afrika. Akizungumza na waandishi wa habari Mwenyekiti wa Kongamano hilo MBUTHO CHIBWAYE amesema kuwa kongamano hilo litasaidia kuleta mabadiliko na maendeleo chanya katika nchi za Afrika. Mbutho amebainisha kuwa Kongamano litachangia kutatua migogoro inayo sababisha machafuko ya kisiasa na kijamii. Aidha ametoa wito kwa Watanzania wote nchini kujitokeza na kushiriki Kongamano...

Like
212
0
Friday, 21 November 2014
CRC YAADHIMISHA MIAKA 25 LEO
Local News

MFUKO wa Watoto wa Umoja wa mataifa UNICEF imeadhimisha miaka 25 tangu kuanzishwa kwa mkataba wa haki za mtoto CRC na taasisi mbalimbali nchini kwa kutambua haki za Watoto wa Tanzania. Hafla hiyo iliyobeba kauli mbiu ya “Watoto milioni 23: Tuongee kuhusu haki zao” imehusisha majadiliano ya namna ya kulinda na kuboresha sheria na haki za watoto na umuhimu wake. Akizungumza katika hafla hiyo Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia na watoto PINDI HAZARA CHANA, amesema mtoto anatakiwa kutunzwa,...

Like
191
0
Thursday, 20 November 2014
SERIKALI YASHUGHULIKIA TATIZO LA UPUNGUFU WA DAWA NCHINI
Local News

SERIKALI imeagiza wizara ya Afya na Ustawi wa jamii kushirikiana ipasavyo na wizara ya fedha katika utendaji wao wa kazi ikiwemo uingizwaji na uagizwaji wa dawa ili kuhakikisha kuwa zinapunguza kwa kiasi kikubwa tatizo la upungufu wa dawa katika hospitali zote nchini. Agizo hilo limetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Waziri mkuu mheshimiwa MIZENGO PINDA wakati akijibu swali la mheshimiwa ANTON MBASA aliyetaka kujua mikakati ya serikali katika kuhakikisha tatizo la upungufu wa dawa katika hospitali zote nchini linatatuliwa....

Like
259
0
Thursday, 20 November 2014
30% YA WATU DUNIANI VIBONGE NA WANAVITAMBI
Local News

gharama za unene wa kupitiliza duniani ni  sawa na utumiaji wa bidhaa za tumbaku ukiwemo uvutaji wa sigara au sawa na gharama za vita na kubwa kuliko unywaji wa pombe au mabadiliko ya tabia nchi. Watafiti wanasema Watu wapatao bilioni 2.1 – kiasi cha asilimia 30% ya idadi ya watu duniani- wana uzito wa kupita kiasi au wana vitambi. Wamesema hatua ambazo zinatakiwa kutumiwa ili kutatua tatizo hili ni mtu binafsi kuwajibika kwa ajili ya afya yake. Ripoti hiyo inasema...

Like
403
0
Thursday, 20 November 2014