Local News

KIWANDA CHA KUZALISHA MBOLEA KUNZISHWA LINDI
Local News

SHIRILA la maendeleo ya mafuta na petrol Tanzania (TPDC) kwa kushrikiana na kampuni tatu wanatarajia kuanzisha kiwanda cha kuzalisha mbolea katika wilaya ya kilwa mkoani lindi. Akizungunza wakati wa semina ya siku mbili ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuhusu uelewa wa sekta ndogo ya mafuta na gesi mkurugenzi wa mkondo wa chini kutoka TPDC dokta Wellington Hudson amezitaja baadhi ya kampuni watakazoshirikiana nazo katika ujenzi wa kiwanda hicho kuwa ni pamoja na kampuni ya ferostar ya Ujerumani na haldo...

Like
343
0
Friday, 29 January 2016
SERIKALI YAAHIDI KUWAWEZESHA WAVUVI WADOGO
Local News

SERIKALI imewahakikishia wananchi hususani wavuvi wadogo kuwa itahakikisha inawawezesha wavuvi hao kufanya shughuli zao za uvuvi kwa manufaa ili kujiletea maendeleo yao pamoja na Taifa kwa ujumla. Hayo yamebainishwa leo Bungeni Mjini Dodoma na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi mheshimiwa Mwigulu Nchemba wakati akijibu swali la mbunge wa Jimbo la Mwibara mheshimiwa Kangi Lugola aliyetaka kufahamu jitihada za serikali katika kuwanufaisha wavuvi. Katika majibu ya swali hilo pia mheshimiwa Nchemba amewataka watu wenye dhamana ya kusimamia shughuli...

Like
158
0
Friday, 29 January 2016
SERIKALI YAAHIDI KUENDELEZA UJENZI WA BARABARA KWA KINGO CHA RAMI
Local News

SERIKALI imeahidi kuendelea na ujenzi wa barabara katika maeneo tofauti nchini kwa kiwango cha lami ili kutatua adha kubwa ya ubovu wa barabara ulipo katika maeneo mengi nchini.   Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  Mhandisi Godwin Ngonyani wakati akijibu maswali ya wabunge waliouliza kuhusu mpango wa serikali kuboresha barabara zilizopo.   Akijibu swali la Mhe Richard Mganga Ndassa Mbunge wa Sumve (CCM) Mhandisi Godwin Ngonyani amesema katika mwaka wa fedha 2014/2015 na...

Like
237
0
Thursday, 28 January 2016
SERIKALI YATOLEA UFAFANUZI TAARIFA YA URUSHAJI WA MATANGAZO YA BUNGE
Local News

SERIKALI imetolea ufafanuzi kuhusu taarifa za upotoshaji kwa umma kuwa imefuta vipindi vya shughuli za Bunge kuoneshwa katika televisheni ya Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) zilizoenea katika maeneo mbalimbali.   Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye wakati akizungumza na wananchi moja kwa moja kupitia vyombo mbalimbali vya habari nchini kutolea ufafanuzi taarifa hizo.   Mheshimiwa Nape amesema Serikali haijafuta vipindi vya Bunge bali ilichofanya ni kubadilisha...

Like
205
0
Thursday, 28 January 2016
SERIKALI YATOA UFAFANUZI WA URUSHAJI WA MATANGAZO YA BUNGE
Local News

SERIKALI imesema kuwa kusitishwa kwa baadhi ya matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge haina maana kuwa matangazo hayo hayataoneshwa bali matangazo yataendelea kwa muda husika uliopendekezwa ili kuruhusu Kituo cha matangazo cha Taifa TBC kuendelea na majukumu mengine hata kabla ya kikao cha Bunge kukamilika. Akijibu swali la mheshimiwa Freeman Mbowe leo Bungeni mjini Dodoma katika kipindi cha maswali ya moja kwa moja kwa waziri mkuu, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Kassim Majaliwa...

Like
296
0
Thursday, 28 January 2016
MRADI WA KUCHAKATA TAKA KUJENGWA KINONDONI
Local News

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kinondoni inatarajia kujenga mradi wa kuchakata taka hususani zile zinazozalishwa kwenye masoko yanayopatikana kwenye manispaa hiyo lengo ikiwa ni kuondoa taka hizo ili manispaa iwe safi. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam leo Meya wa Manispaa ya kinondoni Boniface Jacob amesema kuwa mradi huo unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 2 za kitanzania utajengwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Ujerumani, Halmashauri ya Hambag na Halmashauri ya Manispaa ya kinondoni. Boniface ameeleza kuwa kutokana...

Like
267
0
Wednesday, 27 January 2016
MKUU WA MKOA WA PWANI ATOA SIKU 7 ZA KUTUMBUA MAJIPU
Local News

MKUU wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ametoa muda wa siku saba kwa watendaji wa mitaa, watendaji wa kata na  wazazi wenye watoto waliofaulu kuingia kidato cha kwanza lakini hadi sasa wameshindwa  kuwapeleka shule wanafunzi hao, kuwapeleka shule haraka watoto wanafunzi hao.   Mhandisi Ndikilo ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya siku moja katika halmashauri ya mji wa Kibaha  wakati akizungumza na watumishi na watendaji mbalimbali wa serikali na vyama vya siasa ambapo amesema kuwa mzazi ambaye...

Like
252
0
Wednesday, 27 January 2016
WATANZANIA WATAKIWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUSOMA VITABU
Local News

WATANZANIA wametakiwa kujenga utamaduni wa kusoma vitabu ili kukuza uwezo wa ufahamu na kuongeza ujuzi katika utendaji kazi wao wa kila siku. Wito huo umetolewa jana na Waziri wa Elimu, Sayansi,Teknolojia na Ufundi Profesa Joice Ndalichako kwa niaba ya Rais dokta John Pombe Magufuli katika ufunguzi wa Maonesho ya vitabu yanayofanyika katika meli ya Logos Hope inayozunguka katika maeneo mbali mbali duniani kuhamasisha usomaji wa vitabu. Profesa Ndalichako amewataka Walimu na wakufunzi wa shule na vyuo nchini kutembelea katika meli...

Like
248
0
Wednesday, 27 January 2016
SERIKALI YASISITIZA KUTENDA HAKI KWA VIONGOZI WANAORUHUSIWA KUJIHUSISHA NA SIASA
Local News

SERIKALI imesisitiza kuwa ipo makini kuhakikisha kuwa kila kiongozi anayeruhusiwa kujihusisha na masuala ya kisiasa anapata haki yake bila usumbufu wowote. Hayo yamesemwa leo Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa nchi Ofisi ya rais, Utumishi na Utawala bora Mheshimiwa Angela Kairuki wakati akijibu swali la mheshimiwa Hafidhi Ali Tahir Mbunge aliyetaka kufahamu utaratibu wa serikali juu ya watumishi hao. Mheshimiwa Kairuki amesema kuwa watumishi ambao hawaruhusiwi kujihusisha na masuala ya kisiasa ni pamoja na Wanajeshi wa Jeshi la wananchi wa...

Like
177
0
Wednesday, 27 January 2016
HALMASHAURI YA MANISPAA YA ILALA YAPEWA MWEZI MMOJA KUBOMOA JENGO REFU KATIKA MTAA WA INDIRAGHANDI
Local News

WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi mheshimiwa William Lukuvi amewaagiza watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilala na shirika la Nyumba la Taifa kubomoa jengo refu lililojengwa chini ya kiwango katika mtaa wa Indiraghandi ndani ya kipindi cha mwezi mmoja kuanzia jana. Lukuvi ametoa kauli hiyo Jijini Dar es salaam kabla ya kuelekea kwenye ziara fupi ya kikazi wilayani Bagamoyo mkoani Pwani ambapo huko pia amebaini matatizo mbalimbali katika sekta ya Ardhi. Miongoni mwa changamoto alizozikuta ni pamoja...

Like
312
0
Tuesday, 26 January 2016
BUNGE LA 11 LAANZA KUJADILI HOTUBA YA RAIS
Local News

MKUTANO wa pili wa Bunge la 11 umeanza leo mjini Dodoma ambapo Bunge la Jamhuri ya Muungano linajadili hotuba ya Rais kwa muda wa siku tatu aliyoitoa wakati wa ufunguzi wa Bunge hilo. Kikao cha kwanza cha Bunge hilo kimeanza kwa kipindi cha maswali na majibu ambapo baadhi ya wabunge wamepata nafasi ya kuiuliza maswali serikali na kuhoji mikakati mbalimbali inayotarajiwa kufanywa kwa manufaa ya Taifa. Awali kabla ya kipindi cha maswali na majibu kuanza, Spika wa Bunge mheshimiwa Job...

Like
244
0
Tuesday, 26 January 2016