Global News

Zuckerberg akiri kosa lake na kuomba radhi
Global News

Mkurugenzi Mtendaji wa Facebook Mark Zuckerberg ametoa maelezo katika Bunge la Marekani- Congress kwa mara ya kwanza Jumanne, akijibu wasiwasi ulioelezwa na wabunge juu ya kushindwa kwa mtandao wa jamii maarufu kulinda taarifa zao. Taarifa hizo za siri za watumiaji wanaofikia milioni 87 ulimwenguni zilizotumiwa na kampuni yenye kujishughulisha na siasa- Cambridge Analytica iliyokuwa na mafungamano na Trump. Mahojiano hayo yanaendelea Jumatano wakati Zuckerberg atakapokutana katika raundi ya pili kujibu maswali mbele ya jopo la Wabunge wa...

1
353
0
Thursday, 12 April 2018
Marekani inapima hatua za kujibu shambulio ‘kemikali nchini Syria
Global News

Marekani inasema kuwa “tayari ana maamuzi mengi” za kujibu shambulio linaloshukiwa kuwa la kikemikali nchini Syria, huku viongozi wa magharibi wakiendelea kupima hatua za kijeshi. Msemaji wa Ikulu ya White House Sarah Sanders amewaambia wandishi wa habari kuwa hakuna ushahidi wa mwisho uliokwisha chukuliwa juu ya mashambulio ya kijeshi. Lakini amesema Marekani inaziwajibisha Urusi na Syria kwa tukio hilo. Baraza la Kitaifa la Usalama la Marekani litakutana Alhamisi, huku waziri mkuu wa Uingereza PM Theresa May akiitisha mkutano wa...

1
1106
0
Thursday, 12 April 2018
36 wahukumiwa kifo Misri kwa kushambulia makanisa ya Coptic
Global News

Mahakama ya kijeshi huko Misri imewahukumu watu thelathini na sita adhabu ya kifo kutokana na makosa ya mashambulizi dhidi ya makanisa ya Coptic. Watu sabini walikufa kutokana na shambulizi la bomu katika kanisa kuu la ki Coptic mjini Cairo mwishoni mwa mwaka 2016, na makanisa ya Alexandria na Tanta yaliripuliwa siku kama hiyo mwezi wa nne mwaka uliofuata. Tayari kundi la wanamgambo wa kiislamu wenye msiamamo mkali wamekiri kuhusika na mashambulizi hayo matatu. Wameendelea kukiri kuwa kazi yao kubwa ilikuwa...

Like
762
0
Wednesday, 11 April 2018
Trump aapa ”kutumia nguvu” kujibu shambulio ”la kemikali” Syria
Global News

  Rais wa Marekani Donald Trump ameahidi ” kutumia nguvu ” kujibu madai ya shambulio la kemikali nchini Syria, huku mataifa ya magharibi yakitafakari hatua watakayoichukua. “Tuna njia nyingi za kijeshi,”aliwambia waandishi wa habari. Aliongeza kuwa hatua ya kujibu shambulio hilo itaamuliwa katika kipindi cha “muda mfupi”. Bwana Trump alisema kuwa Marekani inapata ”msaada mzuri” juu ya nani aliyehusika na shambulio la Douma Jumamosi. Duru za kitabibu zinasema makumi kadhaa ya watu waliawa...

Like
372
0
Tuesday, 10 April 2018
Brazil: Lula da Silva kufungwa miaka 12 jela
Global News

  Mahakama ya rufaa nchini Brazil imeagiza kuwa aliyekuwa rais wa nchi hiyo, Luiz Inacio Lula da Silva, ni sharti aanze kutumikia kifungo chake cha miaka kumi na miwili gerezani, baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika na ufisadi. Majaji sita kati ya kumi na mmoja wa mahakama ya rufaa walipinga rufaa hiyo huku watano kati yao wakimuunga mkono. Kesi hiyo imezua hali ya wasi wasi wa kisiasa nchini humo. Hatia hiyo imetokana na uchunguzi wa muda mrefu wa sakata...

Like
381
0
Thursday, 05 April 2018
China  Yaiongezea Ushuru wa Forodha Bidhaa za Marekani
Global News

Baada ya kuidhinishwa na Baraza la Serikali ya China, kamati ya Ushuru wa Forodha ya China imeamua kuwa itasimamisha upunguzaji wa ushuru wa Forodha kwa bidhaa 128 za aina 8 zinazoagizwa kutoka Marekani kuanzia jana tarehe 2 Aprili, huku ikiongeza ushuru wa Forodha kwa bidhaa hizo. Ikumbukwe kuwa tarehe 22 Machi, Rais Donald Trump wa Marekani amesaini kumbukumbu ya kuiwekea China vikwazo kwa mujibu wa matokeo ya ripoti kuhusu ukaguzi wa kipengele cha 301 cha sheria ya biashara, na kuagiza...

Like
493
0
Tuesday, 03 April 2018
Trump apongeza mazungumzo kati ya rais Xi na Kim
Global News

Rais wa Marekani Donald Trump amesema leo kuwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un yuko tayari kukutana naye. Kauli hiyo inaashiria kuwa mkutano wa kihistoria unaopangwa kati yake na kiongozi huyo anayetengwa wa nchi ya bara Asia utaendelea. Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Trump ameandika kuwa alipokea ujumbe jana usiku kutoka kwa rais wa China Xi Jinping ukimweleza kuwa mkutano kati yake na Kim Jong Un uliendelea vizuri na kwamba Kim anatarajia kukutana naye. Ameendelea kusema kuwa kwa...

Like
306
0
Thursday, 29 March 2018
Miguna Miguna : Mwanasiasa wa upinzani atimuliwa tena kutoka Kenya na kupelekwa Dubai
Global News

Mwanasiasa wa upinzani Kenya aliyeidhinisha kiapo cha kiongozi wa upinzani Raila Odinga kuwa ‘Rais wa Wananchi’ Januari Miguna Miguna ametimuliwa tena kutoka nchini humo. Mwanasiasa huyo ametimuliwa huku mzozo kuhusu uraia wake ukiendelea. Bw Miguna ameandika kwenye Facebook kwamba ameamka na kujipata yuko Dubai na kwamba anahitaji matibabu. Amesema anafahamu kwamba kuna mpango wa kumpeleka London lakini anataka kupanda ndege ya kurejea Nairobi pekee. Mwanasiasa huyo amesema amesindikizwa na afisa wa idara ya ujasusi. Serikali...

Like
523
0
Thursday, 29 March 2018
Imethibitishwa Kweli Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amezuru China
Global News

Baada ya siku ya uvumi wa siku nyingi, imethibitishwa kwamba kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amezuru China. Ziara hiyo, ambayo ilithibitishwa na China na Korea Kaskazini, ndiyo ya kwanza inayofahamika ya Bw Kim nje ya taifa lake tangu alipochukua mamlaka mwaka 2011. Bw Kim alifanya “mazungumzo ya kufana” na kiongozi wa China Xi Jinping mjini Beijing, shirika la habari la China, Xinhua liliripoti. China ni mshirika mkuu wa Korea Kaskazini kiuchumi na baadhi ya wachambuzi wanasema uwezekano wa wawili...

Like
558
0
Wednesday, 28 March 2018
Tiangong-1: Kituo cha safari za anga cha Uchina kinaweza kuanguka duniani ”karibuni”
Global News

Kifusi kutoka kwa kituo cha maabara cha safari za anga cha China, kinaweza kupasuka na kuanguka duniani Ijumaa,wanasayansi wanaokifanyia uchunguzi wanasema. Kituo hicho cha Tiangong-1 ni sehemu ya mpango wa safari za anga za mbali wa Uchina, na wa sampuli ya kituo cha safari za anga za mbali cha binadamu wa mwaka 2022. Kiliwekwa kwenye uzio mwaka 2011 na miaka mitano baadae kikamilisha shughuli yake, na baadae kilitarajiwa kuanguka duniani. Muda na mahala kitakapoangukia ni vigumu kutabiri kwasababu sasa hakidhibitiwi....

Like
376
0
Tuesday, 27 March 2018
Uvumi waenea kuhusu ziara ya Kim Jong-un Beijing
Global News

Uvumi waenea kuhusu ziara ya Kim Jong-un Beijing Uvumi kuhusu ziara ya kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un mjini Beijing umehanikiza katika wakati ambapo kukiwa na gumzo kuhusu maandalizi ya mkutano wa kilele kati ya kiongozi huyo wa Korea Kaskazini na rais Trump. Mji Mkuu wa China Beijing, ulikuwa chini ya usalama mkali Jumanne, huku kukiwa na uvumi kwamba kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un alikuwa anafanya ziara ya kustukiza, kufuatia ripoti za kuwasili kutoka Pyongyang, kwa treni maalumu iliyopokelewa...

Like
344
0
Tuesday, 27 March 2018