Global News

EL NINO KUATHIRI MAMILIONI YA WATU 2016
Global News

MASHIRIKA ya misaada yamesema kuwa hali ya hewa ya El Nino ambayo imekuwa ndiyo kali zaidi katika historia itazidisha hatari ya njaa na maradhi kwa mamilioni ya watu duniani 2016.   Hali hii ya hewa inatarajiwa kusababisha ukame baadhi ya maeneo na mafuriko kwingine, ambapo baadhi ya maeneo yanayotarajiwa kuathirika sana yako Afrika, huku uhaba wa chakula ukitarajiwa kufikia kilele mwezi Februari.   Hali ya hewa ya El Nino, hutokana na kuongezeka kwa joto na huathiri hali ya hewa maeneo...

Like
165
0
Wednesday, 30 December 2015
AU YATISHIA MAKUNDI HASIMU BURUNDI
Global News

UMOJA  wa  Afrika  leo  umetishia  kuyawekea vikwazo makundi  hasimu  nchini  Burundi  iwapo  yatashindwa kuhudhuria  mazungumzo  ya  amani  mwezi  ujao, wakati ukiibana  serikali   kukubali jeshi  la  kulinda  amani. Serikali  ya  Burundi  na  upinzani, pande  zilizokutana nchini  Uganda  siku  ya  Jumatatu,  zinatarajiwa  kukutana tena  Januari  Mjini Arusha kwa  mazungumzo  yenye  lengo  la  kumaliza miezi  kadhaa  ya ...

Like
183
0
Wednesday, 30 December 2015
UCHAGUZI WAANZA AFRIKA YA KATI
Global News

WANANCHI wa  Jamuhuri ya Afrika ya kati hii leo wanashiriki katika zoezi la uchaguzi wa Rais na wabunge  nchini humo.   Uchaguzi huo uliokuwa ufanyike tarehe 27 mwezi huu ulisogezwa mbele na tume ya uchaguzi nchini humo hadi  tarehe ya leo Desemba 30 kutokana na kasoro zilizojitokeza wakati wa kipindi cha maandalizi ya uchaguzi huo.   Msemaji wa Tume ya uchaguzi nchini humo Julius Rufin Ngoadebaba ameahidi kuwa uchaguzi huo utakwenda vizuri katika maeneo yote nchini humo  ambako Zaidi ya...

Like
177
0
Wednesday, 30 December 2015
MAREKANI YAFANYA MASHAMBULIZI YA ANGA DHIDI YA IS
Global News

MASHAMBULIZI ya angani yanayoongozwa na Marekani yamefanikisha kuwaua viongozi kumi wa kundi la itikadi kali la  Dola la Kiisilamu katika kipindi cha mwezi uliopita wakiwemo wanaodaiwa kuhusika  na shambulizi la mjini Paris au mashambulizi mengine ambayo yalipangwa kufanyika barani ulaya .   Afisa  mmoja  wa jeshi la Marekani nchini Iraq  Kanali Steve  Warren amesema wanamgambo hao waliuawa wakati wa mashambulizi ya anga yaliyofanywa nchini Iraq na Syria.   Kwa mujibu wa Warren mmoja wa walioua katika mashambulizi hayo ni...

Like
211
0
Wednesday, 30 December 2015
MELI ILIYOBEBA MADINI YA URANI YANG’OA NANGA IRAN
Global News

MELI iliyobeba kilo 11,000 za madini ya Urani ambayo yamerutubishwa kwa kiwango kidogo imeng’oa nanga nchini Iran ikielekea Urusi, katika hatua ya Iran kutekeleza makubaliano kuhusu mpango wake wa nyuklia ambayo yalifikiwa tarehe 14 Julai baina yake na mataifa yenye nguvu duniani. Hayo yamethibitishwa na Marekani. Huku kipengele muhimu cha makubaliano hayo kinaitaka Iran kupunguza akiba yake ya madini ya Urani yaliyorutubishwa kiasi hadi chini ya kilo 300. Yakirutubishwa zaidi, madini hayo yanaweza kutumiwa kuunda silaha za nyuklia, azma...

Like
225
0
Tuesday, 29 December 2015
WAZIRI MKUU WA ZAMANI WA ISRAEL AHUKUMIWA MIEZI 18 JELA
Global News

WAZIRI MKUU wa zamani wa Israel Ehud Olmert ametakiwa kutumikia kifungo cha miezi 18 jela kwa makosa ya rushwa. Olmert alikuwa amehukumiwa kifungo cha miaka sita jela na mahakama mwaka 2014, lakini adhabu hiyo sasa imepunguzwa na Mahakama ya Juu. Mwanasiasa huyo wa umri wa miaka 70 alipatikana na hatia kuhusu mkataba wa ujenzi wa nyumba ambao ulifanyika alipokuwa meya wa Jerusalem, kabla yake kuwa waziri mkuu...

Like
160
0
Tuesday, 29 December 2015
MAREKANI YALIPONGEZA JESHI LA IRAQ KWA KUUREJESHA MJI WA RAMADI
Global News

MAREKANI imelipongeza jeshi la Iraq kwa kuweza kuurejesha mji wa Ramadi uliokuwa ukishikiliwa na wapiganaji wa Islamic State. Waziri wa Ulinzi wa Marekani Ash Carter  amesifu hatua hiyo kwa kusema ni muhimu katika kulishinda kundi hilo, aliloliita kuwa ni la kipuuzi. Amesema ni muhimu pia kwa mamlaka za Iraq kwa kupata nasafi ya kudhibiti amani katika mji huo wa Ramadi na kudhibiti kurudi tena kwa kundi hilo la IS....

Like
189
0
Tuesday, 29 December 2015
WHO KUITANGAZA GUINEA NCHI ISIYO NA EBOLA
Global News

SHIRIKA la Afya Duniani leo linatarajiwa kuitangaza Guinea kuwa nchi isiyo na maambukizo ya ugonjwa wa Ebola. Mlipuko wa virusi vya ugonjwa wa Ebola ulianza nchini humo miaka miwili iliyopita. Ugonjwa wa Ebola umesababisha vifo vya maelfu ya watu katika nchi za Afrika magharibi, hususan katika nchi za Guinea, Liberia na Sierra Leone. Waguinea wanajiandaa kusherehekea kumalizika kwa janga hilo nchini mwao kwa kufanya maonesho na kurusha...

Like
130
0
Tuesday, 29 December 2015
KIMBUNGA CHAUA WATU 43 MAREKANI
Global News

WATU 43 wameuawa katika kipindi cha siku tano zilizopita kutokana na kimbunga maeneo ya kusini na magharibi mwa Marekani. Mafuriko, upepo mkali na barafu vimeharibu mamia ya nyumba na biashara na hivyo kuyumbisha shughuli za uchukuzi. Idara ya taifa ya utabiri wa hali ya hewa nchini humo imetoa tahadhari ya kutokea kwa vimbunga katika majimbo ya Texas, Arkansas, Louisiana, Oklahoma and...

Like
183
0
Monday, 28 December 2015
WATU 2 WAUAWA MANDERA
Global News

WATU wawili wamefariki na wengine watatu kujeruhiwa baada ya wanajeshi kufyatulia risasi gari moja mjini Mandera katika hali ya kutatanisha. Wanajeshi wamekuwa wakifanya operesheni kali mjini humo baada ya kuripotiwa kwa visa kadha vya mashambulio ya kigaidi siku za hivi karibuni. Maafisa wanne wa polisi wameuawa kwenye mashambulio kadha katika mji huo ulioko kaskazini mashariki mwa Kenya katika kipindi cha wiki...

Like
181
0
Monday, 28 December 2015
ALIYEKUWA MLINZI WA OSAMA BIN LADEN AFARIKI DUNIA
Global News

Taarifa kutoka Yemen zinasema aliyekuwa mlinzi wa Osama Bin Laden, amefariki dunia baada ya kuugua kwa muda mrefu. Vyanzo vya habari vya kitabibu vinaeleza  kwamba Nasser al Bahri ambaye pia alikuwa akijulikana kama Abu Jandal alifariki siku ya Jumamosi, katika Hospitali iliyoko kwenye mji wa Mukalla kusini mwa Yemen. Alirudi nchini humo mwishoni mwa mwaka 2008, baada ya kuachiliwa kutoka katika kizuizi alichowekewa na Marekani huko...

Like
265
0
Monday, 28 December 2015