Global News

SUDAN KUSINI YAKABILIWA NA UKOSEFU WA CHAKULA
Global News

MIAKA miwili tangu machafuko yalipoanza Sudan kusini, mashirika ya misaada yametahadharisha kuhusu upungufu mkubwa wa chakula unaotarajia kuikumba nchi hiyo na kutaka hatua za haraka zichukuliwe ili kumaliza vitendo vya uhalifu wa kivita ndani ya Taifa hilo. Ingawa makubaliano ya amani yalitiwa saini miezi kadhaa iliyopita, machafuko bado yanaendelea na karibu watu milioni moja na laki Tano wamelazimika kuyahama makazi yao. Tangu kuanza kwa mapigano nchi nzima miaka miwili iliyopita, Rais na makamu wa rais wa zamani wa nchi hiyo...

Like
126
0
Tuesday, 15 December 2015
KERRY NA PUTIN KUIJADILI SYRIA
Global News

WAZIRI wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry yupo nchini Moscow kwa ajili ya mazungumzo na Rais Vladimir Putin kuhusu njia za kumaliza vita vinavyoendelea nchini Syria. Mazungumzo hayo yanalenga kupunguza mfarakano kati ya Urusi na Marekani, hasa kuhusu makundi ambayo yanafaa kujumuishwa kwenye mazungumzo ya mzozo huo. Urusi ambayo inamuunga mkono Rais wa Syria Bashar Al-Assad, imesema mkutano uliofanyika mwishoni mwa wiki iliyopita wa makundi yanayopinga serikali ya Syria haukuwakilisha makundi yote yanayovutana katika mzozo...

Like
106
0
Tuesday, 15 December 2015
JESHI LA NIGERIA LABOMOA MADHABAHU YA KISHIA
Global News

KUNDI kuu la kiislamu nchini Nigeria linaloungwa mkono na waislamu wa Kishia wa Iran, linasema kuwa mke wa kiongozi mkuu Sheikh Ibrahim Zakzaky, ameuwawa katika makabiliano na jeshi kaskazini mwa mji wa Zaria.   Vuguvugu la kiislamu nchini Nigeria (IMN) linadai kuwa Zeenat Ibraheem ameuwawa kwa pamoja na mwanaye Sayyid Ibraheem Zakzaky.   Sheikh Zakzaky alikamatwa na wanajeshi waliozingira nyumba yao kufuatia madai kuwa wanachama wa kundi hilo walijaribu kumuua kamanda mkuu wa jeshi Jenerali Tukur Buratai huko Zaria siku...

Like
153
0
Monday, 14 December 2015
MISRI: HAKUNA USHAHIDI NDEGE YA URUSI ILIDUNGULIWA
Global News

MAAFISA wa upelelezi wa ajali za ndege kutoka Misri wamesema kuwa hawajapata ushahidi wowote kuwa ndege ya Urusi iliyoanguka katika rasi ya Sinai na kuua watu 224 ililipuliwa.   Ndege hiyo iliyokuwa ikitokea Sharm el-Sheikh ikielekea Moscow ilianguka jangwani mwezi Oktoba.   Kundi moja la wapiganaji wanaoliunga mkono kundi la Islamic State –IS, walidai kuwa wao ndio walioidungua ndege...

Like
153
0
Monday, 14 December 2015
MACHAFUKO: RAIA WA MAREKANI KUONDOKA BURUNDI
Global News

SERIKALI ya Marekani imeshauri Raia wake walio nchini Burundi kuondoka nchini humo haraka iwezekanavyo baada ya watu 87 kuuawa kwenye ghasia zilizotokea siku ya Ijumaa.   Ghasia zilizojitokeza kwenye mitaa ya mji mkuu wa nchi hiyo, Bujumbura ni mbaya zaidi tangu kuanza kwa vurugu mwezi Aprili mwaka huu , baada ya Rais Pierre Nkurunziza kuamua kuwania tena urais kwa muhula wa tatu.   Shirika la kutetea haki za kibinadamu la Human Rights Watch (HRW) limeitisha uchunguzi kuhusu mauaji hayo ya...

Like
171
0
Monday, 14 December 2015
MAREKANI NA CHINA KUENDELEZA USHIRIKIANO JUU YA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI
Global News

RAIS Xi Jinping wa China na Barack Obama wa Marekani walikuwa na mazungumzo ya simu leo na kuahidi kwamba nchi zao zitaendelea kushirikiana  katika suala la mabadiliko ya tabia nchi. Televisheni ya taifa  nchini China  imeripoti kwamba marais hao wawili wamesema watashirikiana kwa karibu kuendeleza mafanikio yatakayotokana na mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu tabia nchi unaoendelea mjini Paris, Nchini Ufaransa....

Like
190
0
Friday, 11 December 2015
NEC YAWATAKA WANANCHI KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA
Global News

TUME ya Taifa ya Uchaguzi nchini-NEC-imewataka Wananchi waliojiandikisha kupiga Kura katika Majimbo na Kata husika, kujitokeza kwenye vituo walikojiandikisha siku ya Jumapili ili kuweza kupiga Kura na kuwachagua viongozi wanaowataka.   Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari Mwenyekiti wa Tume hiyo Jaji Mstaafu Damiani Lubuva amesisitiza kwamba taratibu zilizotumika katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 25 mwaka huu ndizo zitakazotumika katika uchaguzi...

Like
183
0
Friday, 11 December 2015
AMNESTY INTERNATIONAL YATUHUMU MUUNGANO UNAOONGOZWA NA SAUDI ARABIA
Global News

SHIRIKA  la  kutetea  haki  za  binadamu la  Amnesty International limesema  jana  kuwa  muungano unaoongozwa  na  Saudi  Arabia umeshambulia  kwa mabomu shule  nchini  Yemen, na  kukiuka sheria  za kimataifa  za  kiutu na kuzuwia  maelfu  ya  watoto  kupata elimu.   Shirika  hilo  lenye makao  yake  makuu  mjini  London limeyataka  mataifa  yote  ambayo  yanaupatia  silaha muungano wa  kijeshi  unaoongozwa  na  Saudi Arabia , ikiwa ni  pamoja  na  Marekani na  Uingereza, kusitisha  upelekaji...

Like
163
0
Friday, 11 December 2015
MKUTANO MKUU KUJADILI MABADILIKO YA TABIA YA NCHI WAENDELEA PARIS
Global News

WAZIRI wa mambo ya nje wa Ufaransa, Laurent Fabius, amewasilisha rasimu ya mkataba mpya kwa wajumbe katika mkutano mkuu unaojadili kuhusiana na mabadiliko ya tabia nchi mjini Paris, kwa usiku wa pili wa majadiliano. Fabius amesema kwamba lengo lao kuu ni kuhitimisha mazungumzo kwa dhima, sheria, matarajio,na makubaliano ya haki na ya kudumu mpaka kufikia leo, nakuongeza kusema kwamba wajumbe wa mkutano huo wanakaribia kufikia makubaliano ya mwisho. Awali, mkurugenzi wa kitengo cha Umoja wa Mataifa kinachojishughulisha na mazingira, Achim...

Like
220
0
Friday, 11 December 2015
MPIGANAJI WA MWISHO WA TALIBAN AUAWA KANDAHAR
Global News

MPIGANAJI wa mwisho kati ya wapiganaji 11 wa Taliban ambao waliuzingira uwanja wa ndege wa Kandahar, Afghanistan ameuawa, zaidi ya saa 24, baada ya shambulizi kuanzishwa.   Wizara ya Ulinzi ya Afghanistan imesema leo kuwa watu 50 wakiwemo raia na maafisa wa usalama, wameuawa.   Shambulizi hilo ambalo ni kubwa dhidi ya kambi ya jeshi la anga nchini humo, lilifanyika sambamba na mkutano wa kikanda nchini Pakistan, ambako Rais Ashraf Ghani wa Afghanistan aliitaka Pakistan kusaidia kuanzisha tena mazungumzo ya...

Like
211
0
Thursday, 10 December 2015
MAKABURI: VIONGOZI WA MANDERA WAKAMATWA
Global News

VIONGOZI kadha kutoka eneo la Mandera, kaskazini mashariki mwa Kenya, wamekamatwa na polisi kuhusiana na madai ya kuwepo kwa makaburi yaliyozikwa miili ya watu kadha. Seneta Billow Kerrow amekamatwa pamoja na wabunge wengine wanne baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa Wilson, Nairobi na kupelekwa makao makuu ya uchunguzi upande wa akosa ya...

Like
157
0
Thursday, 10 December 2015