Global News

JESHI LA KENYA LATUHUMIWA KUFANYA BIASHARA SOMALIA
Global News

JESHI la Kenya limetuhumiwa kujihusisha na shughuli mbalimbali kinyume na malengo ikiwemo kufanya biashara badala ya kufanya kazi zinazowahusu nchini Somalia. Taasisi ya Waandishi wa habari Wanaopigania haki imelituhumu Jeshi hilo kujiingiza katika masuala mbalimbali ya kibiashara yanayowaletea faida na kuacha kazi ya iliyowapeleka ya kulinda Amani. Hata hivyo Taasisi hiyo imewalaumu baadhi ya maofisa wa jeshi hilo kushirikiana katika biashara haramu na wapiganaji wa Al Shabaab jambo ambalo ni kinyume cha...

Like
234
0
Thursday, 12 November 2015
MYANMAR: KIONGOZI WA UPINZANI ATOA WITO KUFANYIKA MAZUNGUMZO YA KITAIFA
Global News

KIONGOZI wa upinzani nchini Myanmar Aung Suu Kyi, leo ametoa  wito  wa kuwepo kwa  mazungumzo  ya  kitaifa  ya upatanishi  kati ya rais  wa  Myanmar  na  mkuu  wa  jeshi  la nchi  hiyo  lenye  nguvu  kubwa  kisiasa  baada ya chama chake kuonekana  kupata  ushindi  wa  kishindo katika Uchaguzi mkuu. Chama  cha  National League for  Demcracy-NLD-kimeonekana kupata madaraka  baada  ya  kupata asilimia  90  ya  viti vilivyotangazwa  hadi  sasa sawa na viti 163 kati  ya  viti 182 vilivyotangazwa  hadi sasa....

Like
129
0
Wednesday, 11 November 2015
AFRIKA KUSINI: POLISI WANANE WAFUNGWA JELA
Global News

MAAFISA wanane wa polisi waliopatikana na hatia ya kumfanyia ukatili dereva wa teksi kutoka Msumbiji mwaka 2013 wamehukumiwa kifungo cha miaka 15 kila mmoja. Maafisa hao walinaswa kwenye kanda ya video wakimburuza dereva wa gari ndogo (teksi) kutoka Msumbuji aliyetambuliwa kwa jina la Macia mwenye umri wa miaka 27 mtaa wa Macia mashariki mwa Johannesburg. Awali kabla ya kutokea kwa tukio hilo Macia alikuwa amesimamishwa na maafisa tisa wa polisi kwa kosa la kuvunja sheria za usalama...

Like
161
0
Wednesday, 11 November 2015
MPANGO WA CHANJO YA HOMA YA UTI WA MGONGO WAFANIKIWA AFRIKA
Global News

WATAALAMU wa Afya wamesema kuwa mpango wa chanjo kwa umma dhidi ya homa ya uti wa mgongo barani Afrika umepata mafanikio makubwa. Zaidi ya watu milioni mbili walipata kinga dhidi ya maradhi hayo katika nchi 16 barani Afrika, ikiwemo Gambia na Ethiopia. Shirika la Afya Duniani limesema katika kipindi cha mwaka 2013 kulikuwa na wagonjwa wanne wa Uti wa mgongo barani Afrika ingawa awali iliweka rekodi ya kuwa na maelfu ya vifo vinavyotokana na ugonjwa huo kila...

Like
209
0
Wednesday, 11 November 2015
DONALD TRUMP ASHTUMIWA VIKALI KWA KUPANGA KUTIMUA WAHAMIAJI
Global News

DONALD TRUMP, mmoja wa wanaowania nafasi ya Urais kupitia chama cha Republican katika Uchaguzi mkuu nchini Marekani, ameshutumiwa vikali kutokana na mpango wake wa kuwafukuza wahamiaji milioni 11 kutoka nchini humo. Kwenye mdahalo wa moja kwa moja kupitia runinga, wagombea wengine wawili wanaoshindana naye, John Kasich na Jeb Bush, waliukosoa vikali mpango huo wakisema hauwezi kutekelezeka na ni kitendo cha ubaguzi. Hali hiyo imesababisha watu waliohudhuria mdahalo huo kumzomea Trump, wakati alipojaribu kujitetea kuhusu huo mpango...

Like
138
0
Wednesday, 11 November 2015
MAREKANI NA ISRAEL ZAKUBALIANA KUWEKA KANDO MVUTANO
Global News

RAIS wa Marekani Barack Obama na waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu wamekubaliana kuweka kando mvutano uliosababishwa na kutiwa saini makubaliano ya mradi wa nyuklia wa Iran na kuweka nguvu za pamoja kutetea maslahi ya nchi zao mbili katika eneo la mashariki ya kati.   Wakifanya mkutano wa pamoja kwa mara ya kwanza baada ya kupita miezi 13 katika Ikulu ya Marekani rais Obama amesema wazi kuwa usalama wa Israel ndio suala muhimu.   Rais Obama na waziri mkuu wa...

Like
173
0
Tuesday, 10 November 2015
SUU KYI: UCHAGUZI ULIKUWA WA HAKI MYNMAR
Global News

KIONGOZI wa upinzani nchini Myanmar Bi. Suu Kyi amesema kwamba uchaguzi mkuu uliofanyika Jumapili iliyopita nchini humo haukuwa huru lakini ulikuwa wa haki. Kwenye mahojiano ya kipekee, Bi Suu Kyi aliwapongeza wananchi wa Myanmar kwa kumpigia kura ingawa Chini ya katiba ya nchi hiyo hawezi akawa rais, lakini amesema kwamba kama kiongozi wa chama atamteua rais. Uchaguz huo umechukuliwa na wengi kuwa ndio wa kidemokrasia zaidi katika kipindi cha miaka 25, baada ya miongo kadhaa ya uongozi wa...

Like
293
0
Tuesday, 10 November 2015
CHAD YATANGAZA HALI YA HATARI
Global News

CHAD imetangaza hali ya hatari eneo la Ziwa Chad baada ya kuongezeka kwa mashambulio kutoka kwa wapiganaji wa Boko Haram kutoka Nigeria. Uamuzi huo umechukuliwa baada ya watu wawili kuuawa katika shambulio la kujitoa mhanga linalodaiwa kutekelezwa na kundi la wanamgambo hao. Boko Haram wanashukiwa kuhusika katika mauaji ya watu wawili katika kijiji kimoja nchini Chad Jumapili iliyopita na wakimbizi watatu kutoka Nigeria kaskazini mwa Cameroon...

Like
236
0
Tuesday, 10 November 2015
UFARANSA YAPENDEKEZA HATUA KALI KUSITISHA MAUAJI BURUNDI
Global News

UFARANSA imependekeza hatua kali zichukuliwe kwaajili ya kusitisha mauaji ambayo yamekuwa yakiendelea nchini Burundi. Taifa hilo liliwasilisha muswada wa mapendekezo kwa Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa Jumatatu iliyopita likieleza wasiwasi wake juu ya hali ya usalama nchini Burundi. Ghasia zilianza mwezi Aprili baada ya maandamano ya kupinga hatua ya Rais Pierre Nkurunziza kutangaza kuwania urais kwa muhula wa tatu huku ikiaminika kuwa Machafuko hayo ndiyo mabaya zaidi nchini humo katika kipindi cha miaka kumi...

Like
225
0
Tuesday, 10 November 2015
MKURUGENZI MKUU WA MTN AJIUZULU
Global News

MKURUGENZI Mkuu wa kampuni ya simu ya MTN amejiuzulu kufuatia kampuni hiyo kutozwa faini kubwa ya dola bilioni 5.2 na Nigeria Mkuu huyo wa kampuni hiyo kubwa zaidi barani Afrika Sifiso Dabengwa, aliwasilisha barua ya kujiuzulu mara moja kwa maslahi ya wenye hisa na uendelevu wa kampuni hiyo. Faini hiyo ilitozwa na Tume ya mawasiliano ya Nigeria kufuatia uamuzi wa MTN kukataa kuzima namba za simu ambazo hazijasajiliwa kwa mujibu wa kanuni mpya za Taifa hilo....

Like
305
0
Monday, 09 November 2015
IRAN YAIMARISHA ULINZI DHIDI YA URUSI
Global News

IMEELEZWA kuwa nchi ya Iran imenunua silaha kali ya ulinzi dhidi ya ndege za kivita na makombora kutoka Urusi ikiwemo Mtambo wa S-300 wenye uwezo wa kudungua ndege na makombora yakiwa umbali wa kilomita 300. Hii si mara ya kwanza kwa Urusi kufanya makubaliano kama hayo na Iran ambapo Mwaka wa 2007 mataifa hayo yalikubaliana kuhusiana na mitambo hiyo ya ulinzi wa anga lakini walisitisha utekelezaji wake kufuatia marufuku iliyowekewa Iran kutokana na mipango yake ya kumiliki silaha za nyuklia....

Like
303
0
Monday, 09 November 2015