Sports

PICHA: E-FM VS MAGOGONI VETERANI MUZIKI MNENE BAR KWA BAR 2015
Slider

Mchezo wa mpira wa miguu kati ya E-fm Vs Magogoni Veterani umemalizika katika uwanja wa Ufukoni huku matokeo ya mchezo huo yakiwaweka vifua mbele maveterani wa Magogoni wakiwa na ushindi wa magoli 4 – 2. Efm ndio walikuwa wa kwanza kuliona lango la Magogoni Veterani mpaka kipindi cha mapumziko Efm walikuwa mbele kwa magoli mawili kwa moja. Hali ilibadilika katika kipindi cha pili ambapo maveterani wa Magogoni waliongeza mashambulizi katika lango la Efm na kuweza kupata magoli matatu ya haraka....

Like
371
0
Saturday, 10 October 2015
KAMATI YATAKA BLATTER ASIMAMISHWE KAZI
Slider

Kamati ya maadili katika shirikisho la soka duniani FIFA imependekeza Rais wa shirikisho la soka duniani FIFA asimamishwe kazi kwa siku tisaini. Wanachama wa kamati hiyo walikutana wiki hii baada ya Jaji mkuu nchini Uswizi kufungua mashtaka ya uhalifu dhidi ya Blatter mwezi uliopita. Blatter anatuhumiwa kwa kutia saini kandarasi zisizo na manufaa yoyote kwa FIFA mbali na kufanya ‘malipo’ kwa rais wa shirikisho la UEFA Michel Platini. Blatter ambaye ni raia wa Uswizi amekuwa rais wa FIFA tangu mwaka...

Like
172
0
Thursday, 08 October 2015
SAMATTA NA ULIMWENGU WANG’AA STARS
Slider

Chini ya mwalimu mzawa Charles Boniface Mkwasa, kikosi cha timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) kimeendelea kuonyesha mabadiliko ya hali ya juu kufuatia mchezo wao dhidi ya timu ya taifa ya Malawi. Stars imefanikiwa kuitandika Malawi 2-0 katika uwanja wa taifa jijini Daresalaam katika mchezo wa kuwania kucheza Kombe la Dunia . Magoli ya stars yalitiwa nyavuni na Mbwana Samatta  pamoja na Thomas Ulimwengu katika kipindi cha kwanza magoli yaliyodumu hadi mwisho wa...

Like
203
0
Thursday, 08 October 2015
LIVERPOOL YAMTIMUA BRENDAN RODGERS
Slider

Klabu ya soka ya Uingereza Liverpool imemtimua meneja wake Brendan Rodgers siku ya jana baada ya kuitumikia klabu hiyo kwa miaka mitatu na nusu. Baada ya maamuzi hayo kufanyika aliyekuwa bosi wa klabu ya Borussia Dortmund, Jurgen Klopp anatazamwa kuwa chaguo la kwanza kuchukua nafasi ya Brendan Rodgers Maamuzi ya kumtimua Rodgers yalifikiwa siku ya jumapili kabla ya kutoka sare ya 1-1 kwenye mchezo wao dhidi ya Everton Uongozi wa klabu hiyo katika maelezo waliyoyatoa wanaamini hayo ni miongoni mwa...

Like
233
0
Monday, 05 October 2015
Slider

Mapenzi ya dhati tumeyashuhudia katika mji wa kihistoria wa Bagamoyo kwenye mchezo wa mpira wa miguu kati ya E-fm Vs Bagamoyo veterani. mchezo huu ulichezwa katika uwanja wa Mwanakalenge hapa Bagamoyo Tunatoa pongezi kwa Bagamoyo Veterani kwa ushindi wa goli 1-0 Burudani inahamia ADON LODGE MAGETI MIA KWENYE MUZIKI MNENE BAR KWA BAR 2015 Leo muziki utaongea kwenye viwanja hivi kwakuwakutanisha Rdj’s na watangazaji wa efm ‪#‎MuzikiMnenebarkwabar2015‬ ni bure hakuna kiingi MATUKIO KATIKA PICHA KIKOSI CHA E-FM KWENYE PICHA YA...

Like
461
0
Saturday, 03 October 2015
MASAIBU YA DIEGO COSTA YAONGEZEKA
Slider

Kocha wa Uhispania Vicente de Bosque amemuacha nje mshambuliaji wa timu hiyo Diego Costa kwa mechi mbili za kufuzu kwa michuano ya mabingwa Ulaya mwaka ujao. Costa anahudumia marufuku ya mechi moja kwa kupata kadi nyingi za njano na alikuwa hawezi kucheza mechi ya kwanza dhidi ya Luxembourg mnamo tarehe 9 mwezi Octoba. Del Bosque:Tumeona tusimshirikishe kwa mechi ya pili dhidi ya Ukraine. ”Hachezi vibaya”,Del Bosque alisema kuhusu Costa,na kuongezea kwamba Uhispania itamshirikisha katika mechi za usoni iwapo kila kitu...

Like
255
0
Saturday, 03 October 2015
VPL: YANGA, SIMBA NA AZAM MWENDO WA KUGAWA DOZI
Slider

Miamba ya soka Tanzania Yanga, Simba pamoja na Azam FC wameendelea kung’aa katika michezo ya ligi kuu iliyotimua vumbi hapo jana. Katika jiji la Morogoro Mtibwa Sugar iliikaribisha Yanga huku mchezo huo ukimalizika kwa wenyeji hao wakilazimika kupokea kichapo cha magoli 2-0 magoli yaliyotiwa nyavuni na Malimi Busungu na Donald Ngoma matokeo yanayoifanya klabu hii kongwe kuwa kileleni na kuongoza ligi kwa alama 15. Azam nao wakiwa katika uwanja wao wa nyumbani Azam Complex wameiadhibu klabu ya Coastal Union ya...

Like
322
0
Thursday, 01 October 2015
MOURINHO APONYEKA SAKATA LA DAKTARI EVA CARNEIRO
Slider

Meneja wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho hataadhibiwa na Chama cha Soka cha England FA,baada ya kuthibitika hakutumia lugha mbaya dhidi ya aliyekuwa daktari wa timu Eva Carneiro. Fa ilipitia mikanda ya video iliyohusika na tukio hilo la Kocha Jose Mourinho na Eva Carneiro ambapo ilionekana kama kocha huyu alitumia lugha chafu kwa daktari huyo. Dokta Carneiro aliingia uwanjani kumtibu mshambuliaji Eden Hazard wakati wa dakika za lala salama kwenye mchezo wa ligi dhidi ya Swansea, uliomalizika kwa sare ya...

Like
259
0
Thursday, 01 October 2015
WENGER AGOMA KUMJIBU MOURINHO
Slider

Meneja wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger  amekataa kujibu chokochoko za Jose Jose Mourinho na kuonyesha zaidi kuwa na malengo na klabu yake. Mourinho alitoa maneno ambayo kimsingi hayakumtaja Wenger moja kwa moja ila kwa tafsiri ya ndani inaonyesha meneja huyu wa Chelsea alilenga kumsema Arsene Wenger. katika maelezo yake Mourinho alitaja kufanana kwa waalimu wa timu zote zinazoshiriki ligi ya Uingereza kuwa na presha ya kutotaka kufanya vibaya hali inayowafanya wawe na kazi ngumu katika kuhakikisha wanafikia malengo huku akiwataja...

Like
188
0
Tuesday, 29 September 2015
HAMILTON ATWAA TAJI LA JAPAN GP
Slider

Dereva wa magari yaendayo kasi Lewis Hamilton ameshinda michuano ya Suzuki na kutwaa taji la 41 katika mchezo huo. Dereva huyu wa timu Mercedes, alishinda taji hilo na kumfikia mkongwe wa michuano ya Fomula 1 Mbrazili Ayrton Senna. Hamilton alimzidi kwa alama 48 dereva mwenzake wa timu ya Mercedes, Nico Rosberg, katika mbio za michuano hiyo ya Grand prix. Kukiwa kumesalia mbio tano Hamilton, anashikilia alama 48 zaidi ya Rosberg, huku akionekana na uwezo wa kushinda taji lingine la tatu...

Like
239
0
Monday, 28 September 2015
EFM MUZIKI MNENE BAR KWA BAR KIBAHA 2015
Entertanment

93.7 EFM yajinyakulia ushindi baada ya kuwafunga kibaha veterans mabao mawili kwa moja, katika mchezo uliochezwa jumamosi ya juzi katika uwanja wa Tamco kibaha. Mechi hiyo ni baadhi ya mechi zinazoendelea baina ya EFM na timu mbalimbali za wasikilizaji wake, Kupitia kampeni ya Muziki mnene bar kwa bar .   Burudani haikuishia hapo, baada ya mechi hiyo shangwe ziliendelea ndani ya kibaha kontena. Ilikuwa ni bandika bandua ya ngoma kali kutoka kwa Rdj’s wa 93.7 EFM na shamra shamra kutoka...

Like
699
0
Monday, 28 September 2015