Sports

UBAGUZI: WACHEZAJI WA LEICESTER WAOMBA RADHI
Slider

Wachezaji watatu wa timu ya Leicester City ya Ligi Kuu ya England ambao wanadaiwa kuonekana katika mkada wa video wakionyesha vitendo vya ubaguzi wa kimapenzi wameomba radhi kutokana na tabia yao hiyo. Picha ambazo zimekuwa zikiwaonyesha wachezaji Tom Hopper, Adam Smith na James Pearson – mtoto wa kocha Nigel Pearson – walionekana katika gazeti la Sunday Mirror. Mmoja wa wanaume hao katika video hiyo, ambayo ilipigwa nchini Thailand, anasikika kutoa lugha ya matusi ya kibaguzi dhidi ya mwanamke mmoja. Klabu...

Like
241
0
Monday, 01 June 2015
BLATTER ANAWANIA URAIS FIFA
Slider

RAIS  wa shirikisho la soka duniani- FIFA, Sepp Blatter,anagombea kiti cha urais katika uchaguzi wa shirikisho hilo unaotarajiwa kufanyika leo huko Zurich Uswisi. Uchaguzi huo unaendelea katika kongamano la kila mwaka la shirikisho hilo licha ya shinikizo kutoka kwa wadau Blatter ajiondoe kufuatia tuhuma za ufisadi na ulaji rushwa katika shirikisho hilo uliopelekea maafisa wakuu saba kukamatwa mapema juma hili. Blatter anakabiliwa na upinzani mkali kutoka kwa mwana mfalme kutoka Jordan Ali Bin al Hussein....

Like
243
0
Friday, 29 May 2015
UFARANSA YASHAURI KUCHELEWESHWA KWA UCHAGUZI FIFA
Slider

WAZIRI wa Mambo ya nje wa Ufaransa amesema itakuwa ni busara kuuchelewesha uchaguzi wa kumchaguwa rais mpya wa Shirikisho la Soka la Kimataifa FIFA uliopangwa kufanyika hapo kesho kutokana na uchunguzi mpya kuhusu rushwa dhidi ya shirikisho hilo. Akizungumza siku moja baada ya mchezo wa soka kutumbukizwa kwenye machafuko kufuatia kukamtwa kwa maafisa wa FIFA kutokana na madai ya rushwa yaliyotolewa na Marekani Laurent Fabius amesema muda unahitajika ili kuweza kufahamika nini hasa kitakachoendelea....

Like
167
0
Thursday, 28 May 2015
RUSHWA: MAAFISA SITA WA FIFA WAKAMATWA
Slider

MAAFISA  sita wa ngazi ya juu wa shirikisho la kabumbu ulimwenguni FIFA,wamekamatwa na maafisa wa vyombo vya sheria vya Uswisi hii leo mjini Zurich, siku mbili kabla ya mkutano mkuu wa shirikisho hilo. Maafisa hao wanakabiliwa na kitisho cha kuhamishiwa Marekani ambako watakabiliwa na madai ya kuhusika na visa vya udanganyifu, ukandamizaji, na kubadilisha fedha kinyume cha sheria. Kwa mujibu wa idara ya sheria ya serikali kuu ya Uswisi,maafisa hao wa FIFA wanakabiliwa na tuhuma za kupokea rushwa ya mamilioni...

Like
178
0
Wednesday, 27 May 2015
GARETH BALE: NITABAKI REAL MADRID
Slider

Kiungo wa Real Madrid Gareth Bale ameelezea matarajio yake ya kuendelea kubaki ndani ya klabu hiyo msimu ujao, japokuwa kumekuwepo na tuhuma nyingi kutoka kwa mashabiki wa Madrid na baadhi ya vyombo vya habari nchini Hispania kutoridhishwa na kiwango cha mwanandinga huyo ikilinganishwa na pesa zilizotumika kumnunua. Bale ameyasema hayo kupitia ukurasa wake wa twitter huku timu hiyo ikitangaza kuachana na kocha wake Carlo Ancelotti. “nitajituma katika kipindi hiki ambacho msimu umeisha na kutazama mbele juu ya kurejea tena kwenye...

Like
205
0
Wednesday, 27 May 2015
BRENDAN RODGERS: HATMA YANGU IPO KWA WAMILIKI WA LIVERPOOL
Slider

Kocha wa klabu ya Liverpool, England Brendan Rodgers amesema yupo tayari kuondoka klabuni hapo, pale tu wamiliki wa timu hiyo watakapomtaka kufanya hivyo. Liverpool imejikuta ikiaibishwa kwa kukubali kichapo cha bao 6-1 kutoka kwa Stoke City katika mchezo wa kufunga pazia la ligi kuu ya England, lakini pia mchezo huo ndio ulikuwa wa mwisho kwa nahodha Steven Gerrard. “mengi yamepita mwaka huu ambayo yameifanya kazi kuwa ngumu. Msimu uliopita wakati mambo yalipoenda vizuri, tuliungwa mkono na kila mtu, lakini kiwango...

Like
351
0
Monday, 25 May 2015
MALINZI USIONE HAYA KUMPA “MAKAVU” KOCHA STARS
Slider

  Na Omary Katanga. Ni jambo la kuhuzunisha kuona timu yetu ya taifa Taifa Stars,ikigeuzwa kama pombe ya ngomani kila mmoja anajinywea atakavyo,huku maneno ya kutia moyo kutoka kwa viongozi wa shirikisho la mpira nchini TFF yakiendelea kushika hatamu. Tangu mwanzoni uamuzi wa rais wa TFF,Jamali Malinzi wa kuvunja mkataba wa kocha Kim Polsen (Denmark) na kukubali kulipa mamilioni ya shilingi kama fidia ili aondoke na kumleta kocha wa sasa Martin Nooij (Uholanzi),ulipokelewa kwa shingo upande na wadau wa soka....

Like
229
0
Monday, 25 May 2015
SUNDERLAND YAJIKWAMUA KUSHUKA DARAJA
Slider

Klabu ya Sunderland na Arsenal jana wametunushiana misuli baada ya kutoka 0-0 na hivyo kufanikiwa kuondoa mashaka ya kushuka daraja msimu huu katika ligi ya England. Hata hivyo kwa matokeo hayo Arsenal wanashika nafasi ya tatu nyuma ya Manchester City katika ligi hiyo inayomalizika. Hata hivyo katika mchezo huo Sunderland wanapaswa kujilaumu kwa nafasi ambayo walipata na kushindwa kuitumia kupitia mshambuliaji wake Steven Fletcher. Mlinda mlango Costel Pantilimon ndiye aliyeibuka shujaa katika mchezo huo kutokana na uwezo aliouonyesha kwa...

Like
146
0
Thursday, 21 May 2015
RAHEEM STERLING AJIPANGA KUIAGA LIVERPOOL
Slider

Raheem Sterling wa Liverpool anatarajia kumuaga kocha wa klabu hiyo Brendan Rodgers na kuondoka Anfield msimu huu. Mshambulizji huo katika ligi ya England tayari amekwisha saini mkataba mwingine wa kiasi cha Paund laki moja kwa wiki na kukanusha kuwa yeye hana tamaa na pesa,kama alivyohojiwa na BBC. Mchezaji huyo anatarajiwa kukutana na Mkurugenzi wake Ian Ayre na Kocha wake Rodgers siku ya ijumaa,ambapo atakuwa tayari kuwaeleza kuwa sasa anapaswa kuiipa kisogo klabu hiyo. Hata hivyo klabu hiyo ya Liverpool haijataka...

Like
184
0
Tuesday, 19 May 2015
VAN DER GOUW: VALDES NI MBADALA WA DE GEA
Slider

Manchester United tayari ian mtu sahihi wa kusimama mbadala wa David De Gea, hivyo kipa huyo machachari wa Hispania anaweza kwenda kuitumikia Real Madrid hii ni kwa mujibu wa kipa wa zamani wa Manchester Raimond van der Gouw. Man U ilimsajiri Victor Valdes, 33, mapema January na Van der Gouw anaamini kipa huyu anakila sababu ya kuwa kileleni De Gea, 24, amemaliza mkataba wake na Man U katika msimu ujao wa kiangazi richa ya kutosaini mkataba mpya na klabu hiyo....

Like
200
0
Tuesday, 19 May 2015
MALINZI ONDOA PAMBA MASIKIONI,SHUGHULIKIA MALALAMIKO YA VILABU
Slider

Na.Omary Katanga   Ligi kuu msimu wa 2014/15 imemalizika kwa style ya aina yake,malalamiko ya waamuzi kuvibeba baadhi ya vilabu,miundombinu mibovu katika baadhi ya viwanja,adhabu lukuki toka kamati ya usimamizi wa ligi kwenda kwa vilabu na makocha,vimechukua nafasi kubwa. Jambo baya zaidi kutokea msimu huu ambalo halipaswi kuchelewesha utatuzi wake,ni madai ya kuwepo na upulizwaji wa dawa za kunyong’onyesha viungo vya wachezaji katika vyumba vya kubadilishia nguo kwenye uwanja wa Kambarage huko Shinyanga,kitendo kinachodaiwa kufanywa...

Like
251
0
Monday, 18 May 2015