Sports

TIGER WOODS AWEKA MATUMAINI YA KURUDISHA KIWANGO CHAKE
Slider

Aliyekuwa kinara kwenye mchezo wa gofu duniani Tiger Woods ameporomoka katika viwango vya dunia vya mchezo wa gofu baada ya kutolewa katika orodha ya mia bora. Eldrick Tont Woods ambae ni raia wa Marekani hii ni mara kwanza kushuka kiwango katika historia yake ya kipindi cha uchezaji wa mchezo huo. Woods ambaye ni bingwa mara 14 aliingia mia bora kwa mara ya kwanza mwaka 1996 ameweka rekodi ya kuwa bingwa wa dunia kwa wiki 683, lakini sasa ameteremka mpaka nafasi...

Like
189
0
Tuesday, 31 March 2015
LEWIS HAMILTON AONGEZA MKATABA KUITUMIKIA MERCEDES
Slider

Bingwa wa dunia wa mbio za magari Lewis Hamilton anatarajiwa kusaini mkataba mpya wiki hii utakaomwingizia zaidi ya pound milioni 27 kwa mwaka. Hamilton mwenye umri wa miaka 30 raia wa Uingereza amekuwa kwenye mazungumzo na viongozi wa kampuni ya magari ya Mercedes ambapo dili hilo nono kwa dereva huyu lipo kwenye hatua za mwisho kumaliziwa na wanasheria. Hamilton amesema mchakato wa kusaini mkataba huo utamalizika wiki hii wala hakuna sababu itakayokwamisha kwani hakuna makubaliano yaliyoachwa hivyo mchakato huo umekamilika...

Like
219
0
Tuesday, 31 March 2015
AUDIO: DK PANJUAN NA SAKATA LA KUTIMULIWA KWA MTUNZA VIFAA WA TIMU YA TAIFA
Slider

miongoni mwa yaliyojiri kwenye Sports Headquarters leo...

Like
470
0
Monday, 30 March 2015
MALAYSIAN GRAND PRIX: SEBASTIAN VETTEL AMBWAGA LEWIS HAMILTON
Slider

Dereva wa mbio za magari wa timu ya Ferrari Sebastian Vettel raia wa Ujeruamani ameibuka na ushindi kwenye mashindano ya Malaysian Grand Prix baada ya kumbwaga Lewis Hamilton wa timu ya Mercedes. Ushindi huo wa Vettel kwenye michuano hiyo ni wa kwanza katika mashindano hayo akiwa na timu ya Ferrari Ushindi wa mjerumani huyo umemfanya kuwa ndiye dereva mwenye mafanikio makubwa katika eneo la Sepang akiwa na mataji manne Katika pambano hilo lililokuwa na ushindani mkali Hamilton alifanikiwa kushika nafasi...

Like
313
0
Monday, 30 March 2015
TAIFA STARS VS MALAWI
Slider

Katika mchezo wa kirafiki uliochezwa jana kwenye uwanja wa Ccm Kirumba Mwanza kati ya timu ya taifa ya Tanzania (Taifa Stars) na timu ya taifa ya Malawi (The Flames) na kumalizika kwa sare ya kufungana 1-1 wadau wamekuwa na maoni tofauti kufuatia matokeo hayo. Malawi ndio walikuwa wa kwanza kuliona lango Stars katika dakika ya tatu ya mchezo kupitia mchezaji wake Esau Kanyenda goli lililodumu hadi kipindi cha pili cha mchezo. Matumaini ya watanzania waliokuwa wakifatilia mchezo huo yaliletwa na...

Like
275
0
Monday, 30 March 2015
UFARANSA YASHINDWA KUTAMBA MBELE YA BRAZIL
Slider

Richa ya timu ya taifa ya Ufaransa kuanza kuliona lango la Brazil katika dakika ya 21 kwa goli lililofungwa na Raphael Varane, kikosi cha Brazil kilijipanga vyema kuhakikisha wanaondoka na ushindi katika mchezo huo. Bao la kusawazisha la Brazil lilifungwa na Oscar dos Santos Emboaba Júnior katika dakika ya 40 kasi iliongezeka kwa kuindama safu ya ulinzi ya Ufaransa na hatimaye wakaongeza  magoli mengine mawili kupitia kwa Neymar da Silva Santos, Júnior, na Luiz Gustavo na hivyo hadi mechi hiyo...

Like
383
0
Friday, 27 March 2015
KESHI AREJEA KUINOA SUPER EAGLES
Slider

Rais wa shirikisho la soka nchini Nigeria NFF bwana Amaju Pinnick amethibitisha kufanyika kwa mazungumzo na kukubaliana na kocha Stephen Keshi kurejea kuinoa timu ya taifa ya Nigeria Super Eagles. Kocha huyo mwenye umri wa miaka 53 anahistoria ya kuiongoza Super Eagles kutinga raundi ya pili ya kombe la dunia lililofanyika mwaka jana. Keshi amekuwa na kikosi hikcho tangu mwaka 2011 na kuacha kukitumikia alipotoka nchini brazili kwa madai ya kuwa amepata mkataba mwingine. Hata hivyo mzozo katika shirikisho la...

Like
182
0
Friday, 27 March 2015
FA YAPANGA KUANZA MAZUNGUMZO NA ROY HODGISON
Slider

Mwenyekiti wa shirikisho la soka nchini Uingereza Greg Dyke ameonyesha dhamira yakutaka kuanza mazungumzo ya kumuongezea mkataba bosi wa kikosi cha England Roy Hodgson kwa mwaka ujao. Hodgson mwenye umri wa miaka 67 alirithi mikoba ya Fabio Capello mwaka 2012 na kuanza kukinoa kikosi hicho ambacho kwa sasa ndio kinara wa European Championship kwenye hatua za makundi kufuatia ushindi wa michezo yake mine ya awali Mkataba wa meneja huyu kwa sasa unaelekea mwishoni kwenye michuano ya Euro 2016 itakayofanyika nchini...

Like
230
0
Thursday, 26 March 2015
KRIKETI: TANZANIA KUCHUANA NA UGANDA KWENYE MICHUANO YA UFUNGUZI AFRIKA KUSINI
Slider

Tanzania kuchuana na Uganda kwenye mechi ya ufunguzi ya michuano ya Afrika Ligi Daraja la 1 inayotarajiwa kufanyika katika mji wa Benoni huko nchini Afrika kusini Timu teule ya mchezo huo wa Kriketi tayari imeondoka nchini kuelekea Afrika ya kusini kujiandaa na mchezo huo Kikosi hicho cha Tanzania kinaongozwa na nahodha Hamisi Abdallah mwenye uzoefu wa kushiriki michuano ya kimataifa ya mchezo wa kriketi akiichezea Tanzania kwa nafasi hiyo zaidi ya miaka 10 huku akiwa na rekodi ya kucheza kriketi...

Like
229
0
Thursday, 26 March 2015
TWENDE SAWA NA EFM
Slider

Kutokana na mchezo wa ndondi kukua kwa kasi,kituo cha redio cha 93.7EFM kimeamua kusaidia kukuza zaidi mchezo huo nchini. Akipokea msafara uliotoka Afrika ya Kusini na China,Mkuu wa Mahusiano wa ndani wa 93.7 EFM Dennis Ssebo,alisema mda umefika kuendelea kuunga mkono vipaji vya ndani. “Tumeshazungumza na tumekubaliana mbinu mbali mbali za kuendelea kuinua mchezo huu,na ni mikakati gani tutatumia kuendelea kuiweka bendera ya Tanzania katika ramani ya kimataifa”,alisema Ssebo. Mjadala mkali uliendelea katika kipindi cha Sports headaquaters...

Like
499
0
Wednesday, 25 March 2015
STARS KUMENYANA NA MALAWI JUMAPILI
Slider

Timu ya taifa ya Malawi (The Flames) inatarajiwa kuingia nchini hapo kesho siku ya alhamisi ukiwa ni msafara wa watu 25 watakaotua uwanja wa taifa wa Mwl. Jk Nyerere ambapo siku ya ijumaa wanatarajiwa kutua katika jiji la Mwanza tayari kwa mchezo wao wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Stars siku ya jumapili. Afisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Baraka Kizuguto amesema msafara huo utakaokuwa na wachezaji 18 na viongozi 7, kocha mkuu wa The Flames Young Chimodzi...

Like
196
0
Wednesday, 25 March 2015