Sports

PLATINUM FC YAIPONGEZA YANGA KWA USHINDI WA 8-0 DHIDI YA COASTAL UNION
Slider

Katika michezo ya ligi iliyochezwa jana Yanga imeifunza adabu ya timu ya Coastal Union kwakuitandika magoli 8-1. Huenda Yanga iliutumia mchezo huo kama salamu kwa vigogo wa Tunisia Etoile du Sahel, ambao siku za usoni watakutana katika kombe la Shirikisho hatua ya 16 bora. Katika kipindi cha kwanza cha mchezo hadi mapumziko Yanga ilikuwa mbele kwa magoli 3-0. Katika kiindi cha pili cha mchezo Amisi Tambwe alifunga magoli 4, huku Simon Msuva, Salem Telela na Mliberia Kpah Sherman wakiona nyavu...

Like
287
0
Thursday, 09 April 2015
AFCON 2017: STARS YAKABILIWA NA KIBARUA KIZITO
Slider

shirikisho la mpira wa miguu barani Afrika CAF jana limetangaza makundi ya timu yatakayoshiriki kwenye kombe la mataifa Afrika maarufu kama Afcon kwa mwaka 2017 yatakayofanyika huko Gabon. katika makundi hayo timu za Afrika Mashariki hususani Tanzania zina kazi ya ziada kuhakikisha wanapambana vikali kutokana na timu walizopangiwa RATIBA YA MAKUNDI AFCON 2017 Group A: Tunisia, Togo, Liberia, Djibouti Group B: Madagascar, DRC, Angola, CAR Group C: Mali, Equatorial Guinea, Benin, South Sudan Group D: Burkina Faso, Uganda, Botswana, Comoros...

Like
225
0
Thursday, 09 April 2015
SHEPOLOPOLO KUTUA DAR LEO TAYARI KUMENYANA NA TWIGA STARS
Slider

Timu ya soka ya taifa ya wanawake ya Zambia (Shepolopolo) inatarajiwa kuwasili Dar es Salaam leo tayari kwa ajili ya mchezo wa marudiano kati yake na kikosi cha Twiga stars katika mchezo wa kugombania nafasi ya kushiriki michuano ya Afrika mwaka huu inayotarajiwa kufanyika Congo Brazzaville kuanzia Septemba 4-9. Kwenye mchezo huo kikosi cha Twiga stars chini ya kocha Rogasian Kaijage iwapo kitashinda kitakuwa kimefuzu kwenda kwenye fainali hizo kufuatia matokeo ya awali ambapo waliibuka na ushindi wa magoli  4-2...

Like
248
0
Wednesday, 08 April 2015
WIGAN ATHLETIC YAMTANGAZA GARY CALDWELL KAMA MENEJA MPYA WA TIMU HIYO
Slider

Timu ya Wigan Athletic imemtangaza Gary Caldwell kuwa meneja wao mpya akirithi mikoba ya Malky Mackay aliyetimuliwa mapema jumatatu. Mackay kibarua cha kuinoa klabu hiyo kiliota nyasi kufuatia kichapo cha 2-0 dhidi ya Derby katika uwanja wa nyumbani Caldwell aliyekuwa mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Scotland mwenye umri wa miaka 32, ameichezea Wigan michezo 111 lakini pia alikuwa miongoni mwa wachezaji wa kikosi cha timu hiyo kilichotwaa kombe la FA mwaka 2013. Caldwell alitangaza kustaafu mapema kwenye msimu huu...

Like
202
0
Wednesday, 08 April 2015
MCHEZO WA RUGBY WAPAMBAMOTO ARUSHA
Slider

Hizi ndizo team na makundi yaliyogawanywa kwa ajili ya michuano hiyo. Kundi A. Shakaz Irie worriers Buggyz Kundi B. Wakuda Arusha Morans Bokajunior Mashindano yaha ni ya maandarizi yanayoanza 31 May pia niyakujiandaa na mashindano ya safaricom 7s ambayo inafanyika Nairobi Kenya mwezi wa Tisa na Tanzania tunatarajia kupeleka timu ya wasichana na wavulana kwa Mara ya kwanza...

Like
270
0
Tuesday, 07 April 2015
CRYSTAL PALACE YAILAZA MAN CITY 2-1
Slider

Klabu ya soka ya Crystal Palace jana ilifanikiwa kuwaangazmiza mabingwa watetezi Manchester City magoli 2-1 katika mchezo uliuchezwa Selhurst Park.   Ushindi huo wa jana wa klabu ya Cristal Palace ni mafanikio kwa meneja Alan Pardew   Meneja alifunguka na kusema kwamba anaamini kuwa Mameneja katika ligi hiyo hawapati sifa wanayostahiri mara tu wanapozitandika timu kubwa kwa kuwazidi mbinu kimchezo.    ...

Like
271
0
Tuesday, 07 April 2015
YANGA USO KWA USO NA ETOILE DU SAHEL
Slider

Yanga kushuka dimbani kumenyana na Etoile du Sahel ya Tunisia katika raundi ya pili ya michuano ya vilabu ya kombe la Shirikisho barani Afrika. Yanga ambayo inaiwakilisha Tanzania kwenye michuano hiyo imefanikiwa kuwatoa Platinum FC licha ya kufungwa 1-0 katika mechi ya marudiano iliyochezwa Bulawayo, nchini Zimbabwe. Hii inafuatia ushindi wa 5-1 ambao Yanga iliupta katika mechi ya kwanza iliyochezwa hapa Dar es Salaam. Yanga watakuwa na kazi ya ziada kuhakikisha wanaipeperusha vyema bendera ya Tanzania kufuatia rekodi ya klabu ya...

Like
211
0
Tuesday, 07 April 2015
AFCON: MOROCCO YASHINDA BAADA YA KUKATA RUFAA
Slider

Morocco imeshinda kesi baada ya kukata rufaa dhidi ya hukumu waliyopewa na chama cha mpira wa miguu barani Afrika Caf ambapo walifungiwa kushiriki michuano ya mataifa ya afrika Afcon kwa mwaka 2017 na 2019. Mahakama ya usuluhishi wa mambo ya michezo imebadili maamuzi ya Caf baada ya Morocco kukosa nafasi ya kuwa mwenyeji wa fainali za afcon 2015, mahakama hiyo pia imepunguza tozo iliyowekewa timu hiyo dola za kimarekani milioni moja hadi dola 50000. Morocco amabao walipangwa kuwa wenyeji wa...

Like
231
0
Friday, 03 April 2015
RAHEEM STERLING: NAVUTIWA NA KUTWAA MATAJI NA SIO PESA
Slider

Kocha wa klabu ya soka ya Liverpool ya England Brendan Rodgers, amesema Raheem Sterling hataondoka katika klabu hiyo, msimu wa kiangazi japo kuwa mazungumzo kuhusu mpango mpya kati ya mchezaji huyo na vijogoo hao wa Anfield yamevunjika. Sterling mwenye umri wa miaka 20 kwenye mahojiano yake na kituo cha BBC amesema kuwa yeye anavutiwa zaidi kutwaa mataji na wala siyo pesa,maneno ya mchezaji huyo yanakuja baada ya kukataa ushawishi wa mkataba wa kitita cha paundi laki 100,000 kwa wiki. “Liverpool...

Like
268
0
Friday, 03 April 2015
MATOKEO YA MECHI ZA KIRAFIKI KIMATAIFA
Slider

Katika michezo ya kirafiki kwa mataifa usiku wa kuamkia leo , Italy imekuwa mwenyeji wa England Kikosi cha Italy kimekuwa na rekodi yakutofungika kirahisi tokea michuano ya kombe la dunia mchezo huo uliomalizika kwa matokeo ya sare moja ya magoli 1-1 katika michezo mingine iliyochezwa jana Uholanzi ililipa kisasi cha fainali za mwaka 2010, baada ya kuisambaratisha Hispania bao 2-0. Ureno wakicheza bila Christian Ronaldo, walikiona cha moto baada ya kuadhibiwa nyumbani bao 2 kwa nunge dhidi ya Cape Verde,...

Like
383
0
Wednesday, 01 April 2015
MIAMI OPEN: MURRAY AELEZA MATUMAINI YAKE BAADA YA KUTINGA ROBO FAINALI
Slider

Andy Murray amekuwa Mwingereza wa kwanza kuweka historia ya kushinda mara 500 katika mchezo wa tenis baada ya kumshinda Kevin Anderson kutoka Afrika Kusini. Murray alishinda kwa seti 6-4 3-6 6-3 na kuwa mchezaji wa 46 kushinda mara 500 tangu kuanzishwa kwa mashindano ya wazi. Akizungumza na kituo cha BBC Murray alisema amefurahishwa na ushindi huo alioupata huko Miami sehemu ambayo ameitumia kwa muda mrefu kwakufanya mafunzo na kujinoa kwa ajili ya michuano yake, Pia ameongeza kuwa atautumia ushindi huo...

Like
203
0
Wednesday, 01 April 2015