Slider

23% YA WATOTO NCHINI WANASUMBULIWA NA UGONJWA WA MATUNDU YA MOYO
Local News

IMEELEZWA kuwa asilimia 23 ya watoto nchini wanasumbuliwa na ugonjwa wa matundu ya moyo ambao umekuwa ni moja kati ya magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo vingi vya watoto. Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini dar es salaam leo Daktari bingwa wa Magonjwa ya moyo kutoka kitengo cha moyo cha Jakaya Kikwete, Peter Richard amesema kuwa dalili zinazoashiria uwepo wa ugonjwa huo kwa mtoto ni pamoja na kushuka kwa kiwango cha ukuaji na homa kali za mapafu zinazojitokea mara kwa mara....

Like
314
0
Friday, 22 April 2016
TCRA: SIMU BANDIA CHANZO CHA KUUNGUZA NYUMBA
Local News

MAMLAKA ya Mawasiliano Nchini-TCRA-imesema kuwa asilimia 79 ya simu za mkononi zilizofanyiwa utafiti kwa kipindi cha mwezi disemba mwaka jana hadi Februari mwaka huu sio bandia wakati asilimia 18 ya simu hizo ni bandia. Aidha imeeleza kuwa asilimia kubwa ya nyumba zinazoungua kwa umeme kunatokana na simu bandia ambazo betri zake au vifaa vyake hushindwa kuhimili mionzi wakati zinapokuwa zinachajiwa hivyo kusababisha moto. Hayo yamesemwa na meneja uhusiano wa mamlaka hiyo Innocent Mungi wakati akizungumza katika semina ya mfumo wa...

Like
238
0
Friday, 22 April 2016
VOLKSWAGEN YATANGAZA KUNUNUA MAGARI YAKE
Global News

KAMPUNI ya magari ya Volkswagen imetangaza kuyanunua magari ya kampuni yake kutoka kwa wateja nchini Marekani yapatayo laki tano kama sehemu ya kutimiza makubaliano yaliyoafikiwa na idara ya sheria ya Marekani dhidi ya kampuni hiyo kuhusika na kashfa ya uchafuzi wa hali ya hewa. Jaji kutoka San Francisco hajabainisha wazi kiasi ambacho wamiliki wa magari hayo watalipwa na kampuni ya Volkswagen pale watakapo iuzia kampuni hiyo magari yake wanayoyamiliki. Makubaliano mengine yaliyofikiwa ni kwamba Volkswagen itatakiwa kutoa fungu la fedha...

Like
197
0
Friday, 22 April 2016
OBAMA AISIHI UINGEREZA ISIJITOE EU
Global News

RAIS wa Marekani Barack Obama amesema anaunga mkono Uingereza kubaki katika jumuiya ya Umoja wa Ulaya ili kuweza kuchangia katika vita dhidi ya ugaidi na masuala ya wahamiaji na utatuzi wa migogoro ya kiuchumi. Rais Obama amenukuliwa na gazeti la Uingereza la Telegraph, akisema kwamba uanachama wa Uingereza katika umoja wa Ulaya una umuhimu mkubwa na endapo nchi hiyo itajiondoa katika umoja huo itapunguza nguvu katika vita dhidi ya ugaidi duniani. Hata hivyo Obama amesema anatetea hoja ya umoja wa...

Like
227
0
Friday, 22 April 2016
KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI, UTALII, UTAMADUNI NA MICHEZO WA SERIKALI YA MAPINDUZI AAHIDI KUTOA HUDUMA BORA
Local News

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Omar Hassan Omar amesema atahakikisha anasimamia na kutekeleza adhima ya Serikali hiyo ya kuwapatia wafanyakazi wake huduma bora ili waweze kutekeleza kazi zao kwa ufanisi. Mheshimiwa Omar Hassan Omar ameyasema hayo baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi na Katibu mkuu aliyemaliza muda wake Ali Mwinyikai katika ukumbi wa Wizara iliyopo Mnazi mmoja visiwani. Amesema utendaji kazi wa Serikali ni wa pamoja  na sio mtu mmoja mmoja hivyo amewaomba viongozi...

Like
209
0
Friday, 22 April 2016
WATENDAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA WATAKIWA KUTEMBELEA MAENEO YAO YA KAZI
Local News

NAIBU waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa Selemani Jafo amewataka watendaji wa mamlaka za serikali za mitaa kuwa na utaratibu wa kutembelea maeneo yao ya kazi ili kujua changamoto zilizopo na kuzitatua. Akizungumza na walimu wa shule ya msingi Nzuguni B mkoani Dodoma wakati wa ziara aliyoifanya Mheshimiwa Jafo amesema kuwa watumishi hawawezi kufanya kazi kwa ubora iwapo hawatakuwa wakitembelea na kukagua maeneo yao ya kazi. Katika ziara yake amewataka walimu wa...

Like
181
0
Friday, 22 April 2016
KENYA YAITAKA ICC KUIKABIDHI FAILI ZA WASHUKIWA 3
Global News

KENYA sasa inataka faili za kesi zinazowakabili wakenya watatu wanaotuhumiwa kuingilia ushahidi wa mashahidi wa ICC kushtakiwa nchini humo. Mwanasheria mkuu Profesa Githu Muigai amesema kuwa Kenya ina mahakama zilizo na uwezo za kushtaki kesi ndogo kufuatia kuanguka kwa kesi kuu iliowahusisha wakenya sita maarufu kama Ocampo 6. Mwanasheria huyo pia ameshtumu idara ya mashtaka katika mahakama ya ICC kwa kushindwa kushirikiana na Kenya kuhusu ombi la awali lililowasilishwa kwa aliyekuwa kiongozi wa mashtaka Moreno Ocampo kuikabidhi Kenya faili...

Like
177
0
Thursday, 21 April 2016
KANALI WA JESHI AUAWA BURUNDI
Global News

KANALI mmoja wa Jeshi amepigwa risasi na watu wasiojulikana katika mji mkuu wa Burundi ,Bujumbura,kulingana na vyombo vya habari vya kundi la SOS nchini humo. Kanali Emmanuel Buzubona aliuawa pamoja na mtu mmoja aliyekuwa akiendesha pikipiki siku ya Jumatano kaskazini mwa makaazi ya mji huo. Ni miongoni mwa maafisa wa jeshi wa hivi karibuni kuuawa tangu rais Pierre Nkurunziza kunusurika jaribio la mapinduzi na maandamano kufuatia hatua yake ya mwaka jana kujiongezea muda wa kuhudumu kama rais wa taifa...

Like
225
0
Thursday, 21 April 2016
UCHAGUZI MKUU 2015: WADAU WAIPONGEZA NEC
Local News

WADAU mbalimbali kutoka vyama vya Siasa vilivyoshiriki katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika Octoba 25 mwaka jana wameipongeza Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kwa kuendesha zoezi hilo kwa Uwazi, Haki, Amani na kwa kuzingatia Sheria na Kanuni. Hayo yamesemwa leo na Katibu Mkuu wa Chama cha NRA Hassan Kasabya alipokuwa akitoa pongezi kwa Tume hiyo kwa kutoa vyeti vya shukrani kwa washiriki hao kutoka vyama vya siasa na wadau...

Like
210
0
Thursday, 21 April 2016
MKUU WA WILAYA YA KINONDONI AAPISHWA RASMI LEO
Local News

MKUU wa mkoa wa Dar es salaamu mheshimiwa PAUL MAKONDA leo amemuapisha rasmi mteule mkuu wa wilaya ya kinondoni ALY SALUM HAPI ambapo amemtaka kuhakikisha anakuwa mstari wa mbele kutimiza matakwa ya mheshimiwa rais ikiwemo kupinga ufisadi na rushwa . Awali akizungumza mbele ya watendaji ,wakuu wa wilaya na wakuu wa ulinzi na usalama, mheshimiwa PAUL MAKONDA amesema licha ya kuwa na umri mdogo inatakiwa atumie nafasi alio aminiwa na mheshimiwa rais kutekeleza majukumu hasa kuhakikisha kunakuwepo na haki kwa...

Like
290
0
Thursday, 21 April 2016
YANGA, TP MAZEMBE NJE MICHUANO YA KLABU BINGWA AFRIKA
Slider

Wakicheza Ugenini huko Nchini Misri, Yanga wamefungwa 2-1 na Al Ahly na kuondolewa katika michuano ya klabu bingwa Africa. Mabingwa watetezi Tp Mazembe wakaondolewa katika michuano hiyo baada ya sare ya 1-1 dhidi Wydad de Casablanca, na Casablanca wakisonga mbele kwa ushindi 3-1. Enyimba wakasonga mbele kwa ushindi wa penati 4-3 dhidi ya Etoile du Sahel ,As Vita Club nao wakasonga mbele licha ya kufungwa kwa mabao 2-1 na Mamelod Sundowns . Al Ahli Tripoli wakawachapa Asec Mimosas kwa mabao...

Like
299
0
Thursday, 21 April 2016