Slider

WAKIMBIZI ZAIDI KUREJESHWA UTURUKI LEO
Global News

KUNDI la pili la wahamiaji wanatarajiwa kurejeshwa nchini Uturuki kutoka Ugiriki baadaye hii leo, kama sehemu ya mkataba ulioafikiwa na Muungano wa Ulaya, wa kupunguza idadi wa wakimbizi wanaofika Ulaya.   Kundi la kwanza liliwasili Uturuki, siku ya Jumatatu, lakini tangu wakati huo mpango huo umekwama kwa sasa ambapo idadi kubwa ya wahamiaji wanaomba hifadhi nchini Ugiriki.   Inaaminika kuwa boti zingine mbili zitawasili leo, Ijumaa, ikiwa na wahamiaji waliofukuzwa kutoka Ugiriki chini ya mkataba huo wa...

Like
211
0
Friday, 08 April 2016
WAASI WAPAMBAN NA IS SYRIA
Global News

VIKOSI vya waasi wa Syria wamevirejesha nyuma vikosi vya wanamgambo wa dola ya kiislamu wa Islamic State nje ya mji ambao pande zote mbili wanauwinda kuwa chini ya himaya yake upande wa Kaskazini mwa Syria, baada ya siku kadhaa za mapambano makali.   Mji wa Al-Rai,ulioko jirani na jimbo la Aleppo ,ni ngome ya wanamgambo hao wa IS ambao uko kwenye mpaka unaoingia nchini Uturuki hadi kuingia Syria.   Waasi hao wa Syria wamewahi kuhusika na matukio ya kukera ingawa...

Like
256
0
Friday, 08 April 2016
WADAU WA MAENDELEO YA ELIMU WASHAURIWA KUTOA VIFAA VYA KUJIFUNZIA NA KUFUNDISHIA
Local News

WADAU wa Maendeleo ya Elimu nchini wameshauriwa kutoa vifaa vya kujifunzia na kufundishia kwa walimu na wanafunzi wa shule mbalimbali nchini ili kukuza kiwango cha elimu nchini.   Aidha wameshauriwa pia kuboresha miundombinu ya shule hali ambayo itaboresha pia mazingira ya kujifunzia.   Ushauri huo umetolewa na Mbunge wa Segerea Bonna Kaluwa mara baada ya kukabidhi msaada wa kompyuta kwenye shule ya sekondari ya Binti Mussa iliyopo Manispaa ya Ilala Jijini Dar Es Salaam.  ...

Like
236
0
Friday, 08 April 2016
VYOMBO VYA HABARI VIMETAKIWA KUANDAA VIPINDI VYA KUELIMISHA JAMII
Local News

VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kuandaa vipindi vya kuelimisha na kupunguza burudani kwa kuongeza idadi ya vipindi vya kujenga uzalendo, amani, mshikamano pamoja na umoja wa kitaifa.   Rai hiyo imetolewa na Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano (TCRA) Kanda ya Ziwa Enjinia. Lawi Odieri wakati wa ziara ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye alipokutana na wadau wa sekta anazozisimamia Mkoani Simiyu.   Naye mheshimiwa Nauye amesema kuwa uwepo wa vituo vya kutosha vya utangazaji katika...

Like
355
0
Friday, 08 April 2016
GWIJI WA SOKA BARANI AFRIKA NWANKWO KANU AFANYA EXCLUSIVE INTERVIEW NDANI YA EFM REDIO
Slider

Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Nigeria na club za Ajax, Inter Milan, Arsernal, na Portsmouth Nwankwo Kanu ambaye pia ni balozi wa Startimes akiwa katika kituo cha EFM REDIO kwa ajili ya kufanya mahojiano ya moja kwa moja katika kipindi cha SportsHeadquarters. Mtaalamu huyo wa mpira wa miguu akizungumza jambo katika studio za EFM redio Nwankwo Kanu akiwa katika mahojiano studio za EFM redio kwenye kipindi cha sports headquarters. Watangazaji wa sports headquarters katika picha ya pamoja na Nwankwo...

Like
1185
0
Thursday, 07 April 2016
UTAWALA WA SERIKALI YA KIDINI TRIPOL WAKABIDHI MAMLAKA KWA VIONGOZI WANAUNGWA MKONO NA UN
Global News

UTAWALA wa serikali ya kidini katika mji mkuu wa Tripol nchini Libya umekabidhi mamlaka kwa viongozi wanaoungwa mkono na Umoja wa Mataifa. Uamuzi huo ulichapishwa katika mtandao wa wizara ya sheria. Mamlaka mpya ya Libya wiki iliyopita imehamia mji mkuu,Tripoli katika harakati za kutaka kutawala nchi nzima, huku kukiwa na ngome nyingine mbili tofauti za utawala Mashariki mwa nchi hiyo. Hatua hii ni matokeo ya jitihada za umoja wa mataifa kuunda serikali ya pamoja ili kuweza kuondoa mgawanyiko wa utawala...

Like
208
0
Wednesday, 06 April 2016
TED CRUZ AMBWAGA TRUMP JIMBO LA WISCONSIN
Global News

MGOMBEA urais wa chama cha Republican nchini Marekani Ted Cruz ameshinda mchujo wa chama hicho katika jimbo la Wisconsin, hilo likiwa pigo kubwa kwa Donald Trump. Katika chama cha Democratic, Bernie Sanders alipata ushindi mkubwa dhidi ya Hillary Clinton anayeongoza kwa wajumbe kwa sasa. Bw Trump anaongoza kwa wajumbe na katika kura za maoni chama cha Republican, lakini kuna wasiwasi kwamba huenda akashindwa kupata wajumbe wa kumuwezesha kuidhinishwa moja kwa moja kuwa...

Like
247
0
Wednesday, 06 April 2016
HALMASHAURI NCHINI ZAAGIZWA KUAJIRI MAAFISA HABARI
Local News

SERIKALI imeagiza kila mkoa na kila Halmashauri nchini kuajiri Maafisa wa Habari na kuwapa nafasi ya kushiriki katika vikao vyote vya maamuzi pamoja na kutenga bajeti kwa ajili ya shughuli za maafisa habari ili kuboresha mawasiliano ndani ya serikali na mawasiliano ya serikali na umma.   Kauli hiyo imetolewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Michezo na Sanaa, Nape Nauye, wakati wa ziara yake ya siku moja mkoani Kigoma, aliyoifanya kwa ajili ya kutembelea idara zilizo chini ya wizara yake ambapo...

Like
213
0
Wednesday, 06 April 2016
3 WAFUNIKWA NA KIFUSI KAWE
Local News

MTU mmoja anasadikiwa kufariki dunia na wengine watatu kujeruhiwa mara baada ya kuangukiwa na kufunikwa na kifusi katika chumba kimoja   maeneo ya Kawe Ukwamani, jijini Dar es salaam . Akizungumzia tukio hilo Mwenyekiti wa serikali ya mtaa wa Kawe Ukwamani SULTANI JETA amesema mnamo alfajiri ya leo kulisikika mshindo ambao ulitokana na ukuta kudondoka na kuwafunika watu wan ne wa familia moja wakiwepo watoto wawili ,mtu mzima mmoja na msichana mmoja mwenye umri wa miaka kumi na mbili ambao wote...

Like
321
0
Wednesday, 06 April 2016
RAIS WA YEMEN AWATIMUA KAZI WAZIRI MKUU NA MAKAMU WA RAIS
Global News

RAIS wa Yemen Abedrabbo Mansour Hadi amemfukuza kazi Waziri Mkuu na Makamu wa Rais wa nchi hiyo Khaled Bahah kutokana na kile alichoeleza utendaji mbovu ndani ya serikali. Mabadiliko haya yanakuja ikiwa ni wiki moja kabla ya kuanza kwa hatua ya kusimamishwa mapigano kati ya pande mbili zinazohasimiana katika mgogoro nchini humo. Kwa mujibu wa taarifa iliyotangazwa na shirika la habari la serikali nchini humo, Rais Hadi amemteua Ahmed Obaid bin Daghr kuwa waziri mkuu huku akimteua Meja Jenerali Ali...

Like
213
0
Monday, 04 April 2016
SYRIA:VIKOSI VYADHIBITI MJI WA AL-QARYATAIN
Global News

VIKOSI vya Jeshi nchini Syria na washirika wake vimedhibiti tena mji wa Al-Qaryatain kutoka mikononi mwa Islamic State, ukiwa ni muendelezo wa mapambano dhidi ya kundi hilo. Hatua hiyo imekuja siku kadhaa baada ya kundi la IS kuondolewa katika eneo la karibu na mji wa Palmyra. Wanamgambo wa IS waliuteka mji wa Al-Qaryatain mwezi Agosti, na kuwateka mamia ya wakazi wa mji huo wakiwemo Wakristo ambao wengi wao waliachiwa huru...

Like
184
0
Monday, 04 April 2016